MUGABE ATUMA UJUMBE KWA MASENETA WA MAREKANI



Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amewaambia maseneta wa Marekani
waliozuru taifa hilo kwamba watajutia kutofanya urafiki naye iwapo Donald
Trump atachaguliwa kuwa rais katika uchaguzi wa mwezi Novemba.

Maseneta hao Chris Coons na Adam Schiff waliambia gazeti la Politico nchini
Marekani kwamba walikuwa katika taifa hilo kuzungumzia kuhusu usafirishaji
wa wanyama mwitu na kwamba waliomba kukutana na rais huyo na
wakashangaa kwamba alikubali kuonana nao.

Maseneta hao wamesema kuwa Mugabe aliwataka kuelezea kwa nini Marekani
inaliwekea vikwazo taifa hilo ambapo walitoa sababu kadhaa.
Ni wakati huo ambapo bwana Mugabe aliwaambia: ''Wakati Trump
atakapokuwa rais mutatamani mungefanya urafiki nami''.
 
CHANZO:BBC

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia