Ticker

6/recent/ticker-posts

TIMU YA JKT-OLJORO WAANZA MAANDALIZI MAKALI KWA AJILI YA LIGI DARAJA LA KWANZA

PICHA  na maktaba kikosi cha jkt oljoro
Timu ya maafande wa Jkt Oljoro yenye makazi yake jijini Arusha imepania haswa kupanda ligi kuu msimu wa ligi unaofuata baada ya wachezaji wake kuingia kambini mapema wiki hii kwa mazoezi mepesi wakimsubiria kwa hamu kubwa kocha wao Mbwana Makata huku wakijitamba hakuna machawi tena wa kuwabakiza ligi daraja la kwanza.

Wachezaji hao wanaoonekana katika milima na uwanja wa chuo cha uhasibu ulioko nje kidogo ya mji wameonekana kujifua kwa kasi kwa mbio mbali mbali sambamba na mazoezi ya hapa pale kujiandaa ya michuano ya ligi daraja la kwanza mwezi Agost huku wakijisemea “kwa mwaka huu hakuna mchawi kutoka duniani atakaeweza kuwazuia kupanda ligi kuu”

Katibu mkuu wa timu hiyo, Hussein Nalinga alisema kuwa hadi sasa wachezaji 15 wamerejea kambini ambapo hadi ijumaa hii wachezaji wote wataingia kambini na kufikisha idadi ya 28 ambao watajiunga na kocha mkuu baadae M’bwana Makata baada ya msimu wa ligi kuu kwisha ambapo kwa Prison imebakiza mechi tatu.

“Timu kwa sasa inarejea kambini ambapo wamefikia wachezaji 15 na wengine 13 wanaingia kesho hadi ijumaa na wanafundishwa na kocha msaidizi Sande Mussa hadi pale kocha wetu anaefundisha Timu ya Prison kurejea katika clabu yetu”

“Mimi niseme tu kwa mwaka huu Mungu yupo nasi na hakuna wa kutuzuia kupanda ligi kuu si timu zilizoko wala uwezo wa wachezaji wetu, ndio maana tunaanza mazoezi mapemaa ili kujifua ipasavyo ukiachilia mbali usajili wa kufa tutakaofanya msimu huu hivyo wana Arusha watoe sapoti yao kubwa kwa timu hasa ushauri kwani tunakata kiu yao ya kukosa ligi kuu msimu ukianza”

Post a Comment

0 Comments