Ticker

6/recent/ticker-posts

WAIOMBA SERIKALI KUITUPIA MACHO KERO YAO YA MAJI

picha na maktaba
Na woinde Shizza, Arusha
Wakazi wa Kitongoji cha Shimbumbu Kata ya Ngwarusambo wilayani Meru wameimbo serikali kuitupia macho Kero yao ya Maji safi inayowasumbua kwa mda sasa licha ya fedha za Ahadi ya katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kutoa fedha hizo kiasi cha million 50 za uwekaji wa mabomba katika eneo hilo.

Akizungumza na wanahabari kijijini hapo Mwenyekiti wa kitongoji hicho Michael Mungure alisema kuwa wananchi wa kijiji cha Kimundo wamekuwa wakitaabika na adha ya maji kwa muda mrefu sasa ambapo mabomba ya mradi yamefika nusu badala ya kumalizia mradi huo kwa mda sasa.

Alisema kuwa mabomba ya maji ya kueneza maji maeneo mbali mbali katika kata yao yamefika nusu hali inayopelekea wananchi kuapata adha kubwa ya kuacha shughuli za maendeleo na kutafuta maji.

“Mh.Kinana alitoa ahadi ya kukamilisha kwa fedha kiasi cha million 50 hadi leo fedha za ahadi hazijatumika ipasavyo kukamilisha mradi kusudiawa na wananchi kupata maji”alisema Mungure.

Aliwataka viongozi wa wilaya hiyo akiwemo mkurugenzi mpya wa halmashauri ya Meru na diwani wa kata Jeremia Kanuya kutembelea eneo hilo na kuibua kero mbali mbali katika wilaya hiyo ikiwemo uchimbaji wa mawe katika maeneo ya kitongoji hicho mradi ambao umekuwa ukisaidia wananchi kupata fedha za kujikimu kimaisha na kupunguza tatizo la ajira.

Aidha alitoa wito kwa Serikali badala ya kuzui mradi wa uchimbaji mawe ukaibua fursa nyingine za wananchi kujipatia kipato cha kuendesha maisha yao ya kila siku.

Akalitaka jeshi la polisi kufika vijijini na kutoa elimi kwa vikundi vya ulinzi shirikishi wanaolinda maeneo yao kwani wamekuwa wakijichukulia sheria mikononi na vile vile kushirikiana na wenyeviti Vijiji,watendaji wa vijiji na wenyeviti wa vitongoji katika suala zima la ulinzi shirikishi.

Post a Comment

0 Comments