Ticker

6/recent/ticker-posts

RITA YAWATAKA WANANCHI KUANDIKA WOSIO MAPEMA KABLA YA KUFARIKI DUNIA




Afisa Usajili kutoka Rita Makao makuu Jijini Dar es salaam, Augustin Thomas Mbuya ,ambaye ndiye mtaribu wa zowezi la Kampeni ya kitoa huduma Rita,Akizungumza na wananchi Jijini Arusha ambapo kampeni hiyo imezinguliwa rasmi.


Mkuu wa  Wilaya ya Arusha Fadhili Nkulu,ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Kampeni ya Rita , ambapo imeanza rasmi katika Wilaya ya Arusha Mjini na itaendelea kwa siku nne.
Muwakilishi wa Rita Mkoa wa Arusha  Janeth Mandawa.


Afisa Usajili kutoka Rita makao makuu Jijini Dar es salaam Joseph Mwakatobe akizungumza na wananchi ,akitoa maelekezo namna ya kuandika wosia na umuhimu wa kuhifadhi wosia.
Afisa Usajili kutoka Rita Makao Makuu  Grace Shao.



Wananchi kutoka katika Wilaya ya Arusha Mjini wakfuatilia mafunzo 

Na Woinde Shizza,Arusha

 wananchi wametakiwa  kuepuka dhana potofu kuwa kuandika wosia ni Uchuro,jambo ambalo siyo kweli bali kuandika wosia ni kuepusha usumbufu na migogoro kwa ndugu watakaokuwa wamebaki aidha watoto au mjane pindi mlegwa anapokuwa amekufa .

Hayo yamesemwa na Afisa Usajili kutoka Rita  Joseph Mwakatobe katika ufunguzi wa zowezi la kampeni ya kutoa huduma za Rita kwa wananchi ,kuwapa elimu juu ya umuhimu wa kuandika wosia, namna ya kuhifadhi wosia.

Joseph amesema kuwa mara nyingi wosia ni muhimu sana kuandikwa kwasababu inawarahisishia wale wanaobaki kuepusha kunyimwa haki zao ,kudhulumiwa ,Rita inawashauri wananchi kuandika wosia,kwani watu wengi hawana elimu ya kutosha juu ya wosia.

Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Arusha Fadhili Nkulu amewahasa Rita wawaelimishe wananchi sheria ya mirathi pamoja mwongozo,pia wawasaidie wananchi kufahamu na kuelewa maeneo sahihi ya kuhifadhi wosia

Nkulu amesisitiza  kuwa mtu akiandika wosia ni vizuri zaidi maana ndiye anayejua mali zake, na pia anamfahamu mtu sahihi wa kumpatia urithi huo,na hii itaepusha migogoro na migongano ambayo ingeliweza kujitokeza.

Naye Mratibu wa zowezi la kampeni hiyo Augustin Mboya amesema kuwa lengo kuu la kampeni hiyo ni kutoa elimu kwa wananchi waifahamu umuhimu wa.kuandika wosia nakuhifadhi, watambue kuwa ile dhana ya kuwa kuandika wosia ni Uchuro na kujitabiria kifo ni potofu na haina mashiko yeyote ,Pia watambue kuwa mtu anayeandika wosia lazima awe na akili timamu ,bila kusahau kuwa wosia huandikwa kwa hiari na siyo kulazimishwa

Post a Comment

0 Comments