NDUGU YANGU MWENYE KUPENDA,CHONGO HUONA KENGEZA/MAMA
FATU AKATESWA KULE SINZA,AKAZUNGUKA NA MJI HUKU AKITOKWA
MACHOZI,AKIKONDA,AKIDHANI DUNIA IMEMPA KISOGO NA SIYO YAKE BALI YA
WENZAKE.NAKUTANA NA MAMA FATU USO KWA USO PALE MWENGE DAR ES
SALAAM,ANANIKIMBILIA NA KUNIKUMBATIA,ANAONEKANA KAMA NI MTU ASIYEAMANI KAMA
TUMEONANA,ANALIA KWA FURAHA YA KUONANA NAMI.PIA NAMSHIKILIA VYEMA NGUO ALIZOVAA
ZISIMDONDOKE KWANI ALIKUWA KAMA AMEINGIWA `MAJUNUNI`.NAMSIHI ANIACHIE KWA MUDA
HUO KISHA TUSABAHIANE,,ANAZIDI KULIA..WAJA WAPITA NJIA WANATUTAZAMA KWA MACHO
TELE..NAMSHIKA MAMA FATU MIKONO NA KUMPELEKA KATIKA HOTELI MOJA ILIYOPO
JIRANI,ANAAGIZA SODA YA BARADI.ANAZIDI KULIA NA KUTETEMEKA.DHAHIR ALIONEKANA
ANAHITAJI MSAADA WA MAWAZO HARAKA..UMRI WAKE NA WAKE NI VITU VIWILI TOFAUTI
LAIKINI ALIAMINI NAWEZA KUMSAIDIA NA KUMNASUA KATIKA TOPE ZITO LA MAHABA BATILI
YANAYOELEKEA KUMTOA UHAI..AMEPIGWA NA MAPENZI.NAMTAZAMA KATIKA MBONI YA MACHO
YAKE,NAONA WEKUNDU NA MACHOZI YANAMWAIKA..MDOMO UNAMTETEMEKA..SODA ALOAGIZA
BADO HAJAWEKA KINYWANI..NATOA KITAMBAA NA KUMFUTA MACHOZI,,HUKU NIKIMSIHI AWE
MVUMILIVU NA KUNIJUZA `KULIKONI`.MWILI NILOMKUTA NAO MAMA FATU SI
WAKWAKE..MACHO YAKE MALEGEVU YAPO PALEPALE.ANATAMKA NENO MOJA ``NDOA` NA KUANZA
KULIA TENA..ANAJIVUTA NA KUVUTA PUMZI NDEFU KISHA ANATAMKA NENO LA PILI
``MAPENZI``KISHA ANALIA TENA KWA SAUTI KUU ..NAPATA TASWIRA KUWA TAYARI
KESHAPIGWA NA MAPENZI NDANI YA NDOA..NAVUTA KUMBUKUMBU NAMUONA MAMA FATU MWENYE
UMBO KUBWA NA ZURI MIAKA SABA ILIYOPITA KULE ARUSHA..NAMUONA MAMA FATU AKIWA NA
TABASAMU PANA ULIYOAMBATANA NA MWANYA,NAONA USO WAKE WA JAMALA,,SAUTI YAKE YA
`KIBARAWA` MITHILI YA MWIMBAJI MALIKA KULE MOMBASA.MACHO YAKE MAKUBWA
YALOZUNGUKWA NA WEUSI MITHILI YA MWIMBAJI WA TAARAB BI.MWANAHELA KULE TANGA..NAZIDI
KUONA SURA YA MAMA FATU YA MIAKA 7 ILIYOPITA NA KUINAMISHA KICHWA CHINI (
SUBB-HANNAH-LAAH)…HAIBA IMEPOTEA UZURI UMEMTOKA,MALI IMEANGAMIA MARADHI
HAYAKUMTOKA,MSIPENDE UGENINI MTAINGIA HATIANI,KUPENDA KITU ADHIMU NAWAMBIA KUNA
DAWA..MSIKILIZE MAMA FATU KISHA TUMSAIDIE…
KIla nikiwaangalia wanangu Fatu na abdi
nashindwa namna ya kudai talaka kutoka kwa mume wangu Rama.Watoto wangu
wakilelewa na mwanamke mwingine sidhani kama watapata haki zao na hata kusoma
hawatosoma.
Kama tabu ni mauti leo mimi faudhia`mama fatu
`nisingalikuwepo.Kucha kutwa mume wangu anashinda baa,mshahara akipata ndiyo
nyumba anaihama kabisa.Siku moja mchana wa ijumaa nilikaa sebleni na radio
yangu nikiskiliza.hewani mtangazaji aliweka nyimbo ya marehemu Marijani
Rajabu na nyimbo yenyewe iliitwa ukewenza,..niliskiliza mashairi ya ule wimbo
,,hakika yaliniingia na nikaanza nami kuimba kwakuifuatisha...unitizame
..nilivyokondaaa,,sababu ya ukewenzaa...ukewenza mimi sitaki jama sitaki
mamaa,,,,)
Punde nyimbo hiyo ikiwa hewani akaingia Baba fatu.Hapo
ni baada ya kutokuonekana kwa siku kumi akidai gari kubwa analoendesha kwenda
mikoani kuharibikia chalinze akiwa anarudi akitokea Arusha.Nilimpa pole naye
akaitikia asante.Aliomba maji ya kunywa nikampatia.alivyomaliza maji akaniuliza
habari za watoto nami nikamjibu kuwa hawajambo,akauliza wako wapi sasa?
Nikamjibu Fatu yupo shule na Abdi ameenda katika mizunguko yake huko kupiga
piga `debe`..
Hakika kama kuna jambo ambalo sitolisahau ni hili la
mimi kumpenda mume wangu kupita kiasi.
nadhani pia upendo wangu kwake ndiyo uliyosababisha
mimi kuteseka kiasi hiki.Nilimwekea maji ya kuoga akaenda kuoga aliporudi
tukakaa mezani nikatenga chakula kisha tukaanza kula.
Tukiwa mezani kwa mbali niliweka taarab asilia,mwimbaji
alikuwa ni bi shakila saidi,nyimbo iliitwa mapenzi yamepungua ```mapenzi
yamepunguaa,,mimi nimeshayaona..kila nikiyaachunguaa,,hatwishii
kuoneanaaa..mapenzi yamepunguaaa) Niliweka kanda ile kwa sababu maalum)
kwakuwa mume wangu alibadilika,mapenzi yake kwangu yalishaanza
kupungua,,nilianza kupata shaka.Yeye nadhani hakuelewa ni kwanini nimeiweka
nyimbo ile ambayo niliipenda sana.Wakati tunakula simu yake iliita,,aliangalia
kisha akaichukua na kuingia chumbani.Alimaliza kuongea na simu hiyo kisha
akarejea na kuendelea kula.Sikumuuliza chochote.Baada ya wiki mbili,mume
wangu alirejea akanambia amefukuzwa kazi kwasababu gari alilokuwa akiendesha
limeibiwa baadhi ya vifaa alipokuwa amelipaki na boss wake amemwachisha kazi
kwasababu ya uzembe.
Hakika niliumia sana tena pengine kuliko hata mume
wangu.Niliwaza mimi sina kibarua ni mama wa nyumbani,tuna watoto
wanasoma,nyumba niya kupanga,tutaishi vipi yailahh kwakuwa hata wakati akiwa na
kazi bado maisha yalikuwa ni magumu na tulikuwa tukilala na njaa wakati
mwingine.
Nililia sana ila sikusahau kusali na kumuombea mume
wangu apate kazi nyingine.Mimi nilikuwa nikicheza `kibati` na akina mama
wenzangu ,nilipopokea shilingi milioni moja niliacha kucheza ili nijue
nitaitunza vipi familia yangu na mume wangu mpaka atakapopata kazi .
Nilipopata ile fedha nikaanza kuuza vitumbua na
chapati nje ya nyumba yetu.Maisha yaliendelea huku mume wangu akiendelea
kutafuta kazi nyingine bila mafanikio.
AKirudi katika mizunguko yake anakuta chakula na watoto
wanafuraha kama kawaida,nilihakikisha najibana na kuzalisha fedha izo ili
tuweze kuishi.Siku moja nikiwa napika chapati nje ya baraza letu alikuja mtu
mmoja wa makamo akiwa na gari aina ya Suzuki vitara,alisimamisha gari lake na
kunambia nimletee chapati tano nilimfungia na kumpelekea,akanipa fedha
zangu,nikiwa narudi akanipigia honi,nilipogeuka akaniita tena,nikaenda,akaanza
kuniuliza naitwa nani,nikamwambia naitwa mama fatu,akanambia nimpe jila langu
kamili nikamwambia naitwa Faudhia,akasema anashkuru kunifahamu nayeye akanambia
anaitwa Hamza,nami nikamwambia nashukuru kumfahamu mteja wangu mzuri wa
chapati.
Akanambia anaomba namba zangu za simu,,nikamwangalia
kisha nikaguna.mmh.nikamuuliza za nini jamani wakati kila ukija hapa kununua
chapati unanikuta mimi? Akanijibu kuwa anaomba tu namba za simu kwakuwa kuna
jambo jingine anataka kunambia kwa njia ya simu.Nikamwambia mimi nimeolewa na
mume wangu huwa anafuatilia sana simu yangu..akanambia nisiwe na shaka kwakuwa
anafahamu kama nina mume hivyo atatumia vizuri namba zangu..nilimpatia namba
zangu.Aliendelea kupita mara kwa mara na kuja kununua chapati asubuhi huku
akinisabahi na kupita.Wakati huo nilikuwa na jukumu kubwa la kuitunza familia
yangu na mume wangu pia nilibeba jukumu la kumtunza.Siku moja mchana Hamza
alinipigia simu akaniomba jumapili tuonane mjini.Nikamuuliza kuna nini ,akasema
anaomba sana nisimwangushe tukutane mjini kuna suala muhimu anataka kuongea
nami.Nikamwambia aongee katika simu nitamwelewa.akakataa ,nami nikakataa
kumfuata mjini.
Alikata simu lakini baada ya dakika tatu alipiga
tena,akanambia mbona mimi nakuwa kama siyo mtu mzima simwelewi? Nimkamwambia
aseme tu nitamwelewa,,akasema amenipenda sana yupo tayari kufanya lolote
anipate hata ikibidi kuishi pamoja kwakuwa yeye bado hajaoa.
Nikamwambia anisamehe sana mimi nimeshaolewa na
ninampenda sana mume wangu sipo tayari kumsaliti licha ya kuachana
naye.`kwakweli nampenda sana mume wangu ni kifo tu ndiyo kitatutenganisha wala
sitomwacha nilimkatia simu na kuingia chumbani kwangu,alipiga simu tena
nikakata.Nilitafuta kanda za mwanamuziki marijani rajabu nikaanza kusikiliza
ili kuondoa mawazo kwakuwa nilimpenda sana marehemu marijani rajabu..
niliweka nyimbo ya `mpenzi Aisha`Nilianza kuimba
nikimfuatisha Marijani kama kawaida yangu..``Sikiliza tamkoo..sikiliza kwa
makini,,tamko la moyoni,,ama kweli pendo lako limeingia moyoni mwanguu,,`Hakika
mashairi ya marijani huwa nayanipa hamasa sana..nilihamasika na kufunga macho
na kuona sura ya mume wangu mpendwa.Nilianza kukunja nguo nilizofua jana .
Jioni ilifika na mume wangu alirejea na baada ya kuoga tulikaa mezan.Cha ajabu
na kilichonistaajabisha ni kitendo cha mume wangu kulewa siku hiyo,nilimuuliza
kwanini umelewa na maisha yenyewe ndiyo haya? Akanijibu kwa sauti ya kilevi...``aah
nakunywa kuondoa mawazo kazi yenyewe ngumu kupatikana`.Niliangalia chini na
nikaingia chumbani kwangu nikamwacha anakula na watoto..Nilitoa radio yangu na
kuweka kanda ya muziki wa zamani alikuwa ni Marijani Rajabu nyimbo iliitwa
`pombe siyo chai`.Tulipoingia ndani wakati wa kulala nilimsihi mume wangu aache
pombe ,nilimsihi aone huruma jinsi ninavyoangaika kuamka alfajiri kupika
chapati na mandazi ili tuishi.Nikamwambia nimeona tangazo katika gazeti kuna
chuo cha lugha ya kifaransa ambacho ukifanya vizuri unapewa na kazi katika
kampuni ya utalii kwanini asisomee! Akacheka sana na kusema hawezi kurudi
shuleni kwakuwa ameshakuwa mtu mzima
``.Nikamwambia mume wangu asikate tamaa na elimu haina
mwisho,nilimbembeleza sana nikamwambia nitamlipia mimi na tena itakuwa
hafadhali kwakuwa yeye ni dereva na akisoma na lugha hiyo atapata kazi katika
kampuni ya utalii kiurahisi..alinyamaza na baada ya muda nikiendelea kuongea
akaanza kukoroma amelala. Niliwaza sana na sikutaka kumuacha mume wangu kwakuwa
nilimpenda sana mume wangu.Siku hiyo sikupata usingizi.Palikucha nikadamka kama
kawaida nikawasha jiko na kuanza kupika chapatti.Mume wangu aliamka saa mbili
na alipotoka kuoga alikuta nimemtengea chai. Alipokuwa anakunywa chai
nikaanza kumweleza tena juu ya kusomea lugha hiyo akaonekana kukubaliana
nami lakini kwa shingo upande.
Nilishukuru.Saa sita mchana nilipomaliza kuuza chapati
nilikimbia mjini haraka,nikanunua unga wa ngano kilo 20 na vifaa vingine
kwaajili ya kupika chapati na maandazi kwa mwezi mzima.Nikiwa nimefungasha vitu
vyangu nipo njiani natembea kwa miguu..ghafla nilisikia honi ya gari ikipiga
kwa sauti kuu.Nilishtuka na kukimbia pembeni mpaka nikaangusha mzigo wangu
niliyouweka kichwani.
Wapita njia wakaanza kunisaidia na
kunambia..pole..pole nikaitika asanteni jamani. Yule dereva nae alishuka
haraka na kunipa pole.Nikamwangalia usoni kumbe ni Yule baba aliyetaka
nimwache mume wangu ili niwe naye ingawa ana mke na watoto.Alinisaidia kubeba mzigo
wangu na kuingiza ndani ya gari lake.Nikamwambia asiweke ndani ya gari lake
kwakuwa sitopanda gari lake nitakwenda kwa miguu.
Alizidi kunisihi nipande gari lake lakini
nilikataa..akaingia ndani ya gari na mimi nikabaki nje.wakati huo akiwa
ameingia ndani ya gari lake na mzigo wangu.Nilianza kutoa machozi nikitaka
anipe mzigo wangu lakini aliendelea kukataa.Tukiwa tunabishana.. `cha
ajabu`katikati ya mji mume wangu akatokea akiwa na mwenzake ambaye
sikumfahamu.Nilipomwangali nayeye akanaiangalia,kisha akakunja uso..akazidi
kunifuata nikiwa nje ya gari lile..Nikamwambia Yule hamza anipe mzigo wangu
kwakuwa nipo na mume wangu na huyo hapo anakuja..aliposikia hivyo alitoa mzigo
wangu kwa dirishani na kunipa kisha akawasha gari na kuondoka.Mume wangu
alipofika akaanza kuniuliza kwa ukali,,Yule ni nani? Nikiwa naanza kujieleza
huku natetemeka akanipiga `kofi` nikaanguka chini,,akaanza kunishambulia kwa
mateke huku Yule rafiki yake waliyekuwa naye akimzuia asiendelee kunipiga
..Nililia sana na vitu vyangu vilimwagika,unga ukawa haufai tena,mafuta
yakamwagika.watu wakaanza kujaa katika eneo la tukio..alinichania sketi na
blauzi..kuna akina dada walikuwa na khanga wakaniazima ili nijistiri.mzozo
ukaanza huku Yule rafiki yake akimsihii asinipige na badala yake turudi nyumbani
kusuluhisha.Watu walijaa na wengine niliwasikia wakisema..``kamfumania mke wake
```.Niliumia sana moyoni kwakweli.Ila kuna baadhi ya watu walioona mwanzo mpaka
mwisho wa mimi na Yule mwenye gari walikuwa wakijitahidi kumwelewesha mume
wangu kuwa nilikuwa nakataa lifti ya Yule mtu..Nililia sana.
Tulirudi nyumbani wote watatu tukiwa na Yule rafiki
yake .Nilikaa kitandani huku nalia na kushika kifua changu ambacho nilihisi
kimeumia sana.Nikaanza kumwambia mume wangu kuwa Yule mtu alitaka kunipa lifti
lakini nilikataa.Mume wangu alifika sana kisha akaniuliza..kama alitaka kukupa
lifti mbona aliponiona alitoa mizigo yako ndani ya gari na kukimbia na gari?
Nikazidi kumwelewesha kuwa huyo mtu alinipigia honi nikaanguka na ndipo
alipotaka kunipa lifti.Mume wangu hakutaka kunielewa,,akazidi kumwambia Yule
rafiki yake kuwa mimi namsaliti kwakuwa sasa hana kazi na ndiyo tabia ya
wanawake..nilibisha na kujitahidi kumwomba radhi mume wangu.Yule rafiki yake
akasema suala lenyewe limejaa utata hivyo anisamehe tu kwakuwa hajanifumania
ila alinikuta njiani tena mjini nikiwa na mtu ..Nililia sana nikapiga magoti
kumwomba mume wangu anisamehe..alinisamehe lakini akanambia atanifuatilia.nami
nikasema nashkuru akinichunguza kwakuwa najiamini kuwa nampenda na sina sababu
ya kumsaliti.
Tulimaliza mzozo huku mume wangu akiwa amefura kwa
hasira.Walitoka na rafiki yake na kuniacha ndani.Mwanangu fatu aliingia ndani
na kunikuta nalia .Fatu alianza kulia huku akinikumbatia mimi,Tuliendelea kulia
wote,Nilijikaza kiutu uzima na kunyamaza na kumsihi mwanangu fatu anyamaze.Fatu
akaniuliza mama unalia nini huku nayeye akiendelea kulia.nilimwambia naumwa na
kumwambia anyamaze na aende sebleni.alitii amri yangu.Niliwaza...
```nyimbo ambayo sitoisahahu kwa siku hiyo ilikuwa ikipigwa
redioni..kiitikio kilisema hivii```matatizoo..yataka
kunizidiaa..ooohh..ramaaa...sitovumiliaaaaah..niliimba ile nyimbo mpaka mwisho
kisha nikainuka na kwenda kuoga.
JIONI YA SIKU HIYO
Nikiwa na maumivu,nilijitahidi kupika chakula na
kuweka mezani,kabla sijala nikameza dawa za maumivu.Ilikuwa ni saa tatu kasoro
usiku,mume wangu hakurejea,tulikula na watoto huku yeye chakula chake
nikikiweka kabatini.Fatu alianza kusinzia nikamlaza,na abdi alishalala muda
mrefu.Ilitimu saa tano usiku mume wangu akiwa bado hajarudi.Nimpigia simu
alipopokea niliskia kelele nyingi sana kama vile yupo baa! Nikamuuliza vipi uko
wapi mume wangu? Akanijibu kwa sauti ya ukali kuwa nisimsumbue na nimwache
..akakata simu.Nilikosa usingizi mpaka saa kumi usiku bado hajaja.nikapitiwa na
usingizi.
Nilipoamka siku hiyo sikuweza kupika chapati,sikuwa na
unga na pia nilikuwa naumwa kichwa na viungo karibu vyote.Niliamka saa nne
kutokana na kuumwa.Nilipoamka nilipika chai nikamtafuta mwanangu Fatu kwakuwa
aliamka mapema kwenda katika majumba ya watu ,nadhani alienda kuomba chai huyu
mtoto.Nikamwita akaja tukanywa chai.Wakati huo Abdi hayupo kwakuwa alikuwa ni
mtundu na nilijua amekwenda kuzurura hasa stendi .Tukiwa tunakunywa chai
nilichukua radio yangu na kuweka kanda ya nyinmbo ya zamani.Nyimbo iliitwa
`mume wangu`..nikaanza kuimba ili nipate faraja...```mume wangu jerry nimechoka
na visa vyako,,,sitovumilia tena kutokana na vituko
vyakoo,,nashindwaaa..juzijuzi ulinipiga kukuombaa,,utulie nyumbani.)
Tulimaliza chai nikachukua simu kisha kumpigia mume
wangu..iliita sana kama dakika tatu hivi haipokelewi..punde ikapokelewa lakini
alipokea mwanamke.Nikamwambia naomba kuongea na mwenye simu..akanisunya kisha
akaniuliza kwa dharau..kwani we nani? Nikamjibu kwakumwambia mimi mama fatu
naitaji kuongea na mmiliki wa hiyo siku ambaye ni Baba Fatu.Akanambia amelala
nipige baadaye.Kisha akakata simu.
BAADA HAPO!
Niliwaza sana na nikaumia sana moyoni,nilikuwa nashika
tama muda wote nikiwa chumbani kwangu.Nilikwenda chumbani kwa watoto wangu
nikakaa huko kwa muda mrefu.Nilimpigia mume wangu simu kwa mara nyingine saa
sita mchana,haikupokelewa hivyohivyo.mchana huo nikapika ugali nikamtafuta fatu
tukala. Abdi alishanishinda kutokana na utundu usiyomithilika Nilifanya hivyo
kwakuwa Abdi huwa hapatikani mchana ni mtundu ajabu Baada ya kula
nilienda dukani kwa mangi jirani yetu nikamkopa unga wa ngano kila kumi na
mafuta ili nianze kupika chapatti asubuhi kisha nimlipe fedha zake taratibu
kwakuwa mtaji ulitetereka.
Kwa siku mbili Baba Fatu hakutokea nyumbani,ndugu
zangu kama kuna kitu kinajua kuumiza hapa ulimwenguni basi ni mapenzi,niliumia
sana kwani kila nikipiga simu haipokelewi na kama ikipokelewa basi anapokea
mwanamke.Nikiskia sauti ya mwanamke naumi sana najuta kupiga simu na kukaa bila
kumpigia mume wangu siwezi.Nabaki kuumia huku nikijiliwaza na nyimbo za akina
Marijani Raju,Hemed Maneti na wengineo wa zamani.
Siku ya nne Mume wangu alikuja na tulipokaa mezani
nikaanza kumuuliza vipi mbona hajaonekana siku nne kuna usalama? Akanambia
nisimuulize kwakuwa mimi siyo mwaminifu na ameamua kuoa mke wa pili,tukiwa
tunazozana aliingia chumbani na kuchukua begi kubwa na kuweka nguo zake kisha
kuondoka kwa hasira.
Aliniacha nalia machozi.Usiku uliingia,Abdi alikuja na
Fatu tukawa tunakunywa chai na chapati zilizobaki katika harakati za
kuuza.Fautu akaniuliza ``Mama mbona Baba hauypo sikuhizi kwani amesafiri?
Nikamjibu ``ndiyo ameenda tena Arusha.Abdi alikuwa akibugia tu chapati bila kuongea
`yaonekana alikuwa na njaa na hajulikani alitokea wapi.
Pembeni niliweka rekodi ya Bi .Mwanahela ,mwambijai
mkongwe wa taarabu mwenye sauti isiyomithilika..nyimbo iliitwa `RABI SINIPE
MAPENZI..NA WAPENDWAO HAKUNA,,MAPENZI YA SIKUHIZI WATU KUHADAIANA) nilikuwa
naumia sana naposikia nyimbo kama hizo ila ilinilazimu kuzisikiliza kwakuwa
nilizipenda na zilinipa ujasiri na nguvu kutokana na mapenzi makubwa
niliyokuwanayo juu ya nyimbo hizo.
JAMANI MAPENZI YANAMUUMIZA
MAMA FATU……….ANAHITAJI KUNASULIWA..KESHAZAMA..
imeandikwa na mwandishi ma shuhuri wa vitabu mbalimbali hapa nchini Hemed Kivuyo pia mwandishi huyu ameshaandika kitabu kama rais anamtaka mke wangu pamoja na vingine vingi ukivitaka unaweza kuwasiliana
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia