MKUU WA WILAYA YA ARUSHA AELEZA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI KWA KIPINDI CHA MWAKA 2005-2012
Wednesday, January 30, 2013
Woinde Shizza
0 Comments
Wednesday, January 30, 2013 Woinde Shizza 0 Comments
Mkuu wa wilaya ya arusha akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na utekelezaji wa ilayani ya uchaguzi kwa kipindi cha mwaka 2005-2012
picha ya juu na chini ni baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Arusha wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela wakati akielezea mafanikio ya utekelezaji wa ilani ya chama katika manispaa ya Arusha tangu mwaka 2005-2015
Na Woinde Shizza,Arusha
Imeelezwa
kuwa ilani ya ccm kwa miaka saba katika wilaya ya arusha imefanikiwa
kwa kiasi kikubwa katika njanja zote zikiwemo sector ya elimu
,afya,mazingira,na miundombinu ikiwemo mji wa arusha kuwa jiji rasmi.
Hayo
yameelezwa na mkuu wa ilaya ya Arusha John Mogella mbele ya waandishi wa
habari wakati akitoa taarifa hiyo katika hotel ya palace hapa jijini
arusha na kusema kuwa sector zote zimefanikiwa kwa kiasi
kikubwa kwani toka mwaka 2005 hadi mwaka 2012 karibu utekelezaji wa
ilani ya chama cha mapinduzi imetekelezwa.
Bw
Mogella amesema katika sector ya elimu amesema wamejenga madarasa
172,matundu ya vyoo 225,ambapo shule za msingi zimeongezeka 70 ambapo
kwa shule za sekondari zimeongezeka 23ambapo awali zilikuwa saba ,ambapo
walimu na vifaa vya usimamizi wameongezeka 534 kwa miaka hiyo saba
pamoja na idadi ya vyuo vya shahada ya juu vikuu kupandishwa hadhi na kufikia 8 .
Amesema
kwa upande wa afya mkuu mogela amesema kuwa wameweza kuboresha huduma
ya mama na mtoto ambapo vituo 5 na zahanati 68 zimeboreshwa kwa uhakika
wa upatikanaji wa dawa na huduma bora,huku akifafanua kuwa wameipandisha
hadhi kituo cha afya cha kanisa st.elizabert na kuwa hospitali ya
wilaya huku akisema kuwa katika hospitali hilo kuna kituo kikuu
kitakachotoa huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi ambapo
kitatoa huduma bure.
Kwa
upande wa miundo mbinu amesema kuwa barabara nyingi zimejengwa katika
kiwango cha lami katika barabara hasa za katikati ya mji ambapo hadi
sasa barabara 23 zenye urefu wa km 8 zimekamilika ambapo mkradi huu
unaofaziliwa na benki ya dunia kwa kiasi cha dola million 7 za
kimarekani,ambapo ni awamu ya kwanza na awamu ya pili itajenga barabara
ya njiro,kanali ndomba,pamoja na kujenga dampo la kisasa la
kisasa,yakiwemo ujenzi wa madaraja 9 katika wilaya ya arusha.
Mogela
akiongezea kuhusu upande wa maringira hasa upande wa maji amesema
asilimia 83 ya wakazi wanaoishi katika jiji la arusha wanapata maji safi
na salama tofauti na awali ilikuwa ni asilimia 42 tu ya wakazi ndio
waliopata huduma hiyo ya maji salama ,ambapo amesema kuwa wanamkakati wa
mradi wa ujenzi wa miundo mbinu utakao gharimu shilingi million moja.
Katika
swala la mazingira amesema wamepiga hatua kwani wameweza kulinda vyanzo
vya maji kwa kushirikiana na AUWSA ikiwemo misitu,kuzuia uoshaji wa
magari pembezoni mwa mito,na kuzuia ukataji wa miti katika misitu
iliyopo ndani ya jiji ikiwemo kuboresha usafi ndani ya jiji letu.
Aidha
alisema pamoja na mafanikio hayo pia kuna changamoto zinzoikabili jiji
hili ikiwemo ya kusafisha hati chafu ya jiji hili ,ambapo baadhi ya
viongozi wabadhirifu wa raslimali wamewajibishwa kutokana na makosa yao
ikiwemo kufikishwa mahakamani paoja na kufukuzwa kazi.
Pia aliongezea kuwa changamoto nyingine ni demokrasia ambapo wilaya yetu ina viongozi wa vya vya
siasa tofautitofauti ambapo alitolea mfano mbunge wa chadema katika
jimbo la mjini arusha kutofautiana katika utekelezaji na uwajibikaji
katika kuwatumikia wananchi wa wilaya hii .
Mwisho
mkuu wa wilaya ya arusha Mogella alitoa wito kwa wakazi wa jiji la
arusha kuendelea kushirikiana na viongozi katika kuhakikisha hali ya
jiji inakuwa tulivu ambapo kwa kiasi kikubwa katika swala la ulinzi na
usalama ikiwemo dhana ya ulinzi shirikishi na tii sheria bila shuruti.
Wednesday, January 30, 2013
Woinde Shizza
0 Comments
Wednesday, January 30, 2013 Woinde Shizza 0 Comments
SAKATA la mdogo wa Mbunge wa Kinondoni, Seleman Ally Mohamed kudaiwa kumtupia vyombo nje mkewe, Asma Ally limepata ufumbuzi baada ya mmiliki halali wa nyumba waliyokuwa wakiishi wanandoa hao kutinga katika ofisi za gazeti hili na kuanika ukweli.
Mmiliki huyo aitwaye Uddy Juma Boma alitinga katika ofisi zetu Bamaga, Mwenge jijini Dar Alhamisi iliyopita na kuonesha vielelezo vya umiliki wa nyumba hiyo Block D plot Na.382 iliyoko Sinza jijini Dar.
Katika maelezo yake Uddy alisema kuwa aliinunua nyumba hiyo kutoka kwa mzee Patrick Lence Kimolo mwaka 1995 kwa shilingi milioni 7 kwa kulipa fedha katika mahakama ya Magomeni jijini Dar kwa awamu mbili.
“Mwaka 1996 nilihamia na kupokelewa na mjumbe Ally Kuza aliyekuwa mwenyeji wangu,“ alisema.
Uddy alisema mwaka 2000 alihamia Bahari Beach katika nyumba nyingine na hiyo ya Sinza akaipangisha kwa Seleman ambaye ni mdogo wa mbunge wa Kinondoni
(Mheshiwa Idd Azzan) kwa shilingi 150,000 makubaliano yalifanyika kwa wakili Godfrey Boniphace Taisamo.“
Mwaka 2006 Seleman alisema kuwa hana uwezo wa kupanga kutokana na gharama za maisha kupanda, cha kushangaza mkewe Nasma amekataa kutoka ndani ya nyumba akidai kuwa ni ya mumewe.
“Mwaka 2009 kesi ilifika mahakama ya nyumba Magomeni mwaka 2011 ikahamia Kinondoni na wakati wote huo Selemani alikuwa akikiri mahakamani kwamba mkewe hataki kuhama, mahakama ikatoa samansi ya kumuita Asma,“ alisema.
Januari 14, 2013 mahakama ikitoa kibali cha kumtolea vyombo nje.
ASMA ALLY ANASEMAJE
Asma amemwambia mwandishi wetu kuwa haamini kama nyumba hiyo siyo ya Selemani kwa sababu walinunua mwaka 2002.
“Mume wangu ametumia mbinu ili kunitimua katika nyumba baada ya kufanikisha kuwachukua watoto na kwenda kuwaficha kwa ndugu zake.
“Wamenifanyia hila ili niweze kuishi kwa shida, nitaendelea kufuatailia suala hili hadi kieleweke,“ alisema Nasma.
MSIKIE SELEMANI
“Mimi nilikuwa mpangaji tu na alichokifanya mzee Uddy Juma ni kufuata taratibu ili kuchukua nyumba yake, ni kweli baada ya huyu mwanamke hataki kutoka, niliamua kuwachukua watoto wangu ili yeye ajue namna ya kufanya,“ alisema Seleman.
BENKI YA KCB TANZANIA IMETOA MSAADA KWA SHULE ZA MSINGI NA HOSPITALI JIJINI DAR
Wednesday, January 30, 2013
Woinde Shizza
0 Comments
Wednesday, January 30, 2013 Woinde Shizza 0 Comments
Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund
Mndolwa katikati akimkabidhi moja ya msaada wa madawati kati ya 89 Mwalimu Mkuu
wa shule ya Msingi ya Makumbusho Bi.Benedicta Lyimo,yaliyotolewa na benki hiyo
yenye thamani ya Milioni 17.4,anaeshuhudia kulia ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano
wa benki hiyo Bi.Christine Manyenye.
) Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund
Mndolwa kushoto na Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo Bi.Christine
Manyenye wakioneshwa moja ya jengo la wodi ya kujifungulia wakinamama na Mganga
Mkuu wa Hospitali ya Sinza Dare s Salaam mara baada ya kukabidhi rasmi vifaa
mbalimbali vikiwepo vitanda vya kujifungulia vine vyote vikiwa na thamani ya
Milioni 7.4 kwa ajili ya kituo hicho.
Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund
Mndolwa akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki
hiyo Bi.Christine Manyenye,wakati alipokuwa akikagua moja ya vitanda
kati ya vinne vya kujifungulia wakina mama kabla ya kuvikabidhi rasmi
kwa uongozi wa Hospitali ya Sinza iliyopo jijini Dar es Salaam vyote
vyenye thamani ya shilingi milioni 7.4 ,kushoto Meneja Masoko wa benki
hiyo Emelda Gerald.
Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund
Mndolwa akisalimiana na mmoja wa
wanafunzi wa darasa la saba shule ya msingi Makumbusho alipofika shuleni hapo
kutoa msaada wa madawati 89 na vifaa vya kusomea,vyote vyenye thamani
ya shilingi milioni 17.4 kulia ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo
Bi.Christine Manyenye.
Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki ya KCB Tanzania
Bi.Christine Manyenye na Meneja Masoko wa benki hiyo Emelda….wakimsikiliza
Muuguzi wa Hospitali ya Sinza jijini Dar es Salaam Rachel Mshana mara
walipofika hospitalini hapo kukabidhi msaada wa vitanda vine na vifaa mbalimbali
kwa ajili ya kujifungulia akinamama wajawazito vyote vyenye thamani ya shilingi
milioni 7.4.
Mwenyekiti
wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund
Mndolwa kulia akimkabidhi moja ya msaada wa madawati na meza Mwalimu
Mkuu wa shule ya Msingi Kibamba yenye watoto wenye ulemavu wa akili
Bi.Asia
Mpate,yaliyotolewa na benki hiyo yenye thamani ya Milioni 17.4,katikati
ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo
Bi.Christine Manyenye.
Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund
Mndolwa akimkabidhi Mganga Mkuu wa
Hospitali ya Sinza ya jijini Dares Salaam,Benedict Luoga moja ya kitanda kati
ya vinne Salaam vyote vyenye thamani ya shilingi milioni 7.4 vilivyotolewa na
benki hiyo kwa ajili ya kujifungulia akinamama wajawazito.
Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund
Mndolwa kulia akimsikiliza jambo Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Kibamba yenye watoto wenye ulemavu wa akili Bi.Asia
Mpate,baada ya kumkabidhi rasmi msaada wa madawati 89 yenye thamani ya Milioni
17.4,wapili kulia k Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo Bi.Christine
Manyenye,na kushoto ni Mwalimu msaidizi wa shule hiyo Bi.Mwajabu Minja.
Na Mwandishi wetu
Shule
ya Msingi ya Kibamba katika wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam
inakabiliwa na uhaaba wa madawati 500, jambo linalowalazimu wanafunzi
wa shule hiyo kukaa chini wakati wakifundishwa darasani.
Mwalimu
Mkuu wa shule hiyo, Asia Mpate alibahanisha hayo jana na kusema kuwa
shule yake yenye wanafunzi 1,950,kuliwa na madawat 320 na madarasa 13
tu.
Mwalimu
Mkuu huyo alikuwa akizungumza kwenye hafla ya kukabidhiwa misaada na
Benki ya KCB iliyotoa madawati 25, meza tatu, viti vya walimu sita,
madafyari 235 na peni 200 , vyote vikiwa na thamani ya Sh, Milioni 5 kwa
shule hiyo.
Alisema
kuwa uhaba mkubwa wa madawati katika shule yake kumepelekea utoro
mkubwa kwa wanafunzi wake kwani wanafunzi wake hulalamikia hali mbaya
na ugumu wa kukaa chini sakafuni.
Mpate
amesema kuwa wanafunzi wengi wa shule yake wamechanganyikiwa na hali
hiyo na hivyo huamua kutohudhuria masomo, jambo linaofanya ufanisi
mdogo wa elimu kwa wanafunzi wake.
"
Utoro ni mkubwa katika shule yetu kwa sababu hali halisi ya madarasa ni
ya kutisha, hatuna madarasa ya kutosha wala vitendea kazi .
Tunashukuru Benki ya KCB kwa msaada wao ambao tunaamnini kuwa
utatusaidia kuboresha kiwango cha elimu katika shule yetu", alisema
mwalimu mkuu huyo..
Kwa
upende wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo, Dk
Edmund Mndolwa alisema kuwa msaada huo ni sehemu ya wajibu wake wa
benki kusaidia jamii na kwamba benki yake imejidhatiti kusaidia kuinua
kiwango cha elimu nchini Tanzania.
Aliwashauri wanapokea misaada ya benki hiyo kutumia ipasavyo na inavyotakiwa misaada inayotolewa na benki yake.
Kwenye
hafla hiyo pia benki ya KCB ilitoa msaada wa madawati 64 yenye thamani
ya Sh. Milioni tano kwa Shule ya Msingi ya Makumbusho pia ya jijini.
Wakati
huo huo hopsitali ya Sinza ya jijini Dar es Salaam imepokea msaada
wa vifaa vya hospitali vyenye thamani ys Sh. Milioni 7.4 kutoka kwa
Benki ya KCB katika hafla iliyofanyika kwenye hopsitali hiyo jana.
Dokta
Mwandamizi wa hospitali hiyo, Dk Benedict Luwoga alishukuru benki
hiyo kwa msaada huo na kusema kuwa vifaa hivyo vilikuja kwa wakati na
kuvitaja vifaa hivyo ni pamoja na vitanda vinne vya kuzalisha kwa
mama wajawazito.
Alisema
kuwa hospitali yake ilizidiwa uwezo kwa sababu ilikuwa na vitanda
viwili tu vya kuzalisha mama wajawazito , kwa hiyo vitanda hivyo vinne
zaidi ilikuwa ni ukombozi mkubwa kwa hospitali yake.
"Tunashukurui
Benki ya KCB kwa msaada huo, umekuja kwa wakati ambapo hospitali
ilikuwa ikikabiliwa na changamoto nyingi. Amezitaka kampuni zingine
ziige mfano wa benki ya KCB", alisema Dk Luwoga.
Bluestar kuitambulisha singo yake mpya
Wednesday, January 30, 2013
Woinde Shizza
0 Comments
Wednesday, January 30, 2013 Woinde Shizza 0 Comments
MSANII wa mjini Arusha anayekuja kwa kasi katika mziki wa kizazi kipya
hapa nchini Hamisi Omari(20)maarufu kama Bluestar anatarajia kuachia
singo yake ya tatu inayokwenda kwa jina la Tunachafua.
Akizungumza na gazeti hili amesema kuwa singo hiyo ambaye
amemshirikisha Mr Blue na Swaga Boy na kurekodiwa katika studio ya
Danlumark kwa Macko P ya jijini Dar es Salaam itaanza kusikika rasmi
wiki hii katika vituo mbalimbali vya redio na kutazamwa katika
luninga.
“Nawataka wapenzi wa muziki wa kizazi kipya na mashabiki wangu kwa
ujumla wakae mkao wa kula kupokea wimbo huo kwani ni moto wa kuotea
mbali”alisema Bluestar.
Amezitaja nyimbo zake mbali ambazo tayari aliishazitoa mwaka jana kuwa
ni Digidagi aliyemshirikisha Chris G ambayo ameirekodia katika studio
ya Fnock kwa Sumtimber na Njoo aliyeirekodia katika studio ya
Dunlumark.
Msaanii huyo ambaye alianza muziki mwaka jana amesema kuwa matarajio
yake ni kuja kuwa mwanamuziki maarufu sana ndani na nje ya nchi na
kwamba katikati ya mwaka huu atatoa albamu yake ya kwanza na kutoa
wito kwa mashabiki kumuunga mkono.
UN YAENDESHA MAFUNZO KUHUSU SHUGHULI ZA UNDAP NA HAKI ZA BINADAMU KWA WAANDISHI WA HABARI VISIWANI ZANZIBAR
Tuesday, January 29, 2013
Woinde Shizza
0 Comments
Tuesday, January 29, 2013 Woinde Shizza 0 Comments
Afisa habari ngazi ya Taifa wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi.Usia
Ledama akieleza nia ya Umoja wa Mataifa Tanzania kuendesha mafunzo kwa
waandishi wa habari wa Visiwani Zanzibar juu ya Haki za binadamu na
jinsi Mpango wa msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP)
unavyoshirikiana na Serikali ya Zanzibar katika maeneo matatu muhimu
ambayo ni Uchumi, Kupunguza umaskini na Utawala na uwajibikaji. Semina
hiyo imefanyika katika Hoteli ya Zanzibar Ocean View visiwani Zanzibar.
Mratibu
wa FAO Ofisi ya Zanzibar Ali Haji Ramadhan akitoa hotuba ya makaribisho
katika mkutano na waandishi wa habari wa Visiwani Zanzibar ambapo
amesema wanatarajia kupata mawazo mengi zaidi ya kujenga kutoka kwa
waandishi ambapo yatasaidia Umoja wa Mataifa pamoja na Serikali
kuihudumia nchi kwa upeo wa juu zaidi.
Mwakilishi
wa mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa Zanzibar Anna Senga akizungumza na
waandishi wa habari wa visiwani Zanzibar kuhusu changamoto
wanazokabiliana nazo wao kama UN katika kutekeleza hoja za mipango wa
maendeleo (UNDAP) kutokana na kuchelewa kupewa majibu na uchelewashaji
wa utekelezaji wa mipango ya maendeleo.
Afisa
Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu akizungumza na
waandishi wa habari wakati wa mafunzo hayo ambapo ameelezea Mpango
Mkakati wa UNDAP visiwani Zanzibar ikiwemo kutoka ufafanuzi wa mafanikio
pamoja na changamoto zinazoukabili mpango huo.Amesema
mpango huu ni wa pamoja kwa ajili ya Tanzania unaendena na mafanikio ya
malengo ya maendeleo ya kimataifa ambapo unachukua nafasi ya program za
pamoja na miradi mingi inayodhaminiwa na UN chini ya Model ya misaada
ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa kwa mpango wa kazi moja ulioshikamana
kwa ajili ya mifuko ya fedha, program na wakala zote za Umoja wa Mataifa
nchini Tanzania.
Baadhi
ya waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo hayo ya siku moja
wakimsikiliza Afisa Mawasilano wa Umoja wa Mataifa nchini Hoyce Temu.
Katibu
wa Chama cha wanasheria wanawake Zanzibar Hamisa Mmanga Makame akitoa
somo katika mafunzo hayo ambapo amezungumzia masuala ya Haki za
Binadamu, umuhimu wa kuzingatia jinsia na wajibu wa vyombo vya habari
katika kuleta usawa.
Afisa
Mipango mwandamizi wa shirika la kazi duniani (ILO) Anthony
Rutabanzibwa ambapo amevipongeza vyombo vya habari vya Afrika Mashariki
kwa kutoa kipaumbele katika habari zinazohusu haki za binadamu na
kuwataka waandishi kuzingatia zaidi habari za kiuchunguzi ili kuwa na
uhakika zaidi na yale wanayoaandika ikwemo kujua chanzo cha habari
unayoitoa.
Mwenyekiti
wa UNCG Yusuph Al Amin akielezea mada ya umuhimu wa mawasiliano kwa
maendeleo na kuwataka wamiliki wa vyombo vya habari na serikali kwa
ujumla kubadilisha sera zinazosimamia vyombo hiyo ili ziweze kutoa fursa
kwa waandishi kuwa huru katika uandishi na kuripoti habari bila
kubanwa.
Kutoka
kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Zanzibar Hassan Khatibu,
Mratibu wa FAO Ofisi ya Zanzibar Ali Haji Ramadhan, Mwakilishi wa
mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa Zanzibar Anna Senga, Mwezeshaji wa
mafunzo hayo mwandishi mkongwe Salim Said Salim na Mwenyekiti wa UNCG
Yusuph Al Amin.
Rais
wa Umoja wa vilabu vya waandishi wa habari Kenneth Simbaya akitoa maoni
yake kuhusiana na nini kifanyike katika kuboresha tasnia ya habari
ambapo ameshauri mafunzo kuendelea kutolewa si tu kwa waandishi pia kwa
wamiliki wa vyombo vya habari.
Pichani Juu na chini ni baadhi ya waandishi ws habari wa visiwani Zanzibar wakichangia mawazo yao wakati wa mafunzo hayo.
Afisa mipango wa Baraza la Habari Tanzania Ofisi ya Zanzibar Shifaa Said Hassan akichangia hoja wakati wa mafunzo hayo.
Sehemu ya waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo ya siku yaliyoendeshwa na Umoja wa Mataifa visiwani Zanzibar.
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu akijadili jambo na wafanyakazi wenzake wakati wa mafunzo hayo
CHADEMA SASA WAPANGA SAFU...., KUINGIA IKULU 2015
Tuesday, January 29, 2013
Woinde Shizza
0 Comments
Tuesday, January 29, 2013 Woinde Shizza 0 Comments
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akifungua mkutano huo
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akimkabidhi
kadi ya uanchama wa chama hicho aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Bara wa
Chama cha NCCR-Mageuzi, Clemence Tara baada ya kujiunga na chama hicho.
