Ticker

6/recent/ticker-posts

TAASISI YA KURITHI ICTR KUANZA KAZI RASMI JUMATATU IJAYO

Taasisi ya Kimataifa itakayorithi kazi zitakazoachwa na Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) mjini Arusha,Tanzania,itaanza kazi rasmi Jumatatu ijayo.
Miongoni mwa kazi za taasisi hiyo ijulikanayo kwa kifupikama IRM ni pamoja na kuendelea kuwasaka watuhumiwa watatu maarufu ambao bado hawajatiwa mbaroni, akiwemo mtu anayesadikiwa kuwa ndiye mfadhili wa mauaji hayo,Felicien Kabuga.
Kabuga anakabiliwa na mashitaka ya mauaji ya kimbari ikiwa ni pamoja na madai kwamba alinunua mapanga ambayo yanadaiwa kutumika kwa kiasa kikubwa katika mauaji dhidi ya Watutsi wakati wa mauaji hayo mwaka 1994.Mshitakiwa huyo ni ndugu yake aliyekuwa Rais wa Rwanda Juvenal Habyarimana.
Washitakiwa wengine wawili waliobaki ni pamoja na Waziri wa Ulinzi wa zamani waRwanda, Augustin Bizimana na aliyekuwa Kamanda wa Walinzi wa Kikosi cha Rais, Protais Mpiranya.
Naye Mwendesha Mashitaka wa ICTR, Hassan Bubacar Jallow Julai 2, 2012 pia atakuwa Mwendesha Mashitaka wa IRM. Alikuwa kila mara akitoa wito kwamba ‘’vigogo’’ hao washitakiwe na mahakama ya kimataifa. ICTR imeshasikiliza ushahidi maalum kuhusu watu hao watatu ambao bado wanatafutwa ili ushahidi huo uweze kutumika hapo baadaye iwapo watatiwa mbaroni.
‘’Kuwasaka washitakiwa vigogo hao watatu kutaendelea kuwa changamoto huku zikiwepo taarifa zinazomhusisha Kabuga kuwa yuko nchiniKenya, Mpiranya yukoZimbabwena Bizimana anatajwa kuwa yupo katika maeneo mbalimbali ya kanda hiyo pia,’’ Jallow alisema katika hotuba yake aliyoitoa Juni 7, mbele ya Umoja wa Mataifa (UN).’’ Ni muhimu kwa kuzingatia suala la amani na haki, nchi zote ziunge mkono juhudi za ICTR katika kuwasaka watuhumiwa hao,’’ alisema.
Baadhi ya vyanzo vya habari vinadai kwamba Bizimana na Mpiranya wamekufa lakini Ofisi ya Mwendesha Mashitaka inakana. Kwa mujibu wa mwendesha mashitaka madaikamahayo ni ujanja wa kuwasaidia watu hao kukwepa mkondo wa sheria.
Wapo watuhumiwa wengine sita wa ICTR wa ngazi ya chini ambao pia bado wanasakwa. Mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa pia imeanza kuhamisha majalada ya kesi nyingine za watuhumiwa kwenda kusikilizwa nchini Rwanda kama sehemu ya mkakati wa kuhitimisha kazi za mahakama hiyo.Kazi ya kuwasaka watuhumiwa sita hao sasa itakuwa chini ya Ofisi ya Mwendesha Mashitaka Mkuu nchini Rwanda.Watu hao sita wanajumuisha Luteni Kanali mmoja, mameya wa zamani watatu, inspekta wa zamani wa polisi na mmiliki wa mgahawa.

Post a Comment

0 Comments