MkuuwaWilayayaArusha
GabrielDaqqaroakikabidhihundiyashilingimilioni 500
yamkopowakinamamailiyotolewanaHalmashauriyaJiji la Arusha
KinamamanavijanawaliokusanyikakatikaukumbiwaArusha
School kupewamafunzokablayakupatiwamikopoyahalmashauri.
Na Woinde Shizza,Arusha
Jumla ya
Shilingi milioni 605 zimetolewa kama mkopo wa kuwanufaisha wajasiriamali
walioko kwenye vikundi vya kinamama na vijana pamoja na walemavu waliopo katika Halmashauri ya Jiji la Arusha.
Akizungumzia
mikopo hiyo inayotolewa na Halmashauri Afisa Ustawi wa Jamii Jiji la Arusha Hanifa
Ramadhani amesema kuwa mikopo hiyo inatolewa ili kuwawezesha kinamama na vijana
kuondokana na hali ngumu za kiuchumi zinazowakabili ili kuinua uchumi .
Mkuu wa
Wilaya ya Arusha Gabriel Daqqaro amewataka Vijana ambao ni wasomi kujiunga
katika vikundi hivyo na kupata mikopo ili kujiendeleza kiuchumi badala ya
kusubiri ajira serikalini ile hali nafasi ni chache na wahitimu wa vyuo ni
wengi.
Kwa upande
wao Wanufaika wa Mikopo hiyo kwaniaba ya Walemavu Mwajuma Juma na Patrick Petro wameishukuru serikali kwa kutoa mikopo hiyo
yenye masharti nafuu ambayo itawasaidia kujikwamua kiuchumi.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia