Diwani
aliyehusika kuwarekodi viongozi wa Halmashauri ya Meru wanaodaiwa kuwa
walikuwa wakiwashawishi kwa ahadi ya fedha na mambo mengine Madiwani wa
CHADEMA ili wajiuzulu, amejitokea na kusema kuwa yeye alifanya hivyo
kutokana na kuchukia rushwa.
Diwani
wa Kata ya Mbuguni, Ahimidiwe Rico aliyasema hayo wakati akizungumza na
waandishi wa habari baada ya kutoka katika ofisi za Taaisisi ya Kuzuia
na Kupamba na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Arusha ambao alihojiwa kwa
takribani saa tatu kuhusu tuhuma hizo za rushwa.
Rico
aliwaambia waandishi wa habari kuwa alifanya hivyo kutokana na kuchukia
rushwa na ni kwa manufaa ya maslahi mapana ya taifa na sio kwamba ni
masuala ya kisiasa.
Akizungumzia
kuhojiwa na TAKUKURU, Rico alisema kuwa alifika katika ofisi hizo baada
ya kupokea wito uliomtaka kufanya hivyo, na alipofika alikutana na
maafisa wa TAKUKURU kutoka Makao Makuu Dar es Salaam, ambapo walimhoji
na yeye alitoa ushirikiano wote wakati wa mahojiano hayo.
Alisema
kuwa alipoulizwa kuhusu vifaa vilivyotumika kurekodi, alisema kuwa ni
mali ya Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari ambavyo alivitoa
nchini Uingereza alipokuwa akisoma, na kwamba ushahidi huo
walishirikiana kuukusanya.
Rico
hakuweka wazi na masuala gani aliyoulizwa au aliyowaambia maafisa hao
akisema kuwa, jambo hilo lipo chini ya uchunguzi hivyo ni vyema
wakaachiwa TAKUKURU wenyewe wafanye kazi yao.
Mbali
na Rico, maafisa hao waliwahoji kwa zaidi ya saa sita, madiwani
waliojiuzulu Chadema wanaotuhumiwa na Mbunge Nassari kuwa walipewa
rushwa na si kweli kwamba walijiuzulu kwa hiar yao kama ambavyo walidai
kwa nyakati tofauti.
Wengine
waliohojiwa ni Catherine Mtui, aliyekuwa Diwani wa Viti Maalumu, Japhet
Jackson, aliyekuwa Diwani wa Ambuleni na Bryson Isangya, aliyekuwa
Diwani wa Maroroni.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia