Ticker

6/recent/ticker-posts

HAYA NDIO YALIOJIRI BAADA YA CHATU MKUBWA KUUWAWA JANA


BAADA YA chatu mkubwa kutokeza katika nyumba ya mfanyabishara mkubwa wa jiji la Arusha mengi yaibuka 
 akielezea tukio halisi mmoja wa mtoto wa mwenye nyumba hiyo ambaye jina lake alijafahamika alidai kuwa yeye na mfanya kazi walikuwa wanakunywa chai sebuleni ndipo wakasikia kitu kinagonga katika moja ya chumba ambacho walishapigwa marufuku kukifungua

aliasema kuwa wakati kinaendelea kugonga ndipo walipoamua kwenda kufungu chumba hicho wakiwa na mfanya kazi ili waone nini kinachogonga

mara tu baada ya kufungua chumba kile walisema walikutana uso kwa uso na chatu huyo ndipo walipoamua kukimbia na kupiga kelele



kutokana na shutuma hizi za kudaiwa chatu huyu alikuwa anafugwa na mfanyabiashara huyo aliyetambulika kwa jina la joseph magessa timu nzima ya libeneke la kaskazini ilijitaidi kutafuta ukweli huu kwa kumtafuta mwenye nyumba magesa au mke wake ili aelezee tukio hili lakini hazikufanikiwa kwani  tulivyofika nyumbani akuwepo na tulivyojaribu kupiga simu yake haikupatikana hatukuishia apo bali tulimtafuta pia mke wake lakini atukumpata.

 taswira halisi ya eneo la tukio imeonekana watu wengi kutoka katika sehemu mbalimbali wakienda kushuhudia kama tukio hilo ni lakweni na wengine walienda kuangalia  mabaki ya nyoka uyo aina ya chatu 


Post a Comment

0 Comments