Ticker

6/recent/ticker-posts

MFANYABIASHARA MAARUFU AWAWA NA MFANYAKAZI WAKE KISA SHILINGI LAKI MOJA



 
Mfanyabiashara maarufu jijini hapa  Anset Anselim Mashallo (34) mkazi wa Unga Limited   ameuwawa na mfanyakazi wake  kwa kuchomwa kisu mgongoni  wakati akidai kodi  ya pango ya kiasi cha shilingi laki moja   .
Akiongea na waandishi wa habari kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo alisema kuwa tukio hilo lilitokea May 19  majira ya saa 21:15 usiku katika maeneo ya Unga limited wilayani Arusha mjini.
Kamanda alimtaja mtuhumiwa wa mauaji hayo ni Prosper Adeline (47)mkazi wa Unga Limited ambaye alikuwa akifanyakazi ya kuchoma nyama katika bar ya marehemu ijulikanayo kwa jina  The Place bar iliopo jirani na kituo cha polisi ungalimited.

Alisema kuwa mtuhumiwa wa tukio hili alikuwa na ugomvi na marehemu   kwani marehemu alikuwa akimdai mtuhumiwa hela ya pango la jiko  lilikuwa ndani ya bar hiyo ambapo alikuwa akimdai kodi ya miezi miwili.

Mkumbo alisema kuwa hadi sasa matuhumiwa anashililiwa na jeshi la polisi kwa mahojiano zaidi na pindi upelelezi  utakapo kamilika atafikishwa mahakamani ,na mwili wa marehemu umeifadhiwa katika hospitali ya mkoa wa Mounti Meru .

Post a Comment

0 Comments