Ticker

6/recent/ticker-posts

KATIMBA : VIJANA IGENI MAISHA YA MWALIMU JULIUS NYERERE


Na Mwandishi Wetu, Kigoma
Mbunge wa vijana mkoa kigoma zainab Katimba amesema ili vijana nchini waweze  kubadili maisha yao, kujijenga kiuchumi, kielimu na kujitegemea, hawana budi kuiga na kufuata nyayo za maisha aliyoishi Baba wa Taifa marehemu  Mwalimu julisu kanbarage Nyerere.
Amesema Mwalimu Nyerere  katika maisha yake aliamini kazi ndiyo heshima ya kila mtu, kazi humpa mtu heshima na kukuza thamani ya utu wa mtu  mahali na wakati wowote alipo  .
Katimba alitoa matamshi hayo juzi wakati aliposhiriki katika kongamano la kukumbuka siku ya kifo cha muasisi wa Taifa letu Mwalimu Nyerere  huko Kigoma Mjini Mkoani hapa.
Alisema kazi za uzalishajimali viwandani na mashambani lazima zifanywe na vijana wenyewe kwasababu ndiyo nguvu kazi ya Taifa pia kutokaana na uimara wa ujana walionao, upeo na ufahamu huwasaidia na kuwafanya wabuni na kutenda kwa haraka na usahihi.
"Kufuata au kupita juu ya nyayo na kuiga maisha ya Mwalimu Nyerere kijana   anaweza kufaidika aidha katika kujijenga kiuchumi, kisiasa na kiuongozi kwasabahu muasisi wetu aliishi kwa kimaadili, kikazi na kinidhamu "alieleza Katimba.
Aidha  aliwataka vijana mkoani kigoma kutambua na kufahamu umuhimu wa dhana ya kujituma na kufanya kazi kwa bidii huku akieleza kwamba changamoto zinazowakabili vijana mijini na vijijini atazifikisha bungeni na serikali itazipatia ufumbuzi.
Pia aliwahimiza vijana wenzake wajenge utamaduni wa kupenda kusoma vitabu vya historia, majarida na maandiko mbalimbali yanayoelezea maisha ya Mwalimu Nyerere  , alivyoanzisha chama TANU, kupigania   uhuru wa Tanganyika , kuanzishwa kwa Taifa la Tanzania na kushiriki kwake harakati za ukombozi kusini mwa Afrika.
"Mwalimu Nyerere katika maisha yake alipenda kujitolea kwa hali na mali  hakusubiri kutoa msaada wa aina yoyote aidha kwa kuombwa au kwa masharti kwani alijiona ana haki na wajibu wa kumsaidia kila binadamu  na kumfanya awe huru "alieleza Mbunge huyo wa vijana
Hata hivyo aliipongeza serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk John Magufuli  kwa msisitizo wa kauli mbiu ya hapa kazi na kusema kila mmoja ikiwa ataikubali kufanya kazi kwa bidii, Tanzania ya maendeleo ya viwanda itawezekana, uchumi utaimarika na maisha bora yatatimia.
Katimba aliwahimiza vijana kujikita katika kazi za kilimo, ufugaji, uvuvi, kazi za mikono, ufundi pia za ujasiriamali na biashara mbalimbali kwani alisema kijana kukaa bila kujituma hakuleti maana wala utatuzi wa matatizo au  changamoto zilizopo.
"Kila wakati ninapopata nafasi ya kuchangia au kupeleka hoja binafsi bungeni nimekuwa niguswa na ugumu maisha ya vijana, huwa sina mzaha, naibana serikali na kuitaka itoe majibu ya kuridhisha "alieleza
Alisema kwasababu ameingia bungeni kwa minajili ya kuwawakilisha vijana kamwe alusisitiza  hataacha kutotetea au kutopigania haki na maslahi yanayohusu maisha ya vijana kiuchumi, kisiasa na kimaendeleo.

Post a Comment

0 Comments