Ticker

6/recent/ticker-posts

HAYA NDO MAMBO NILIOYAONA KILA MMOJA WETU AKIZUNGUMZIA MAANA YA ‘VALENTINE DAY’ NA MAADHIMISHO ,SASA WEWE MWENZANGU EMBU TUELEZE MAANA HALISI YA SIKU HII KWA JINSI UNAVYOELEWA NA JE INAFAIDA AU HAINA FAIDA KWA JAMII



down-arrow
Hervé Léger 
Hervé Léger  front
Hervé Léger  back
Hervé Léger  outfit
Hervé Léger  close up
down-arrow
Hervé Léger 
ntino.
Siku ya Mtakatifu Valentino hufahamika
kama Siku ya w


Jina “Valentino” ni Jina la
Mtakatifu wa Kiroma aliyeitwa
Vale
apendanao
wanaiita “Valentine Day”, ikiwa ni
maadhimisho ya mwaka, yaani kila
tarehe 14 Februari, Watu
husherehekea upendo na
kuthaminiana na kujaliana kati
ya watu wenye uhusiano
binafsi, na mara nyingi hutumika
kwa mahusiano ya kimapenzi.
ASILI YAKE:
Siku hii asili yake ni
baada ya wakristo wa zamani
kuteswa hadi kufa kwaajili ya
kuupenda Ukristo. Kihistoria
Mtakatifu Valentino alitumika
kama kiongozi wa dini kanisani
katika utawala wa Mfalme
Claudia. Mfalme Claudia
alimkamata Mtakatifu Valentino na kumfunga.
Mtakatifu Valentino aliteswa
kwaajili ya Imani yake ya
Ukristo na Kufa tarehe 14
mwezi Februari, 269 AD.
Kwaajili ya msimamo, na Imani
yake na kufa kwa kutetea
Ukristo, Papa Gelasius
aliitangaza tarehe 14 mwezi Februari Mwaka 496 AD, kuwa siku ya
Mtakatifu Valentino.
Je! Watu
wanasherehekeaje
siku hii?
Jinsi watu wanavyo
ichukulia siku hii ni
kutokana na TABIA ZAO ZILIVYO
au kiasi cha hofu ya
kumuogopa Mungu kilivyo.
Watu wengi huichukulia Siku hii
kama ni siku ya Mapenzi,
Wengine hufanya kama siku ya
kujenga mahusiano upya,
kupatana na wapendwa wao
au kufurahi na wale
wanaowapenda.
Ila sehemu
mbaya zaidi watu huchukulia
siku hii kama ni siku ya
KUFANYA MAOVU NA UFUSKA.
Hili ni Chukizo kwa Mungu, na ni Kinyume na Maana Halisi ya siku ya Mtakatifu Valentino (Valentine Day). Ni
bora Tuichukulie siku hii kidini
zaidi kama waasisi wa
Valentine walivyofanya. Mungu
aliupenda ulimwengu na
kumtoa mwanawe kama
kafara ya Dhambi zetu.
Ni vizuri
tukitumia mda tulio nao
kujitakasa na kutubu dhambi
zetu. Je! Sisi ni nini mbele za
Mungu zaidi ya wale waliokuwa
wanachinjwa na kuuawa
kikatili kwaajili ya kulinda imani
yao? HADI PUMZI YAO YA MWISHO
WALIMTAMKA KRISTO. Tuwaenzi
kwa kutenda wema tu.
Kile kidogo ulichonacho, jaribu kukitumia na Ndugu, Jirani, Rafiki, Watu wasiojiweza na Watoto wa Mitaani. Naamini utabarikiwa zaidi. Hiyo ndiyo Maana ya Siku ya Wapendanao.


Valentine Day ni Nini?Nini Asili Ya Valentine?Ni Sikukuu Ya Kipagani?

Leo nimeona niongelee kidogo nini maana ya Valentine kwa asili yake kisha kila mtu kwa Imani yake na mapana yake akatambua kuwa anapokuwa sehemu ya Valentine Day anakuwa ana adhimisha nini na kwa sababu gani wengi tunasheherekea kama sio kuadhimisha Valetine Pasipo kujua asili yake.
Valentine’s Day kama Sikukuu Ya Kipagani:
Valentine’s Day si siku ya Sikuu ya Kikristo, hata kama jina lake asili yake inatokana na Ukristo  haiwezi kuhalalisha sasa Valentine kuwa Siku Ya Kikristo. Tukiangalia suala sikukuu hii kwa jicho la tatu, hatuoni uhusiano mkubwa kati ya watu wa Mungu  na Malove dove yaani mapenzi. Kuna mambo mengi yanaweza ibua mjadala na kutokuelewana miongoni mwa jamii ya wakristo na wasomi juu ya chimbuko ya Siku ya wapendanao al maarufu Valentine’s Day. Hatutaweza kamwe kuwa na uwezo wa kuwa na jibu muafaka kuhusu uhalali wa kusheherekea valentine kwa namna moja ama nyingine kutokana na tofauti za  kitamaduni na kidini ili mwisho wa siku tujenga upya hadithi kamili na madhubuti, lakini uhusiano kipagani hadi sasa na nguvu zaidi kuliko wale wa Kikristo kwa namna yoyote ile.

Februari 14 & Juno Fructifier au Juno Februata (
February 14th & Juno Fructifier or Juno Februata)
Enzi hizo Warumi walikuwa wakisheherekea  kwa kupumzika kabisa kama sikukuu ya muungano ama sikukuu zozote za hapa bongo kila  Februari 14  kama siku ya kutoa heshima kwa Juno Fructifier. Huyu Juno Fructifier alikuwa nani?huyu alikuwa  Malkia wa miungu ya Kirumi ambaye alikuwa Mungu mke kama mmoja wapo wa  miungu ya ndoa kama ndo zilikuwa zinasua sua basi tarehe 14 February ndo ilikuwa kama siku ya kufanya matambiko. Enzi hizoilikuwa  Katika sherehe moja, wanawake walikuwa wakiwasilisha majina yao na kuweka kwenye kisanduku na baadae wanaume wangepita mbele ya kisanduku hicho na kila mmoja kujitwalia jina moja. Kilichokuwa kinatokea katika sherehe kila aliyejiokotea jina hulitaja na kujitwalia huyo mwanamke kuwa mwanandoa kwa muda wote wa sikukuu wakati mwingine ilikuwa ni mwanandoa wako kwa mwaka mzima mpaka Valentine nyingine akaweke jina pale kwenye kibox. Mila hii ilitumika kukuza Jamii ya Kirumi kwa maana ya uzazi na maisha mengine kwa ujumla, kasheshe kama ulibeba ile ya mwaka mzima then Valentine imefika kisha unataka kubadilisha halafu uliyembeba mwaka jana mjamzito tehe tehe imekula kwako.

Post a Comment

0 Comments