Ticker

6/recent/ticker-posts

CUF WATIKISA ARUSHA,DIWANI ALIYEFUKUZWA CHADEMA AJIUNGA NAO.


mwanachama mma mjane akipokea kadi ya uwanachama wa  CUF katika mkutano uliofanyika jijini Arusha

KAti kati ni aliyekuwa diwani wa kata ya elerae John Bayo ambapo alirudisha kadi ya chadema na kurudi katika chama chake cha awali CUF

CHAMA cha wananchi (CuF)  jana kimeuteka mji wa Arusha baada ya kufanya mkutano mkubwa wa hadhara katika uwanja wa Levolosi jijini hapa na kuwataka wakazi Arusha kutowachagua viongozi wanaowapatia vijana pombe za viroba na konyagi  kwa lengo la kufanya vurugu.

Katika mkutano huo diwani wa kata ya Elerai aliyefukuzwa ndani ya Chadema,John Bayo alijiunga rasmi na chama hicho huku akitaja sababu iliyomfaya ajiunge ni baada ya kuona chama hicho kinaendeshwa kwa rimoti na mbunge  wa amani wa jinmbo la Arusha mjini,Godbless Lema.

Akihutubia umati wa watu waliofurika katika viwanja hivyo,mwenyekiti wa Cuf taifa,Prof Ibrahim Lipumba aliwataka wakazi wa Arushakutowapa fursa baadhi ya viongozi wa kisiasa mkoani Arusha mabo wamekuwa wakihamasisha vurugu na mauaji.

Biala kutaja majina yao hadharani Lipumba alisema kwamba baadhi ya viongozi wa kisiasa mkoani  Arusha wameshindwa kusimamia maaadili ya uongozi na badala yake wamekuwa wakiwapa pombe za viroba na konyagi vijana ili wafanye vurugu.

“Wengine wanawapa vijana viroba na konyagi wafanye vurugu tunahitaji viongozi wenye kuisimamia Arusha  sio wanaowapa viroba wafanye vurugu”alisema Lipumba huku akishangiliwa na wafuasi wa Cuf

Hatahivyo,aliusifia mji wa Arusha kwamba ni mji wa kitalii duniani na inachangia pato kubwa kla taifa lakini amani ndiyo imekuwa ikitia doa katika uso wa dunia.

Alisema kwamba rasilimali za taifa kama madini ya Tanzanite yaliyopo Mererani mkoani Manyra yamekuwa hayatumiki ipasavyo pamoja na kutajirisha nchi nyingine huku akisema kwamba ni lazima wapatikane viongozi wa kusimamia rasimali hizo.

Hatahivyo,aliponda sera ya majimbo inayotamkwa na Chadema huku akisema kwamba sera hiyoitachagia mpasuko kwa taifa na kudai wao sera yao ni kuwaunganisha watanzania bila kuwabagua wanakotoka.

Naye,katibu mkuu wa chama hicho ambaye ni makkamu wa kwanza wa Rais Zanzibar,Maalim Seif Sharif Hamad akihutubia viwanjani hapo alilaani baadhi ya vyama vya siasa na wanasiasa kutumia nguvu kazi ya vijana vibaya kwa kuwapa pombe za viroba badala ya kuwajenga kiuchumi.

Alitoa rai kwa wanasiasa nchini na mkoani Arusha kufanya siasa za kistaarabu kwa kuwa amani iliyopo kwa sasa pindi ikitoweka itawagharimu watanzania kuirudisha na watahukumiwa na damu iliyomwagika ardhini.

 Naye,naibu katibu mkuu wa chama hicho upande wa bara,Julius Mtatiro aliutumia mkutano huo kumshambulia aliyekuwa mbunge wa jimbo la Arusha mjini,Godbless Leman a kumtaka aache kuwatumia vijana wa Arusha kufanya vurugu na badala yake awasaidie kimaendeleo.

Mtatiro,alipinga madai ya udini ambayo baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakiinyoshea Cuf na kusema kwamba kule alikozaliwa mkoani Mara waislamu na wakristio wanaishi kwa amani kama ndugu na kudai chama chao kina madiwani katika wilaya za mkoani humo ambao ni waislamu na wanashirikiana bila ubaguzi na wa dini nyingine.

Katika hatua nyingine chama hicho kilitangaza kuweka kambi mkoani Arusha hadi kieleweke kwa lengo la kukieneza chama hicho huku kikisema kwamba uwekaji wa kambi Arusha utakifanya kiifikie mikoa ya Klimanjaro,Tanga na Manyara kwa urahisi.

Post a Comment

0 Comments