Ticker

6/recent/ticker-posts

NICE & LOVELY MISS TANGA 2014 WACHUKUA NA KURUDISHA FOMU ZA KUSHIRIKI


Gari aina ya Toyota Vitz atakalokabidhiwa mshindi wa shindano hilo la Nice & Lovely Miss Tanga 2014

Mratibu wa Mac D Promotions, waandaaji wa mashindano ya Nice & Lovely Miss Tanga 2014, Benson Jackson leo amezungumza na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari katika hoteli ya Mkonge jijini Tanga, ambapo amesema mpaka sasa jumla ya washiriki 19 wamechukua na kurudisha fomu za kushiriki shindano hilo linalosubiriwa kwa hamu kubwa na wakazi wa jiji la Tanga, shindano ambalo litafanyika jumamosi ya tarehe 21/ 06/ 2014 Mkonge Hotel.

Shindano hilo limedhaminiwa na Nice & Lovely, EATV, Redd's, Tanga Beach Resort, Breeze Fm, CXC Africa, Rweyunga Blog na Mwambao Fm.

Post a Comment

0 Comments