Ticker

6/recent/ticker-posts

JOSE KAMILION KUNOGESHA SHINDANO LA KUMSAKA REDD'S MISS ARUSHA KESHO KATIKA VIWANJA VYA TRIPLE A

 MMOJA  wauguzi wa hospitali ya maria stopes Hamza Mzira akiwa anagawa vipeperushi kwa warembo


 Dr,Sober Mzighani  akiwa anawapa elimu warembo wanaogombania ulibwende wa jiji la Arusha waliotembelea hospitali ya maria stopes





 Picha ikionyesha warembo wakiwa wanatembelea baadhi ya ofisi za hospitali hiyo




warembo wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wauguzi wa hospitali hiyo wakati walipomaliza kupewa elimu

warembo wanaogombania taji la redd’s miss arusha wakiwa na mrembo ambae anasubiri kuachia ngazi ya urembo wa jiji la arusha Glory Stephen   nje ya hospitali ya maria stopes








Picha ikionyesha warembo wakiwa wanatembelea baadhi ya ofisi za hospitali hiyo




WAREMBO 13 wa Redd’s Miss Arusha 2014 jana  wametembelea kituo cha uduma za afya cha Maria stopes kwa ajili ya kujifunza Afya  ya uzazi wa mpango na maradhi mbalimbali ya saratani ya kizazi
Akiongea na warembo hao Msimamizi wa hospitali hiyo ya mariastopes ya jijini hapa  Dr,Sober Mzighani alisema kuwa hospitali yao imeamua kutoa elimu hiyo kwa warembo hawa ambao ni vijana ili waweze kusambaza ujumbe kuhusu uzazi wa mpango na afya ya uzazi.

Alisema kuwa elimu hii watatoa kwa  vijana wote ili wasambaze kwa wananchi nchi wote uku akisema kuwa ,vijana wengi ndio wananguvu  na uwezo wa kusambaza taarifa hizi kwa jamii .
Kwa upande wa mrembo ambaye anashikilia taji la Redd’s missArusha Glory Stephen  alisema kuwa anawashukuru sana wauguzi wa maria stopes kwa jinsi walivyowapa elimu kwani wengi wao walikuwa awajui elimu ya uzazi .

Alisema kuwa vijana wengi wamekuwa wafanya ngono uzembe wengine wamekuwa wanapata mimba pasipo mpangilio lakini kwa kutumia elimu hii na kwa kutumia nafasi zao ambazo wanazo watajitaidi kuelimisha wengine kuhusiana na uzazi wa mpango

Kwa upande wa muaandaji  wa Redd’s Miss Arusha, Faustine Mwandago, alisema kuwa warembo hao ni washindi waliotokana na mashindano ya ngazi ya vitongoji yaliyomalizika hivi karibuni.
Mwandago, aliwataja warembo hao kuwa ni Janeth Alex (20), Neema Urio (19), Lilian Deus (18), Leila Thomas (19), Husna Hamis (20), Happyness Tarimo (19), Eveline Baasa (19), na Marry Joel (21).
Wengine ni Neema Charles (19), Dyness Peter (21), Rahisa Mboye (21), Joselyn Mirashi (21), na Amber Gladys (20).
Mwandago alisema kuwa shindano hilo litasindikizwa na burudani ya aina yake kutoka kwa msanii anaewika katika nchi za afrika mashariki  Jose kamilione pamoja na wasanii mbalimbali wa Mkoa wa Arusha.

Shindano hili la kusaka mlimbwende wa mkoa wa Arusha (Redd’s miss Arusha) linatarajiwa kufanyika Juni 7 katika viwanja vya ukumbi wa Triple A na kiingili katika shindano hili vip watalipa kiasi cha shilingi 60000 huku viti vya kawaida wakilipa 30000.

Post a Comment

0 Comments