Ticker

6/recent/ticker-posts

VIONGOZI WA SEREKALI MKOA WA ARUSHA WAGOMA KUSAIDIA MICHEZO MKOANI HAPA





SERIKALI imelaumiwa kwa kutosapoti michezo, hali inayozifanya klabu za mikoani kushindwa kupanda daraja hadi kufikia ligi kuu.
Akizungumza na LIBENEKE LA KASKAZINI jijini hapa , Katibu wa Chama cha Soka Mkoa wa Arusha (ARFA), Adam Brown, alisema kuwa, klabu za mkoani hapa zinashindwa kushika nafasi nzuri kwenye mashindano hasa ya kitaifa na kimataifa, kutokana na viongozi wa serikali kuanzia ngazi ya mkoa hadi kata kushindwa kuzisapoti.
Mbali na serikali, Brown alisema kuwa, mkoani hapa kuna wawekezaji wengi wenye viwanda, mashamba makubwa ya biashara pamoja na wafanyabiashara wakubwa, lakini wamekuwa wagumu kusapoti suala la michezo pale maombi yanapopelekwa, hali inayosababisha ukata na kushusha kiwango cha michezo.
“Wewe mwenyewe unashuhudia klabu za hapa mkoani ni tofauti na za mikoa mingine inayopata sapoti kwa wadau wa michezo, kwa mfano JKT Oljoro wakishindwa kuwafunga Yanga, watarudi nyumbani na madhara yake Kanda nzima ya Kaskazini itakosa timu ya ligi kuu,” alisema na kuongeza:
“Mimi niwaombe tu wadau wa michezo na viongozi wa serikali, wawe wanachangia na kudhamini klabu hizi, siyo kufurahia tu mafanikio au kuponda, bali wawe na michango itakayowezesha klabu hizi kushiriki ligi mbalimbali na mechi za kirafiki.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, John Mongela, alipokuwa akijibu malalamiko hayo, alisema kuwa hakuna mafungu yaliyopo kwa ajili ya michezo, hivyo kama watahitaji fedha ni vema kuandika maombi (proposal), ambako kwa msimu ujao wa bajeti, fedha zikiwepo watapewa.
“Sisi kama serikali hakuna fedha inayotengwa kwa ajili ya michezo, halafu tambua pia kuwa hakuna fedha inayokaa haina kazi, si wanakurupuka na kusema wanataka fedha na wakapatiwa, bali waandike proposal ya kuombea fedha, na msimu wa bajeti ukifika, kama itapatikana watapewa kama hakuna basi,” alisema Mongela.

Post a Comment

0 Comments