Ticker

6/recent/ticker-posts

UPINZANI UMERITHIA SER ZA KISULTAN NA UKOLONI


vingeundwa kizalendo visingembeza Dk Magufuli 

Na Mwandishi Wetu , Kigoma 

Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) umesema upinzani uliopo ni mabaki ya vyama vya wanasiasa uchwara waliojitahidi kwa miaka mingi kuvipinga Vyama vya TANU na ASP hatimaye Serikali zake mara baada ya Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961 na Mapinduzi ya Zanzibar ya  mwaka 1964. 

Pia Umoja huo umesema upinzani wa ulipo nchini hauna chochote cha kupoteza kwasababu vyama hivyo vimerithi sera na mipango ile ile ya wakoloni na sultan ya kuwawagawa wananchi, kuwagombaniaha na ikibidi wakiomba hata damu imwagike.

Msimamo huo umeelezwa  jana na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM  Shaka Hamdu Shaka wakati alipozumgumza na viongozi na wananchma wa ccm kata ya Nguruka wilaya ya Uvinza Mkoani hapa  .

Shaka alisema baadhi viongozi wa vyama vya upinzani laiti vingelikuwa vimenazisha kwa ajili ya kupigania maslahi ya umma, kupigania  maendeleo, vikikerwa na umasikini wa watu,  ufisadi, rushwa na ubadhirifu, visingebeza juhudi za serikali ya Rsis Dk John Magufuli. 

Alisema kwasababu viongozi wa vyama hivyo hawajali shime ya uzalendo huku baadhi yao kuwa nai sehemu ya saratani ya ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma, ndiyo maana hawana jipya kwani  hata wanaposhinda serikali za vijiji ,uwakilishi wa kata na majimbo  hushindwa kubuni na kuleta kasi ya maendeleo.

"Wapinzani  wa sasa ni wale wale warithi wa msimamo ya kuvipinga TANU na ASP ni mabaki na masalia ya sera za kisultan na ukoloni,  hawana jipya ndiyo maana wanabeza juhudi za serikali ya Dk Magufuli, wangelikuwa wazalendo na waungwana, wasingeona aibu kumuunga mkono Rais badala ya kumpinga "Alisema Shaka 

Aidha alisema si hivyo tu lakini pia wapinzani hao hata mchakato na mpango mkakati wa kuyaunganisha yaliokuwa Mataifa huru ya Tanganyika na Zanzibar na kuunda muungano, waliupinga na hata sasa wanataka kutugawa kwa manufaa ya wale wanaowatuma na kuwatumikia  

Shaka alisema vyama hivyo vya zamani ambavyo zimeacha urithi wake kwa vyama vya upinzani vilivyopo ,havipendi kuona umoja, mshikamano na upendo ukimarika na kuwanufaisha wananchi kuendelea kuishi pamoja kwa kufuata sheria na kutii katiba ya nchi. 

"Unapovipima vyama vya upinzani,uwepo wa viongozi wake wanaoshika madaraka kwa miaka mingi  ,sera zake , mipango yao na matamshi wanayotamka, yatamjengea picha kila mmoja wetu kuviona vyama hivyo vimejaa wanasiasa wababajishaji wenye malengo ya  kusimamia urithi wa sera za kisultan na kikoloni "Alieleza shaka .

Kaimu huyo katibu Mkuu wa UVCCM aliwataka wananchi kutambua kuwa Muungano wa Tanganyika na zanzibar  hautakufa kama inavyokusudiwa na na wapinzani ili kuligawa Taifa na kulisibabishia mitafaruku. 

"Kwa bahati mbaya Rais Dk Magufuli amekwishasema na kuweka msimamo,atakayejaribu kuusambaratisha muungano atasambaratika yeye kabla ya kuuyumbusha muungano na watu wake "Alisema Shaka. 

Alisema chama cha mapinduzi kitaendelea kuwatumikia wananachi wake wa Bara na Zanzobar na kamwe hakuna mtu atakayeturudisha katika zama ya ukoloni au usultan. 

Post a Comment

0 Comments