Katibu Mkuu Dk. Willbroad Slaa akizungumza katika mkutano huo.
bungo John
Mnyika akitete jambo na Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Willbroad Slaa
(kulia) wakati wa Kikao cha dharura cha Baraza Kuu la Chadema
kilichofanyika jijini Dar es Salaam, leo.
Katibu Mkuu Dk. Willbroad Slaa akisalimiana na baadhi ya wajumbe katika mkutano huo.
Mbunge
Kigoma, Zitto Kabwe akiwasikiliza kwa makini wajumbe wa kikao cha
dharura cha Baraza Kuu la Chadema kutoka mkoa wa Mtwara.
Muasisi wa Chadema, Edwin Mtei akiingia katika ukumbi wa mkutano huku akifuatana na Mwenyekiti wa Chadema, Freema Mbowe.

Picha juu na Chini sehemu ya wajumbe wakiitikia Peoples Power
Sehemu ya Wabunge wa Chadema
Wajumbe wa mkutano.
Baadahi ya wabunge wa Chadema wakiwa katika kikao hicho.
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika(katikati) akiwa amepozi na baadhi ya wajumbe.Picha zote na Mdau Dande Francis
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) kimepitisha mpango mkakati wake wa kuelekea kushika dola
mwaka 2015 kwa kumega madaraka ya makao makuu katika kanda kumi.
Maazimio hayo yalipitishwa na Kamati Kuu (CC) juzi kwa agenda moja kubwa ambayo ni kupitisha mpango mkakati wa mwaka 2013 ili kushinda chaguzi zote kuanzia serikali za vitongoji, vijiji na mitaa mwaka 2014 na Uchaguzi Mkuu 2015.
Akizungumza na wajumbe wa kikao cha dharura cha Baraza Kuu jana, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema kuwa mpango mkakati huo umelenga kufanya mabadiliko ya uongozi kuanzia ngazi ya taifa kwenda katika majimbo na kukipanga upya chama hicho kwa mustakabali wa taifa.
“Mtakumbuka kwamba wakati tunakianzisha chama chetu, tulizungumzia sera ya majimbo na kuainisha kazi zake…sasa tumeanza kupanga kazi zenyewe kwa kugawa majukumu katika kanda kumi.
“Tunataka tuishi vile tunavyosema kwa kuwa katika miaka mingi ya kuwa chini ya uongozi wa serikali ya CCM, wananchi wamekuwa wakiamriwa mambo yao na kundi dogo la watu wanaojikusanya sehemu moja ya nchi, hilo kwetu si mfano bora wa uongozi,” alisema.
Mbowe aliongeza kuwa katika miaka 20 ya kuhimili misukosuko ya kisiasa chama hicho kimejifunza mengi na sasa kiko tayari kushika dola ndio maana wameanza kugawa majukumu kwa wananchi kupitia uongozi wa kikanda.
Alisema kuwa wamejiandaa kwa mashambulizi ya aina zote na sasa jukumu kubwa la kila kanda litakuwa ni kuhakikisha kila mwananchi anaiunga mkono CHADEMA katika eneo atakalokuwa.
Mwenyekiti huyo alitaja kanda hizo na mikoa husika kuwa ni Kanda ya Ziwa Magaharibi (Mwanza, Geita, Kagera), Ziwa Mashariki (Mara, Simiyu, Shinyanga), Ziwa Magharibi (Kigoma, Tabora, Katavi) na Kati (Singida, Dodoma, Morogoro).
Zingine ni Kata za Nyanda za Juuu Kusini (Mbeya, Ruvuma, Iringa), Kusini (Lindi na Mtwara), Mashariki (Pwani, Dar es Salaam na Tanga), Kaskazini (Kilimanjaro, Manyara, Arusha), Pemba na Kanda ya Unguja.
Mbowe alisema katika kuhakikisha vikosi hivyo vinafanya kazi zake vizuri, kila kanda itajengewa ofisi, kununuliwa magari, pikipiki na vifaa vyote vya ofisini na za mikutano.
“Lengo la mkakati huo pia ni kuhakikisha CHADEMA inasimama katika chaguzi zote bila kupingwa…tunataka CCM ndiyo ipingwe katika chaguzi na hili tutalifanikisha,” aliongeza.
Katika suala zima la Muungano, Mbowe alisema uwepo wa serikali tatu hauepukiki kwa kuwa tayari Tanzania Visiwani wameshakuwa na serikali yao hivyo ni jukumu la Watanzania Bara kupata serikali ya Tanganyika na kisha kuwepo na serikali ndogo ya Muungano.
Alisema serikali tatu inawezekana ikiwa viongozi wataacha unafiki wa kusema muungano utavunjika huku tayari wakitoa uhuru wa Zanzibar kuwa na Rais, bendera na wimbo wao ya taifa.
Tunawaunga mkono wenzetu Wazanzibar katika kupigania uhuru kamili na kwa sasa sisi ndio tunaoonekana wa ajabu kushindwa kuuliza serikali ya Tanganyika,” alisema.
Mbowe pia aligusia tume huru ya uchaguzi akisema serikali ihakikishe Watanzania wanapata tume hiyo kwa kuwa tayari hata viongozi wa chombo hicho wameshatoa maoni na kutaka wapewe uhuru wa kufanya kazi.
Alisema serikali kama inafikiri kuwa CHADEMA itaingia katika uchaguzi wa 2015 ikiwa chini ya tume iliyopo sasa watakuwa wanajidanganya na badala yake watalazimisha upatikanaji wa tume hiyo.
Wailiza CCM Kagera
Katika hatua nyingine chama hicho kimeiliza CCM katika uchaguzi mdogo wa vijiji na vitongoji uliofanyika wilayani Muleba mkoani Kagera Jumapili iliyopita.
Licha ya wilaya ya Mulebe yenye majimbo mawili ya uchaguzi kusini na kaskazini yakiwa chini ya CCM, CHADEMA imeweza kunyakuwa viti vingi vilivyokuwa vikishikiliwa na chama hicho tawala.
Katika uchaguzi huo CHADEMA ilinyakuwa vijiji vitatu kati ya vitano katika jimbo la Muleba Kusini linaloongozwa na Prof. Anna Tibaijuka ambavyo ni Kasenyi, Kabunga na Ihangilo.
CHADEMA pia imechukua vitongoji sita vya CCM kati ya 12 vilivyofanya uchaguzi. Vitongoji hivyo ni Nyamagojo, Mushumba, Nyakabingo, Kyamyorwa, Katanda na Kyogoma.
Katika Jimbo la Muleba Kaskazini, linaloshikiliwa na Charles Mwijage, CCM ilipoteza vijiji viwili vya Katoke na Kahumulo kati ya vitano vilivyofanya uchaguzi huku vitongoji vinne vya Rundu, Kalee, Lwanganilo na Kituvi vikiangukia kwa CHADEMA.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu kutoka Muleba, Katibu wa Baraza la Vijana wa Taifa (BAVICHA), Robert Rwegasira, alisema wamepata ushindi huo kutokana na wananchi kuanza kuwaamini.
Mafanikio hayo yametokana na hamasa ya vuguvugu la mabadiliko la CHADEMA (M4C) ambalo lilifanyika katika mkoa wa Kagera Novemba mwaka jana.
Katika jimbo la Muleba Kusini, CHADEMA ingeweza kupata viti vya vitongoji zaidi ya idadi iliyopata kwani walisimamisha wagombea tisa kati ya 12 huku nafasi tatu wakiwaachia CUF na NCCR-Mageuzi ambao hawakuambulia chochote.
Maazimio hayo yalipitishwa na Kamati Kuu (CC) juzi kwa agenda moja kubwa ambayo ni kupitisha mpango mkakati wa mwaka 2013 ili kushinda chaguzi zote kuanzia serikali za vitongoji, vijiji na mitaa mwaka 2014 na Uchaguzi Mkuu 2015.
Akizungumza na wajumbe wa kikao cha dharura cha Baraza Kuu jana, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema kuwa mpango mkakati huo umelenga kufanya mabadiliko ya uongozi kuanzia ngazi ya taifa kwenda katika majimbo na kukipanga upya chama hicho kwa mustakabali wa taifa.
“Mtakumbuka kwamba wakati tunakianzisha chama chetu, tulizungumzia sera ya majimbo na kuainisha kazi zake…sasa tumeanza kupanga kazi zenyewe kwa kugawa majukumu katika kanda kumi.
“Tunataka tuishi vile tunavyosema kwa kuwa katika miaka mingi ya kuwa chini ya uongozi wa serikali ya CCM, wananchi wamekuwa wakiamriwa mambo yao na kundi dogo la watu wanaojikusanya sehemu moja ya nchi, hilo kwetu si mfano bora wa uongozi,” alisema.
Mbowe aliongeza kuwa katika miaka 20 ya kuhimili misukosuko ya kisiasa chama hicho kimejifunza mengi na sasa kiko tayari kushika dola ndio maana wameanza kugawa majukumu kwa wananchi kupitia uongozi wa kikanda.
Alisema kuwa wamejiandaa kwa mashambulizi ya aina zote na sasa jukumu kubwa la kila kanda litakuwa ni kuhakikisha kila mwananchi anaiunga mkono CHADEMA katika eneo atakalokuwa.
Mwenyekiti huyo alitaja kanda hizo na mikoa husika kuwa ni Kanda ya Ziwa Magaharibi (Mwanza, Geita, Kagera), Ziwa Mashariki (Mara, Simiyu, Shinyanga), Ziwa Magharibi (Kigoma, Tabora, Katavi) na Kati (Singida, Dodoma, Morogoro).
Zingine ni Kata za Nyanda za Juuu Kusini (Mbeya, Ruvuma, Iringa), Kusini (Lindi na Mtwara), Mashariki (Pwani, Dar es Salaam na Tanga), Kaskazini (Kilimanjaro, Manyara, Arusha), Pemba na Kanda ya Unguja.
Mbowe alisema katika kuhakikisha vikosi hivyo vinafanya kazi zake vizuri, kila kanda itajengewa ofisi, kununuliwa magari, pikipiki na vifaa vyote vya ofisini na za mikutano.
“Lengo la mkakati huo pia ni kuhakikisha CHADEMA inasimama katika chaguzi zote bila kupingwa…tunataka CCM ndiyo ipingwe katika chaguzi na hili tutalifanikisha,” aliongeza.
Katika suala zima la Muungano, Mbowe alisema uwepo wa serikali tatu hauepukiki kwa kuwa tayari Tanzania Visiwani wameshakuwa na serikali yao hivyo ni jukumu la Watanzania Bara kupata serikali ya Tanganyika na kisha kuwepo na serikali ndogo ya Muungano.
Alisema serikali tatu inawezekana ikiwa viongozi wataacha unafiki wa kusema muungano utavunjika huku tayari wakitoa uhuru wa Zanzibar kuwa na Rais, bendera na wimbo wao ya taifa.
Tunawaunga mkono wenzetu Wazanzibar katika kupigania uhuru kamili na kwa sasa sisi ndio tunaoonekana wa ajabu kushindwa kuuliza serikali ya Tanganyika,” alisema.
Mbowe pia aligusia tume huru ya uchaguzi akisema serikali ihakikishe Watanzania wanapata tume hiyo kwa kuwa tayari hata viongozi wa chombo hicho wameshatoa maoni na kutaka wapewe uhuru wa kufanya kazi.
Alisema serikali kama inafikiri kuwa CHADEMA itaingia katika uchaguzi wa 2015 ikiwa chini ya tume iliyopo sasa watakuwa wanajidanganya na badala yake watalazimisha upatikanaji wa tume hiyo.
Wailiza CCM Kagera
Katika hatua nyingine chama hicho kimeiliza CCM katika uchaguzi mdogo wa vijiji na vitongoji uliofanyika wilayani Muleba mkoani Kagera Jumapili iliyopita.
Licha ya wilaya ya Mulebe yenye majimbo mawili ya uchaguzi kusini na kaskazini yakiwa chini ya CCM, CHADEMA imeweza kunyakuwa viti vingi vilivyokuwa vikishikiliwa na chama hicho tawala.
Katika uchaguzi huo CHADEMA ilinyakuwa vijiji vitatu kati ya vitano katika jimbo la Muleba Kusini linaloongozwa na Prof. Anna Tibaijuka ambavyo ni Kasenyi, Kabunga na Ihangilo.
CHADEMA pia imechukua vitongoji sita vya CCM kati ya 12 vilivyofanya uchaguzi. Vitongoji hivyo ni Nyamagojo, Mushumba, Nyakabingo, Kyamyorwa, Katanda na Kyogoma.
Katika Jimbo la Muleba Kaskazini, linaloshikiliwa na Charles Mwijage, CCM ilipoteza vijiji viwili vya Katoke na Kahumulo kati ya vitano vilivyofanya uchaguzi huku vitongoji vinne vya Rundu, Kalee, Lwanganilo na Kituvi vikiangukia kwa CHADEMA.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu kutoka Muleba, Katibu wa Baraza la Vijana wa Taifa (BAVICHA), Robert Rwegasira, alisema wamepata ushindi huo kutokana na wananchi kuanza kuwaamini.
Mafanikio hayo yametokana na hamasa ya vuguvugu la mabadiliko la CHADEMA (M4C) ambalo lilifanyika katika mkoa wa Kagera Novemba mwaka jana.
Katika jimbo la Muleba Kusini, CHADEMA ingeweza kupata viti vya vitongoji zaidi ya idadi iliyopata kwani walisimamisha wagombea tisa kati ya 12 huku nafasi tatu wakiwaachia CUF na NCCR-Mageuzi ambao hawakuambulia chochote.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Hi There, I am
Follow Me
{getWidget} $results={3} $label={comments} $type={list1}
Popular Posts
Labels
- .atukio
- Afya
- atukio
- BAADHI YA WANACHAMA WA KLABU YA WAZEE WA ARUSHA WAKIFUATILIA KWA UMAKINI UCHAGUZI WA KLABU YA WAZEE YA ARUSHA ULIOFANYIKA JUMAPILI ILIYOPITA KATIKA VIWANA VYA GENERAL TYRE MKOANI ARUSHA
- Biashara
- biashira
- bishara
- buradani
- burudan
- Burudani
- ELIMU
- FILAMU
- HABAARI
- HABABARI
- HABAERI
- HABAQRI
- habar
- Habari
- habari matukio
- habari siasa
- habari makala
- HABARI MATUKIO
- habari matuko
- habari utalii
- habariVICHW
- habrai
- habri
- hanari
- haqbari
- hatari
- Havari
- hawa ni vijana wa chadema walio uthuria msiba wa msanii albert magwehaa
- katibu mkuu wa cuf ambaye ni makamu wa rais wa kwanza wa zanzibar sharif hamad akimnadi mgombea wa udiwani kupitia chama chao john bayo
- KILIMO
- lakini hatimaye katika hatua za mwisho viongozi hawa walisomewa mashitaka na wakawekewa zamana na kesi yao itasikilizwa tena tarehe 21
- m atukio
- maatukio
- MAISHA
- MAjanga gari hii libeneke imeikuta maeneo ya mitaa ya kaloleni karibu na msikiti likiwa limegonga nguzo ya umeme mara baada ya kukosa nguvu wakati ikipanda mlima
- makala
- Makamu wa rais wa huduma ya JSMI Terry Savelle Foy akigawa msaada wa maindi kwa wanakijiji wanaoishi kwenye mazingira magumu ambao wamekubwa na njaa
- Makamu wa rais wa huduma ya JSMI Terry Savelle Foy akigawa msaada wa maindi kwa wanakijiji wanaoishi kwenye mazingira magumu ambao wamekubwa na njaa katika kijiji cha Lopilukuny katika kata ya Kisongo
- mapenzi
- marukio
- mat+ukio
- matakio
- matikio
- matilop
- matuikio
- MATUIO
- MATUK
- matuki
- matuki9o
- matukiio
- MATUKIO
- MATUKIO MICHEZO
- MATUKIO UTALII
- matukio biashara
- matukio burudani
- MATUKIO ELIMU
- MATUKIO HABARI
- mAtukio maonyesho nanenane arusha
- matukio michezo
- MATUKIO RIADHA
- MATUKIO SIASA
- MATUKIO UTALII
- matukio.
- MATUKIO.BURUDANI
- MATUKIO.HABARI
- MATUKIO\
- MATUKIO9
- matukiobiashara
- MATUKIOL
- MATUKIOM
- matukiop
- matukkio
- MATUKO
- matukom
- matyukio
- MAUKIO
- mautkio
- mbunge wa jimbo la Arusha mjini akiwa amelazwa katika hospitali ya mounti meru mara baada ya kuanguka gafla huku picha ingine ikionyesha mbunge akiuguzwa na mke wake
- Meneja wa masoko wa Kcb Christina Manyenye akimkabithi msaada wa madawati Sister Rashmi Mattappally
- Mgombea mwenza wa urais wa chama cha APPT Maendeleo Rashid Mchenga akiwahutubia wananchi wa mkoa wa Arusha katika moja ya kampeni zake alizozifanya jana
- Mgombea ubunge akipanda mti katika tawi la ccm kata ya kaloleni
- Mgombea ubunge wa tiketi ya chama cha mapinduzi Dr.Batilda Buriani anayefuata kushoto ni mgombea udiwani wa kata ya Sombetini Alifonsi Mawazo akicheza na wananchi nyimbo za chama
- Mgombea udiwani wa kata ya daraja mbili akihutubiwa wananchi wa daraja mbili na kuwaomba kura ikiwa zimebaki siku chache kabla ya uchaguzi
- MICHEZO
- MICHUZI
- mmatukio
- MQATUKIO
- mtukio
- muonekano wa sehemu ya standi ya magari madogo Arusha
- MUZIKI
- mwatukio
- Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Arusha Jubilet Kileo akimnadi mgombea ubunge wa CCM jimbo la Arusha mjini kwa wananchi wa Elerai alipokuwa kwenye moja ya kampeni zake
- mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Arusha Sabaya lengai akiongea na waandishi wa habari leo
- natukio
- olasiti
- Picha meneja wa benki ya Kcb tawi la Arusha Judith Makule akiwatambulisha wafanyakazi wenzake kwa wananchi wa kata ya Terati walipoenda kugawa madawati
- Picha mgombea ubunge wa ccm jimbo la simanjiro Ole Sendeka akiwa na mgombea ubunge wa jimbo la Arusha mjini Dr.Batilda Burian wakibadilishana mawazo siku ya sherehe za kufunga kampeni za Arusha mjini
- Picha mgombea ubunge wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema Godbless lema akiwa anaondoka katika ofisi ya halmashauri ya jiji mara baada ya kutangazwa kuwa mbunge wa jimbo la Arusha mjini
- Picha mgombea ubunge wa jimbo la Simanjiro akiomba kura zote za ndio ziende kwa wagombea wa CCM
- Picha msimamizi wa uchaguzi jiji la Arusha Estomhn Chan'gah katikati aliyevaa kofia nyeupe kichwani akitangaza matokeo ya uchaguzi jimbo la Arusha mjini na kata zake
- Picha ni wananchi wakipiga kelele mbele ya ofisi ya msimamizi mkuu wa uchaguzi wakidai majibu ya kura zao
- picha timu yenye rangi blue ni timu ya Polisi morogoro na rangi ya bahari ni Jkt Oljoro mechi iliyochezewa katika uwanja wa Sherk Amri Abeid
- Picha wananchi wa kata ya Ngarenaro wakiwa katika kituo cha Shule ya msingi Sombetini wakiwa wanaangalia majina yao kama yapo katika orodha ya wapiga kura
- Picha wananchi wa mkoa wa Arusha wakiwa nje ya jengo la halmashauri ya jiji la Arusha wakisubiri kumjua mbunge wa jimbo lao la Arusha mjini hivi leo
- Pihca mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema akiwasalimia wananchi mara tu baada ya kutangazwa mshindi leo
- POLISI
- RIADHA
- SIASA
- Sister Rashmi Mattappally ambaye ni muhasisi wa kikundi cha Zinduka akiwakaribisha wageni kutoka KCB Bank
- TEKNOLOJIA
- tukio
- ukarabati wa barabara ukiendelea katika barabara ya majengo jijini arusha
- UT
- utalii
- wafanyakazi wa KCB wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutoa msaada wa madawati katika shule ya awali ya Tegemeo iliyopo katika kata ya terati
- Wananchi wa jimbo la Arusha mjini wakiwa katika barabara wakishangilia ushindi wa chadema
- Watoto wa elimu ya awali wa shule ya tegemeo wakicheza kwa furaha mbele ya wafanyakazi wa KCB
Ad Banner
Wanaonitembelea
4928698
KUMBUKUMBU
Categories
- MATUKIO(4611)
- Habari(3251)
- Burudani(471)
- SIASA(431)
- MICHEZO(217)
- Biashara(170)
- utalii(114)
- HABARI MATUKIO(112)
- habari matukio(97)
- MATUKIO HABARI(60)
- makala(19)
- matukio burudani(15)
- Afya(14)
- MATUKIO SIASA(10)
- MATUKIO MICHEZO(6)
- MATUKIO UTALII(6)
- matukio biashara(6)
- ELIMU(5)
- mapenzi(4)
- POLISI(3)
- FILAMU(2)
- KILIMO(1)
- MAISHA(1)
- MATUKIO ELIMU(1)
- MATUKIO RIADHA(1)
- MATUKIO UTALII(1)
- MUZIKI(1)
- RIADHA(1)
- TEKNOLOJIA(1)
- habari siasa(1)
- habari makala(1)
- hatari(1)
- matukio michezo(1)
Blogu Marafiki
Recents
{getWidget} $results={3} $label={recent} $type={list1}
0 Post a Comment:
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia