JINSI MABADILIKO YA TABIA NCHI YANAVYO MUHATHIRI MWANAMKE

 

Na Woinde Shizza , ARUSHA

Lesika Simoni akiwa kama mama wa familia anaeleza zaidi namna anavyoathirika na mabadiliko ya tabia nchi hususa ni katika eneo analoishi ambapo anadai kuwa  ukame uliokuwepo wa muda mrefu umemsababishia hata uchumi wake kuyumba. 


Mmoja wa mwananchi wa Kijiji cha  cha Elkaria kilichopo katika kata ya Sepeko wilayani Monduli akichota maji nje ya nyumba ya mmoja wa mwananchi ambaye ananunua maji mjini Arusha Kwa bei ya shilingi 350000 na kuja kuuza Kijijini hapo Kwa bei ya shilingi 1000 Kwa dumu la lita 20


 Pia amekuwa akipata tabu ata ya kupata maji ya kunywa yeye na familia yake ,mifugo na hata ameshidwa kufanya kilimo  kutokana na ukame


Anaenda mbali zaidi na kusema muda mwingine anashidwa hata kutimiza majukumu yake kama mlezi anae hudumia familia kwa karibu zaidi mabadiliko haya  humfanya kuwa katika mazingira hatari zaidi wakati wa  ukame unapotokea kama  kipindi hichi.

Changamoto zipi zinamkumba katika kipindi hichi?

Anaenda mbali zaidi na kubainisha kuwa kuna matatizo mbalimbali ambayo yamemkumba kutokana na mabadiliko haya ambapo alisema kitu kikubwa kinacho mtesa ni ukame uliopo katika kijiji chao


Mbuzi wakiwa wanakula vumbi na mabaki ya majani yaliyokauka kutokana na ukame

Ukame


Amebainisha kuwa katika kijiji chao wanakabiliwa na tatizo la ukosefu wa maji safi na salama ya kunywa wao pamoja na familia yake ambapo anafafanua zaidi na kueleza kuwa imefikia hatua wanalazimika kununua maji kutoka mji wa  Arusha mjini   karibia kilometa 37  ambayo yanafutwa na mmoja wa wananchi na kuyaleta kijiji hapo ambapo wanauziwa kwa shilingi 1000 kwa ndoo moja ya lita 20

 

“mimi kiukweli mabadiliko haya ya tabia nchi yameniathiri kwa kiasi kikubwa kwanza katika swala la maji sisi hapa kijijini kwetu hatuna mradi wowote wa maji tulikuwa tunategemea maji kutoka katika mto Nanja ule pale unaouona lakini kama unavyoona mto huu umekauka na mbali ya kukauka ,  maji haya kidogo unayoyaona hayafai ata kupikia chakula kwani ukipikia ugali unabadilika badala ya kwa na rangi nyeupe unakuwa  wa kijani na pia unakuwa na ladha mbaya ya magadi  ambapo  ukipikia chakula hakifai hata kuliwa”alisema

 Ameathirikaje katika kilimo ?

Anaeleza kuwa  kwa upande wa kilimo ameathirika sana kwa kuwa awali alikuwa anategemea  kulima mazao kama mahindi na maharage lakini  kutokana na ukame uliopo ameshindwa kulima




“uku kwetu pia tumezoea kulima kwa msimu mmoja lakini msimu huo ulikuwa unatusaidia kupata kilimo ambacho tuta uza mazao na hapo hapo tutapata chakula kwa ajili ya watoto  lakini kinachoniumiza nikiangalia   sasa hata hicho chakula tu chakuwapa watoto atupati apa kwetu gunia la mahindi limefika hadi shilingi laki na nusu na ukiangalia mazingira yetu ni ngumu kununua  watoto wanakufa njaa  ,tuliomba serikali wakatupatia mahindi kwa bei nafuu ya shilingi elfu 80000 lakini pia tunashindwa kwenda kuyachukuwa kwakuwa hatuna ela  ya kununua na hata kusafirisha kwa iyo mimi kama mimi naweza sema nimeathirika sana na haya mabadiliko yatabia nchi naomba nimuombe Rais aangalie tu namna ya kutusaidia “alifafanua




 

ASASI ZISIZO ZA KISERIKALI ZAONGEA ?




Mkurugenzi wa Shirika la  ustawi wa wanawake na watoto (Mimutie  women organization )MWO  Mery Mushi  anaeleza zaidi   baadhi ya athari za mabadiliko hayo ya tabia nchi kwa mwanamke

Anaeleza kuwa wanawake huwa katika hatari zaidi za kuathiriwa na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi, na haswa katika mazingira ya umasikini, kutokana na uwezo wao mdogo wa kukabiliana na majanga kama vile kiangazi na mafuriko

 

Mabadiliko ya tabia nchi yanavyowaathiri wanawake  yanawaumiza kwa namna kubwa  kwa kuwa ukiangalia wanawake ndio wanapata shida kubwa pale wanapokuwa wenyewe ni watafutaji haswa  katika nyakati hizi ambazo asilimia kubwa ya wanawake wamekuwa ni watafutaji wa familia zao  hasa kwa jamii za pembezoni pamoja na wale waliopo mjini

 

Tukiangalia kwa jamii za pembezoni  tunaona kwamba wao wanaathirika zaidi wanawake wa vijijini kwa mfano  kwa kipindi hichi kumetokea wimbo la wafugaji  kuhama maeneo yao  na wanavyohama  na mifugo imekuwa nayo inaondoka  sasa inapo ondoka mifugo wanaondoka na vijana wa kiume au watoto wa kiume  lakini pia ile  mifugo ilikuwa ikikaa nyumbani ilikuwa inawanufaisha wa njia nyingine aidha ya kuwapatia maziwa   ambapo yale maziwa walikuwa wanaweza  kusaidia Kwa kutumia kwa kuwapa watoto au  kwa kuuza kwenye  jamii zao

 

Bei kuendelea kuwa juu kutokana na mabadiliko ya tabia nchi

-Mvua zimechelewa kunyesha  hivyo zimepelekea bidhaa nyingi  au mazao mengi kutoweza kupatikana kiurahisi  kwa hiyo hii imechangia kwa kiasi kikubwa kipato cha mwanamke kuanza kushuka kwa sababu wanakosa  munkhari  ya kuweza kufanya biashara zao kutokana na namna ambavyo mitaji yao ilivyokuwa mwanzo na sasa hivi inashuka kutokana na  vile ambavyo mitaji ina kuwa  labda ilikuwa mtu anamtaji wa elfu 50000 lakini  bidhaa zimeenda kuongezeka bei sokoni  kwa hiyo mtaji wake aliokuwa nao hauwezi tena kununua vitu alivyokuwa akiviitaji hivyo anakuwa ajatimiza malengo yake aliyojiwekea .

 

 SERIKALI IFANYE NINI ILI JAMII HIZI  KUKABILIANA NA MABADILIKO  YA TABIA NCHI

-Jamii za kifugaji zipewe uelewa  wa nini cha kufanya pindi janga hili la mabadiliko ya tabia nchi linapotokea   ambapo  wanafunzi wanao soma vyuo vya kilimo pindi wanapotoka vyuoni  wapite katika jamii hizo na   kutoa elimu kwa wananchi   ya nini kifanyike mfano ukame ukitokea ,mafuriko na nk.

 

-Mabadiliko haya yapoadhiri wananawake kwa namna moja ama nyingine  serikali inatakiwa iangalie  namna gani itaweza kuwawezesha kiuchumi ili waweze kuendelea na shughuli zao za kuwaingizia kipato mfano kuwapatia mikopo ambayo itawasaidia kuendeleza biashara zao  ili waweze kufanikisha kazi zao za kila siku

 

WAANDISHI WA HABARI WAFANYE NINI

-Ili kukabiliana na mabadili haya ni wajibu wa kila mwaandishi wa habari na mtangazaji kutumia elimu yake  pamoja na kalamu yake  kuelimisha  uma kuhusiana na  mathara ya ukataji miti hovyo  na namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi pindi yanapo tokea

 

WANANCHI WAFANYE NINI IILI KUKABILIANA NA MABADILIKO HAYA


-Ni wajibu wa wananchi kutambua mathara ya uchafuzi wa mazingira ambayo yanapelekea  kuongezeka kwa mabadiliko ya tabia nchi

-Ni vyema wananchi wakajitaidi kupanda miti kwa wingi ,kutokata miti ovyo  ili kuondokana na janga hili

 

-Kila mwananchi awe balozi wa mwenzake wa kumueleza madhara ya mabadiliko ya tabia nchi ili kila mmoja ayajue

 

TAKWIMU ZA UMOJA WA MATAIFA ZINASEMAJE?


Kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa  zinaonyesha asilimia 80 ya watu wanaolazimika kuhama makazi yao kutokana na mabadiliko ya tabia nchi ni wanawake.

 

Majukumu yao kama walezi na wanao hudumia familia kwa karibu zaidi huwafanya kuwa katika mazingira hatari zaidi wakati wa mafuriko na ukame unapotokea.

 

 

Makubaliano ya mjini Paris mwaka 2015 yaliweka kipaumbele maalum cha kuwawezesha na kutambua kwamba wanawake huathiriwa kwa kiasi kikubwa zaidi katika jamii kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.

 

Wakati wa kiangazi wanaume wanaenda mjini na kuwaacha wanawake vijijini kuangalia jumuiya, Hivyo wanawake wanalazimikia kufanya kazi zaidi ili kutunza watoto bila msaada wowote.

 

 

Lakini sio wanawake wa maeneo ya vijijini peke yake ndio wanaathirika.

Duniani kote wanawake wanaathirika zaidi kutokana na umaskini na kutokuwa na uwezo mkubwa zaidi ya wanaume katika masuala ya kiuchumi hivyo hali ambayo huwafanya washindwe kujikwamua kutoka katika majanga ambayo yanaharibu miundombinu ,ajira na makazi yao.

 

 

Aidha zaidi ya nusu ya familia zinazo ishi mjini zinatunzwa na wanawake.



Wakati Katrina ilipotokea mwaka 2005,wanawake na watoto ndio waliathirika zaidi katika upande wa makazi ,afya na hata walikumbana na unyanyasaji wa kijinsia kama kubakwa.

Vile vile mabadiliko ya tabia nchi huathiri shughuli za kibinadamu, athari za hali ya hewa na maafa yanayotokea katika jamii husika huwa na athari tofauti kwa wanawake na wanaume.


About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia