Ticker

6/recent/ticker-posts

NASSARI ASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUMTEKA MTENDAJI KATA


MBUNGE wa jimbo la Arumeru Mashariki Joshua Nassari anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kutuhumiwa na tukio la kumteka mtendaji wa kata ya makiba .

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Lebaratus Sabas alisema kuwa mtuhumiwa huyu alikamatwa majira ya saa moja usiku  December 16 katika eneo la Doli lililopo  katika kijiji cha Usa -river  kwenye gari  aina ya land Gruzer  lenye namba za usajili T 753 AQR.

Alisema kuwa    mbunge huyo anatuhumiwa kumteka mtendaji kata aliyefahamika kwa jina la Nemani Ndundu  wa kata ya makiba tarafa ya Mbuguni wilayani Arumeru mkoani Arusha  December 15  majira ya saa mbili asubui katika eneo la maji ya chai  .

Alibainisha kuwa mtendaji huyo alikumbwa na tukio hilo wakati alipokuwakatika pikipiki yake akielekea kwenye kata yake ndipo mbunge huyo alimkamata na kumpiga na kumjeruhi katika sehemu mbalimbali za mwili wake huku akimtaka amuonyeshe majina ya wanachama waliopiga kura katika kituo cha  huduma na maendeleo kilichopo katika kata yake   .

Aidha kamanda sabas alisema kuwa  mpaka sasa Joshua Nassari anashikiliwa na polisi na anatarajiwa kufikisha mahakamani  ya wilaya ya Arumeru leo December 17 kujibu tuhuma zinazomkabili.

Post a Comment

0 Comments