KAA MKAO WA KULA KWA FILAMU MPYA YA FREEMASON

Wednesday, January 30, 2013 Woinde Shizza 0 Comments


0 Post a Comment:

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

MKUU WA WILAYA YA ARUSHA AELEZA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI KWA KIPINDI CHA MWAKA 2005-2012

Wednesday, January 30, 2013 Woinde Shizza 0 Comments

 Mkuu wa wilaya ya arusha akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na utekelezaji wa ilayani ya uchaguzi kwa kipindi cha mwaka 2005-2012

 picha ya juu na chini ni baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Arusha  wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Arusha John Mongela wakati akielezea mafanikio ya utekelezaji wa ilani ya chama katika manispaa ya Arusha tangu mwaka 2005-2015
 Na Woinde Shizza,Arusha
Imeelezwa kuwa ilani ya ccm kwa miaka saba katika wilaya ya arusha imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika njanja zote zikiwemo sector ya elimu ,afya,mazingira,na miundombinu ikiwemo mji wa arusha kuwa jiji rasmi.

Hayo yameelezwa na mkuu wa ilaya ya Arusha John Mogella mbele ya waandishi wa habari wakati akitoa taarifa hiyo katika hotel ya palace hapa jijini arusha  na kusema kuwa sector zote zimefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani toka mwaka 2005 hadi mwaka 2012 karibu utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi imetekelezwa.

Bw Mogella amesema katika sector ya elimu amesema wamejenga madarasa 172,matundu ya vyoo 225,ambapo shule za msingi zimeongezeka 70 ambapo kwa shule za sekondari zimeongezeka 23ambapo awali zilikuwa saba ,ambapo walimu na vifaa vya usimamizi wameongezeka 534 kwa miaka hiyo saba pamoja na idadi ya vyuo vya shahada ya juu vikuu kupandishwa hadhi  na kufikia 8 .

Amesema kwa upande wa afya mkuu mogela amesema kuwa wameweza kuboresha huduma ya mama na mtoto ambapo vituo 5 na zahanati 68 zimeboreshwa kwa uhakika wa upatikanaji wa dawa na huduma bora,huku akifafanua kuwa wameipandisha hadhi kituo cha afya cha kanisa st.elizabert na kuwa hospitali ya wilaya huku akisema kuwa katika hospitali hilo kuna kituo kikuu kitakachotoa huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi ambapo kitatoa huduma bure.

Kwa upande wa miundo mbinu amesema kuwa barabara nyingi zimejengwa katika kiwango cha lami katika barabara hasa za katikati ya mji ambapo hadi sasa barabara 23 zenye urefu wa km 8 zimekamilika ambapo mkradi huu unaofaziliwa na benki ya dunia kwa kiasi cha dola million 7 za kimarekani,ambapo ni awamu ya kwanza na awamu ya pili itajenga barabara ya njiro,kanali ndomba,pamoja na kujenga dampo la kisasa la kisasa,yakiwemo ujenzi wa madaraja 9 katika wilaya ya arusha.

Mogela akiongezea kuhusu upande wa maringira hasa upande wa maji amesema asilimia 83 ya wakazi wanaoishi katika jiji la arusha wanapata maji safi na salama tofauti na awali ilikuwa ni asilimia 42 tu ya wakazi ndio waliopata huduma hiyo ya maji salama ,ambapo amesema kuwa wanamkakati wa mradi wa ujenzi wa miundo mbinu utakao gharimu shilingi million moja.

Katika swala la mazingira amesema wamepiga hatua kwani wameweza kulinda vyanzo vya maji kwa kushirikiana na AUWSA ikiwemo misitu,kuzuia uoshaji wa magari pembezoni mwa mito,na kuzuia ukataji wa miti katika misitu iliyopo ndani ya jiji ikiwemo kuboresha usafi ndani ya jiji letu.

Aidha alisema pamoja na mafanikio hayo pia kuna changamoto zinzoikabili jiji hili ikiwemo ya kusafisha hati chafu ya jiji hili ,ambapo baadhi ya viongozi wabadhirifu wa raslimali wamewajibishwa kutokana na makosa yao ikiwemo kufikishwa mahakamani paoja na kufukuzwa kazi.
Pia aliongezea kuwa changamoto nyingine ni demokrasia ambapo wilaya yetu ina viongozi wa vya  vya siasa tofautitofauti ambapo alitolea mfano mbunge wa chadema katika jimbo la mjini arusha kutofautiana katika utekelezaji na uwajibikaji katika kuwatumikia wananchi wa wilaya hii .

Mwisho mkuu wa wilaya ya arusha Mogella alitoa wito kwa wakazi wa jiji la arusha kuendelea kushirikiana na viongozi katika kuhakikisha hali ya jiji inakuwa tulivu ambapo kwa kiasi kikubwa katika swala la ulinzi na usalama ikiwemo dhana ya ulinzi shirikishi na tii sheria bila shuruti.

0 Post a Comment:

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Wednesday, January 30, 2013 Woinde Shizza 0 Comments


Na Haruni Sanchawa

SAKATA la mdogo wa Mbunge wa Kinondoni, Seleman Ally Mohamed kudaiwa kumtupia vyombo nje mkewe, Asma Ally limepata ufumbuzi baada ya mmiliki halali wa nyumba waliyokuwa wakiishi wanandoa hao kutinga katika ofisi za gazeti hili na kuanika ukweli.
Seleman Ally Mohamed akiwa na mkewe, Asma Ally.
Mmiliki huyo aitwaye Uddy Juma Boma alitinga katika ofisi zetu Bamaga, Mwenge jijini Dar Alhamisi iliyopita na kuonesha vielelezo vya umiliki wa nyumba hiyo Block D plot Na.382 iliyoko Sinza jijini Dar.
 Katika maelezo yake Uddy alisema kuwa aliinunua nyumba hiyo kutoka kwa mzee Patrick Lence Kimolo mwaka 1995 kwa shilingi  milioni 7 kwa kulipa  fedha katika mahakama ya Magomeni jijini Dar kwa awamu mbili.
“Mwaka 1996 nilihamia na kupokelewa na  mjumbe Ally  Kuza aliyekuwa mwenyeji wangu,“ alisema.
Uddy alisema mwaka 2000 alihamia Bahari Beach katika nyumba nyingine na hiyo ya Sinza akaipangisha kwa Seleman ambaye ni mdogo wa mbunge wa Kinondoni
(Mheshiwa Idd Azzan) kwa shilingi 150,000 makubaliano yalifanyika kwa wakili Godfrey Boniphace Taisamo.“
Mwaka 2006 Seleman alisema kuwa hana uwezo wa kupanga kutokana na gharama za maisha kupanda, cha kushangaza mkewe Nasma amekataa kutoka ndani ya nyumba akidai kuwa ni ya mumewe.
“Mwaka 2009 kesi ilifika mahakama ya nyumba Magomeni mwaka 2011 ikahamia Kinondoni na wakati wote huo Selemani alikuwa akikiri mahakamani kwamba mkewe hataki kuhama,  mahakama ikatoa samansi ya kumuita Asma,“  alisema.
Januari 14, 2013 mahakama ikitoa kibali cha kumtolea  vyombo nje.

ASMA ALLY ANASEMAJE
Asma amemwambia mwandishi wetu kuwa haamini kama nyumba  hiyo siyo ya Selemani kwa sababu walinunua mwaka 2002.
“Mume wangu ametumia mbinu ili kunitimua katika nyumba baada ya kufanikisha kuwachukua watoto na kwenda kuwaficha kwa ndugu zake.
“Wamenifanyia hila ili niweze  kuishi kwa shida, nitaendelea kufuatailia suala hili hadi kieleweke,“ alisema Nasma.

MSIKIE SELEMANI
“Mimi nilikuwa mpangaji tu  na alichokifanya mzee Uddy Juma ni kufuata taratibu ili kuchukua nyumba yake, ni kweli baada ya huyu mwanamke hataki kutoka, niliamua kuwachukua watoto wangu ili yeye ajue namna ya kufanya,“ alisema Seleman.

0 Post a Comment:

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

BENKI YA KCB TANZANIA IMETOA MSAADA KWA SHULE ZA MSINGI NA HOSPITALI JIJINI DAR

Wednesday, January 30, 2013 Woinde Shizza 0 Comments


 Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund Mndolwa katikati akimkabidhi moja ya msaada wa madawati kati ya 89 Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Makumbusho Bi.Benedicta Lyimo,yaliyotolewa na benki hiyo yenye thamani ya Milioni 17.4,anaeshuhudia kulia ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo Bi.Christine Manyenye.
 ) Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund Mndolwa kushoto na Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo Bi.Christine Manyenye wakioneshwa moja ya jengo la wodi ya kujifungulia wakinamama na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Sinza Dare s Salaam mara baada ya kukabidhi rasmi vifaa mbalimbali vikiwepo vitanda vya kujifungulia vine vyote vikiwa na thamani ya Milioni 7.4 kwa ajili ya kituo hicho.   
  Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund Mndolwa  akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo Bi.Christine Manyenye,wakati alipokuwa akikagua moja ya vitanda kati ya vinne vya kujifungulia wakina mama kabla ya kuvikabidhi rasmi kwa uongozi wa Hospitali ya Sinza iliyopo jijini Dar es Salaam vyote vyenye thamani ya shilingi milioni 7.4 ,kushoto Meneja Masoko wa benki hiyo Emelda Gerald.
 Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund Mndolwa  akisalimiana na mmoja wa wanafunzi wa darasa la saba shule ya msingi Makumbusho alipofika shuleni hapo kutoa  msaada wa madawati  89 na vifaa vya kusomea,vyote vyenye thamani ya shilingi milioni 17.4 kulia ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo Bi.Christine Manyenye.
 Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki ya KCB Tanzania Bi.Christine Manyenye na Meneja Masoko wa benki hiyo Emelda….wakimsikiliza Muuguzi wa Hospitali ya Sinza jijini Dar es Salaam Rachel Mshana mara walipofika hospitalini hapo kukabidhi msaada wa vitanda vine na vifaa mbalimbali kwa ajili ya kujifungulia akinamama wajawazito vyote vyenye thamani ya shilingi milioni 7.4.
 Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund Mndolwa kulia akimkabidhi moja ya msaada wa madawati na meza  Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Kibamba   yenye watoto wenye ulemavu wa akili Bi.Asia Mpate,yaliyotolewa na benki hiyo yenye thamani ya Milioni 17.4,katikati  ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo Bi.Christine Manyenye.
 Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund Mndolwa  akimkabidhi Mganga Mkuu wa Hospitali ya Sinza ya jijini Dares Salaam,Benedict Luoga moja ya kitanda kati ya vinne Salaam vyote vyenye thamani ya shilingi milioni 7.4 vilivyotolewa na benki hiyo kwa ajili ya kujifungulia akinamama wajawazito. 

Mwenyekiti wa bodi ya benki ya KCB Tanzania,Bw.Edmund Mndolwa kulia akimsikiliza jambo Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Kibamba   yenye watoto wenye ulemavu wa akili Bi.Asia Mpate,baada ya kumkabidhi rasmi msaada wa madawati 89 yenye thamani ya Milioni 17.4,wapili kulia k Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo Bi.Christine Manyenye,na kushoto ni Mwalimu msaidizi wa shule hiyo Bi.Mwajabu Minja.

 Na Mwandishi wetu
Shule ya Msingi ya Kibamba  katika wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam inakabiliwa na  uhaaba wa madawati 500,  jambo linalowalazimu wanafunzi  wa shule  hiyo kukaa chini wakati wakifundishwa darasani.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Asia Mpate alibahanisha hayo jana na kusema  kuwa shule yake yenye wanafunzi 1,950,kuliwa na  madawat 320  na madarasa 13 tu.
Mwalimu Mkuu huyo alikuwa akizungumza kwenye hafla ya kukabidhiwa misaada na Benki ya  KCB iliyotoa madawati 25, meza  tatu,   viti vya walimu sita, madafyari 235 na peni 200 , vyote vikiwa na thamani ya Sh, Milioni 5 kwa shule hiyo.

Alisema kuwa uhaba  mkubwa wa madawati katika shule yake kumepelekea utoro mkubwa kwa wanafunzi wake  kwani wanafunzi wake hulalamikia  hali mbaya na ugumu wa  kukaa chini sakafuni.

Mpate  amesema kuwa wanafunzi wengi wa shule yake wamechanganyikiwa na hali hiyo  na hivyo huamua kutohudhuria masomo, jambo linaofanya  ufanisi  mdogo wa elimu kwa wanafunzi wake.

" Utoro ni mkubwa katika shule yetu kwa sababu hali halisi ya madarasa ni  ya kutisha, hatuna madarasa ya kutosha wala vitendea kazi . Tunashukuru Benki ya KCB kwa msaada wao ambao tunaamnini kuwa  utatusaidia kuboresha  kiwango cha elimu  katika shule  yetu", alisema mwalimu mkuu huyo..

Kwa upende wake Mwenyekiti wa Bodi ya  Wakurugenzi wa benki hiyo,  Dk Edmund  Mndolwa alisema kuwa  msaada huo  ni sehemu ya wajibu wake  wa benki kusaidia jamii na kwamba benki yake imejidhatiti kusaidia kuinua  kiwango cha elimu  nchini  Tanzania.

Aliwashauri wanapokea misaada ya benki hiyo kutumia ipasavyo na inavyotakiwa   misaada  inayotolewa na benki yake.

Kwenye hafla hiyo pia  benki ya KCB ilitoa msaada wa madawati 64 yenye thamani ya Sh. Milioni  tano kwa Shule ya Msingi ya Makumbusho pia ya jijini.
Wakati huo huo  hopsitali ya  Sinza  ya jijini Dar es Salaam imepokea msaada wa  vifaa vya hospitali vyenye thamani ys Sh. Milioni 7.4 kutoka kwa Benki ya KCB katika hafla  iliyofanyika kwenye hopsitali  hiyo jana.

Dokta Mwandamizi wa  hospitali  hiyo, Dk Benedict  Luwoga  alishukuru benki hiyo kwa msaada huo  na kusema kuwa  vifaa hivyo vilikuja kwa wakati na kuvitaja  vifaa hivyo ni  pamoja na vitanda vinne  vya kuzalisha kwa mama  wajawazito.

Alisema kuwa  hospitali yake ilizidiwa uwezo  kwa sababu ilikuwa na   vitanda  viwili tu vya kuzalisha mama wajawazito , kwa hiyo vitanda hivyo vinne zaidi ilikuwa ni ukombozi mkubwa kwa hospitali yake.

"Tunashukurui Benki ya KCB kwa msaada huo, umekuja kwa wakati ambapo hospitali ilikuwa ikikabiliwa na changamoto nyingi. Amezitaka kampuni zingine ziige mfano wa benki ya KCB", alisema Dk Luwoga.

0 Post a Comment:

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Bluestar kuitambulisha singo yake mpya

Wednesday, January 30, 2013 Woinde Shizza 0 Comments


MSANII wa mjini Arusha anayekuja kwa kasi katika mziki wa kizazi kipya
hapa nchini Hamisi Omari(20)maarufu kama Bluestar anatarajia kuachia
singo yake ya tatu inayokwenda kwa jina la Tunachafua.

Akizungumza na gazeti hili amesema kuwa singo hiyo ambaye
amemshirikisha Mr Blue na Swaga Boy na kurekodiwa katika studio ya
Danlumark kwa Macko P ya jijini Dar es Salaam itaanza kusikika rasmi
wiki hii katika vituo mbalimbali vya redio na kutazamwa katika
luninga.

“Nawataka wapenzi wa muziki wa kizazi kipya na mashabiki wangu kwa
ujumla wakae mkao wa kula kupokea wimbo huo kwani ni moto wa kuotea
mbali”alisema Bluestar.

Amezitaja nyimbo zake mbali ambazo tayari aliishazitoa mwaka jana kuwa
ni Digidagi aliyemshirikisha Chris G ambayo ameirekodia katika studio
ya Fnock kwa Sumtimber na Njoo aliyeirekodia katika studio ya
Dunlumark.

Msaanii huyo ambaye alianza muziki mwaka jana amesema kuwa matarajio
yake ni kuja kuwa mwanamuziki maarufu sana ndani na nje ya nchi na
kwamba katikati ya mwaka huu atatoa albamu yake ya kwanza na kutoa
wito kwa mashabiki kumuunga mkono.

0 Post a Comment:

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

UN YAENDESHA MAFUNZO KUHUSU SHUGHULI ZA UNDAP NA HAKI ZA BINADAMU KWA WAANDISHI WA HABARI VISIWANI ZANZIBAR

Tuesday, January 29, 2013 Woinde Shizza 0 Comments



Afisa habari ngazi ya Taifa wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi.Usia Ledama akieleza nia ya Umoja wa Mataifa Tanzania kuendesha mafunzo kwa waandishi wa habari wa Visiwani Zanzibar juu ya Haki za binadamu na jinsi Mpango wa msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP) unavyoshirikiana na Serikali ya Zanzibar katika maeneo matatu muhimu ambayo ni Uchumi, Kupunguza umaskini na Utawala na uwajibikaji. Semina hiyo imefanyika katika Hoteli ya Zanzibar Ocean View visiwani Zanzibar.
Mratibu wa FAO Ofisi ya Zanzibar Ali Haji Ramadhan akitoa hotuba ya makaribisho katika mkutano na waandishi wa habari wa Visiwani Zanzibar ambapo amesema wanatarajia kupata mawazo mengi zaidi ya kujenga kutoka kwa waandishi ambapo yatasaidia Umoja wa Mataifa pamoja na Serikali kuihudumia nchi kwa upeo wa juu zaidi.
Mwakilishi wa mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa Zanzibar Anna Senga akizungumza na waandishi wa habari wa visiwani Zanzibar kuhusu changamoto wanazokabiliana nazo wao kama UN katika kutekeleza hoja za mipango wa maendeleo (UNDAP) kutokana na kuchelewa kupewa majibu na uchelewashaji wa utekelezaji wa mipango ya maendeleo.
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mafunzo hayo ambapo ameelezea Mpango Mkakati wa UNDAP visiwani Zanzibar ikiwemo kutoka ufafanuzi wa mafanikio pamoja na changamoto zinazoukabili mpango huo.Amesema mpango huu ni wa pamoja kwa ajili ya Tanzania unaendena na mafanikio ya malengo ya maendeleo ya kimataifa ambapo unachukua nafasi ya program za pamoja na miradi mingi inayodhaminiwa na UN chini ya Model ya misaada ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa kwa mpango wa kazi moja ulioshikamana kwa ajili ya mifuko ya fedha, program na wakala zote za Umoja wa Mataifa nchini Tanzania.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo hayo ya siku moja wakimsikiliza Afisa Mawasilano wa Umoja wa Mataifa nchini Hoyce Temu.
Katibu wa Chama cha wanasheria wanawake Zanzibar Hamisa Mmanga Makame akitoa somo katika mafunzo hayo ambapo amezungumzia masuala ya Haki za Binadamu, umuhimu wa kuzingatia jinsia na wajibu wa vyombo vya habari katika kuleta usawa.
Afisa Mipango mwandamizi wa shirika la kazi duniani (ILO) Anthony Rutabanzibwa ambapo amevipongeza vyombo vya habari vya Afrika Mashariki kwa kutoa kipaumbele katika habari zinazohusu haki za binadamu na kuwataka waandishi kuzingatia zaidi habari za kiuchunguzi ili kuwa na uhakika zaidi na yale wanayoaandika ikwemo kujua chanzo cha habari unayoitoa.
Mwenyekiti wa UNCG Yusuph Al Amin akielezea mada ya umuhimu wa mawasiliano kwa maendeleo na kuwataka wamiliki wa vyombo vya habari na serikali kwa ujumla kubadilisha sera zinazosimamia vyombo hiyo ili ziweze kutoa fursa kwa waandishi kuwa huru katika uandishi na kuripoti habari bila kubanwa.
Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Zanzibar Hassan Khatibu, Mratibu wa FAO Ofisi ya Zanzibar Ali Haji Ramadhan, Mwakilishi wa mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa Zanzibar Anna Senga, Mwezeshaji wa mafunzo hayo mwandishi mkongwe Salim Said Salim na Mwenyekiti wa UNCG Yusuph Al Amin.
Rais wa Umoja wa vilabu vya waandishi wa habari Kenneth Simbaya akitoa maoni yake kuhusiana na nini kifanyike katika kuboresha tasnia ya habari ambapo ameshauri mafunzo kuendelea kutolewa si tu kwa waandishi pia kwa wamiliki wa vyombo vya habari.
Pichani Juu na chini ni baadhi ya waandishi ws habari wa visiwani Zanzibar wakichangia mawazo yao wakati wa mafunzo hayo.
Afisa mipango wa Baraza la Habari Tanzania Ofisi ya Zanzibar Shifaa Said Hassan akichangia hoja wakati wa mafunzo hayo.
Sehemu ya waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo ya siku yaliyoendeshwa na Umoja wa Mataifa visiwani Zanzibar.
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu akijadili jambo na wafanyakazi wenzake wakati wa mafunzo hayo

0 Post a Comment:

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

CHADEMA SASA WAPANGA SAFU...., KUINGIA IKULU 2015

Tuesday, January 29, 2013 Woinde Shizza 0 Comments


  Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akifungua mkutano huo
 Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akimkabidhi kadi ya uanchama wa chama hicho aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Bara wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Clemence Tara baada ya kujiunga na chama hicho.
 Katibu Mkuu Dk. Willbroad Slaa akizungumza katika mkutano huo.
 bungo John Mnyika akitete jambo na Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Willbroad Slaa (kulia) wakati wa Kikao cha dharura cha Baraza Kuu la Chadema kilichofanyika jijini Dar es Salaam, leo.
  Katibu Mkuu Dk. Willbroad Slaa akisalimiana na baadhi ya wajumbe katika mkutano huo.
 Mbunge Kigoma, Zitto Kabwe akiwasikiliza kwa makini wajumbe wa kikao cha dharura cha Baraza Kuu la Chadema kutoka mkoa wa Mtwara.
 Muasisi wa Chadema, Edwin Mtei akiingia katika ukumbi wa mkutano huku akifuatana na Mwenyekiti wa Chadema, Freema Mbowe.
 Picha juu na Chini sehemu ya wajumbe wakiitikia  Peoples Power
Sehemu ya Wabunge wa Chadema
  Wajumbe wa mkutano.
 Baadahi ya wabunge wa Chadema wakiwa katika kikao hicho.
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika(katikati) akiwa amepozi na baadhi ya wajumbe.Picha zote na Mdau Dande Francis

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepitisha mpango mkakati wake wa kuelekea kushika dola mwaka 2015 kwa kumega madaraka ya makao makuu katika kanda kumi.
Maazimio hayo yalipitishwa na Kamati Kuu (CC) juzi kwa agenda moja kubwa ambayo ni kupitisha mpango mkakati wa mwaka 2013 ili kushinda chaguzi zote kuanzia serikali za vitongoji, vijiji na mitaa mwaka 2014 na Uchaguzi Mkuu 2015.
Akizungumza na wajumbe wa kikao cha dharura cha Baraza Kuu jana, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema kuwa mpango mkakati huo umelenga kufanya mabadiliko ya uongozi kuanzia ngazi ya taifa kwenda katika majimbo na kukipanga upya chama hicho kwa mustakabali wa taifa.
“Mtakumbuka kwamba wakati tunakianzisha chama chetu, tulizungumzia sera ya majimbo na kuainisha kazi zake…sasa tumeanza kupanga kazi zenyewe kwa kugawa majukumu katika kanda kumi.
“Tunataka tuishi vile tunavyosema kwa kuwa katika miaka mingi ya kuwa chini ya uongozi wa serikali ya CCM, wananchi wamekuwa wakiamriwa mambo yao na kundi dogo la watu wanaojikusanya sehemu moja ya nchi, hilo kwetu si mfano bora wa uongozi,” alisema.
Mbowe aliongeza kuwa katika miaka 20 ya kuhimili misukosuko ya kisiasa chama hicho kimejifunza mengi na sasa kiko tayari kushika dola ndio maana wameanza kugawa majukumu kwa wananchi kupitia uongozi wa kikanda.
Alisema kuwa wamejiandaa kwa mashambulizi ya aina zote na sasa jukumu kubwa la kila kanda litakuwa ni kuhakikisha kila mwananchi anaiunga mkono CHADEMA katika eneo atakalokuwa.
Mwenyekiti huyo alitaja kanda hizo na mikoa husika kuwa ni Kanda ya Ziwa Magaharibi (Mwanza, Geita, Kagera), Ziwa Mashariki (Mara, Simiyu, Shinyanga), Ziwa Magharibi (Kigoma, Tabora, Katavi) na Kati (Singida, Dodoma, Morogoro).
Zingine ni Kata za Nyanda za Juuu Kusini (Mbeya, Ruvuma, Iringa), Kusini (Lindi na Mtwara), Mashariki (Pwani, Dar es Salaam na Tanga), Kaskazini (Kilimanjaro, Manyara, Arusha), Pemba na Kanda ya Unguja.
Mbowe alisema katika kuhakikisha vikosi hivyo vinafanya kazi zake vizuri, kila kanda itajengewa ofisi, kununuliwa magari, pikipiki na vifaa vyote vya ofisini na za mikutano.
“Lengo la mkakati huo pia ni kuhakikisha CHADEMA inasimama katika chaguzi zote bila kupingwa…tunataka CCM ndiyo ipingwe katika chaguzi na hili tutalifanikisha,” aliongeza.
Katika suala zima la Muungano, Mbowe alisema uwepo wa serikali tatu hauepukiki kwa kuwa tayari Tanzania Visiwani wameshakuwa na serikali yao hivyo ni jukumu la Watanzania Bara kupata serikali ya Tanganyika na kisha kuwepo na serikali ndogo ya Muungano.
Alisema serikali tatu inawezekana ikiwa viongozi wataacha unafiki wa kusema muungano utavunjika huku tayari wakitoa uhuru wa Zanzibar kuwa na Rais, bendera na wimbo wao ya taifa.
Tunawaunga mkono wenzetu Wazanzibar katika kupigania uhuru kamili na kwa sasa sisi ndio tunaoonekana wa ajabu kushindwa kuuliza serikali ya Tanganyika,” alisema.
Mbowe pia aligusia tume huru ya uchaguzi akisema serikali ihakikishe Watanzania wanapata tume hiyo kwa kuwa tayari hata viongozi wa chombo hicho wameshatoa maoni na kutaka wapewe uhuru wa kufanya kazi.
Alisema serikali kama inafikiri kuwa CHADEMA itaingia katika uchaguzi wa 2015 ikiwa chini ya tume iliyopo sasa watakuwa wanajidanganya na badala yake watalazimisha upatikanaji wa tume hiyo.
Wailiza CCM Kagera
Katika hatua nyingine chama hicho kimeiliza CCM katika uchaguzi mdogo wa vijiji na vitongoji uliofanyika wilayani Muleba mkoani Kagera Jumapili iliyopita.
Licha ya wilaya ya Mulebe yenye majimbo mawili ya uchaguzi kusini na kaskazini yakiwa chini ya CCM, CHADEMA imeweza kunyakuwa viti vingi vilivyokuwa vikishikiliwa na chama hicho tawala.
Katika uchaguzi huo CHADEMA ilinyakuwa vijiji vitatu kati ya vitano katika jimbo la Muleba Kusini linaloongozwa na Prof. Anna Tibaijuka ambavyo ni Kasenyi, Kabunga na Ihangilo.
CHADEMA pia imechukua vitongoji sita vya CCM kati ya 12 vilivyofanya uchaguzi. Vitongoji hivyo ni Nyamagojo, Mushumba, Nyakabingo, Kyamyorwa, Katanda na Kyogoma.
Katika Jimbo la Muleba Kaskazini, linaloshikiliwa na Charles Mwijage, CCM ilipoteza vijiji viwili vya Katoke na Kahumulo kati ya vitano vilivyofanya uchaguzi huku vitongoji vinne vya Rundu, Kalee, Lwanganilo na Kituvi vikiangukia kwa CHADEMA.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu kutoka Muleba, Katibu wa Baraza la Vijana wa Taifa (BAVICHA), Robert Rwegasira, alisema wamepata ushindi huo kutokana na wananchi kuanza kuwaamini.
Mafanikio hayo yametokana na hamasa ya vuguvugu la mabadiliko la CHADEMA (M4C) ambalo lilifanyika katika mkoa wa Kagera Novemba mwaka jana.
Katika jimbo la Muleba Kusini, CHADEMA ingeweza kupata viti vya vitongoji zaidi ya idadi iliyopata kwani walisimamisha wagombea tisa kati ya 12 huku nafasi tatu wakiwaachia CUF na NCCR-Mageuzi ambao hawakuambulia chochote.

0 Post a Comment:

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia