Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga ameziagiza kamati za shule za
sekondari pamoja na kamati za maendeleo za kata kuweka mikakati
itakayowezesha shule zilizoko katika maeneo yao kuchukuwa wanafunzi wote
waliofaulu kuingia kidato cha kwanza.
Makunga ametoa agizo hilo
wakati akiendesha harambee ya kuchangia ukamilishaji wa darasa la shule
ya sekondari ya Lerai iliyoko katika wilaya hiyo kwa ajili ya maandalizi
ya kuchukuwa wanafuni waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza
Makunga
ameeleza kuwa kutokana na ufaulu mzuri wa wanafunzi katika wilaya,idadi
ya wanafunzi wote waliofaulu wamechaguliwa kujiunga na kidato cha
kwanza na hivyo wilaya inahitaji madarasa kumi na mawili.
Alisema
kuwa amelazimika kuhitisha haraka zaidi harambe ya shule ya sekondari
ya Lerai kutokana na halmashauri ya wilaya ya Hai kuwapanga wanafunzi
wote 67 kutoka kijiji hicho jamii ya wafugaji wa Kimasai katika shule
ya sekondari ya Boma ambayo ipo umbali wa kilometa saba.
Alisema
kuwa shule hiyo tayari ina chumba cha darasa darasa kinachotumiwa kama
ofisi ya walimu huku ikiwa na jengo linalohitaji kiasi cha shilingi
milioni nane na laki saba ili kukamilika na baadaye kutumiwa kama ofisi
ya walimu.
Shule ya sekondari ya Lerai iliyoanzishwa mwaka 2011
ina wanafunzi 98 wa kidato cha kwanza na cha pili na hivyo kuchukuliwa
kwa wanafunzi hao 67 kutafanya shule kuwa na wanafunzi 165.
Aliwaeleza
wananchi wa kijiji hicho kwamba ni vyema kuhakikisha watoto wanasoma
katika mazingira rafiki badala ya kutembea umbali mkubwa huku walipigwa
na jua na huku njiani wakikutana na watu wa tabia tofauti.
"Nawashukuru
kwa kujitokeza kwa wingi na kutoa michango ya ari na moyo ili
kuhakikisha watoto wetu wanasoma hapa hapa katika shule iliyopo jirani
badala ya kwenda Boma,"alisema Makunga.
Amezitaka kamati za
maendeleo za kata kukutana haraka iwezekanavyo na kamati za shule ili
kuweka mkakati wa kuchukiwa wanafuni wote waliofaulu kujiunga na kidato
cha kwanza
Aidha Makunga amemtaka mkurugeni mtendaji wa
halmashauri ya wilaya ya Hai,Melkizedeck Humbe kuhakikisha anasimamia
kwa ukaribu michango yote ya fedha iliyotolewa na wananchi kwa ajili ya
kukamilisha madarasa
Katika harambee hiyo jumla ya shilingi
milioni tano zilichangwa na jamii hiyo ya wafugaji wa kijiji cha Lerai
ambao walifikia maamuzi ya ujenzi kuanza mara moja.
Aidha Makunga
alitumia nafasi hiyo kuwapongeza wananchi wote wa Hai na wadau katika
elimu kwa kuwezesha wilaya hiyo kufanya vizuri katika mtihani wa
kumaliza elimu ya msingi.
Alisema kuwa wilaya ya Hai kati ya
halmashauri saba za mkoa wa Kilimanjaro, imeweza kushika nafasi ya pili
kwa kuwa na wastani wa ufaulu wa asilimia 86 ikiwa nyuma ya halmashauri
ya manispaa ya Moshi.
Alisema kuwa kwa mkoa mzima jumla ya
wanafunzi waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi ni 40,162
ambapo kati ya hao wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha
kwanza mwakani ni 32,905.
Alisema Kwa upande wa wilaya ya Hai
katika mtihani huo wa darasa la saba waliofanya watoto 4,826 ambapo
kati ya hao waliofaulu na kuchaguliguliwa kidato cha kwanza ni 4,128
sawa na asilimia 85.5.
Alisema kuwa wanafunzi 19 wamefanikiwa kuchaguliwa kujiunga na shule za bweni za ufaulu mzuri zaidi,ufundi na bweni kawaida
Shule
hizo kwa upande wa wasichana ni Kilakala,Msalato,Moshi
Technical,Iringa,Mgugu na Korogwe na kwa upande wa wavulana ni
Ilboru,Tabora,Moshi Technical,Ifunda Technical,Tanga
Technical,Iyunga,Mpwapwa,Malangali, Moshi na Songea.
Wilaya ya Hai ina jumla ya shule za sekondari ambazo ni za serikali 29.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia