Ticker

6/recent/ticker-posts

TAHA KUSHIRIKIANA NA SIDO WAANDAA MONYESHO YA WAJASIRIAMALI WADOGO WADOGO




 meneja wa shirika la SIDO  Isdori  Kiyenze Akiwa anaongelea maonyesho hayo jinsi yatakavyokuwepo ambapo alisema zaidi ya wafanyabiashara wadogo wadogo 250 watashiriki


Mkurugenzi wa TAHA, Bi Jacqueline Mkindi akiwa anawaelezea waandishi wa habari nia haswa ya wao kama taha kushiriki kuandaa maonyesho haya

 waandhishi wa habari wakiwa   kikazi zaidi

Tanzania Tanzania Horticultural Association (TAHA)  kwa kushirikiana na shirika la kuhudumia viwanda vidogo vidogo (SIDO) wameandaa maonyesho ya siku sita kwa ajili ya kuwaelimisha wananchi pamoja na wajasiriamali jinsi ya kuzifanya bidhaa zao kuwa na ubora wa kimataifa.

Akiongea leo na waandishi wa habari meneja wa shirika la SIDO  Isdori  Kiyenze alisema  kuwa maonyesho hayo yanatarajiwa kuanza rasmi tarehe saba  hadi kumi na mbili ambapo alibainisha kuwa yanatarajiwa kufunguliwa june 9 na waziri wa viwanda na biashara Abudala kigoda katika viwanja vya makumbusho vilivyopo jijini hapa.

Alisema kuwa nia haswa ya kuandaa maonyesho haya  nikuwajengea uwezo mkubwa wajasiriamali wadogo wadogo na kuwafundisha namna  mbalimbali za kisasa za kutengeneza bidhaa zao na kuzihifadhi (kuparki) katika hali nzuri ya kimataifa ikiwa ni pamoja na kusindika .

Alisema kuwa pia watatoa mafunzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwafundisha teknoligia  mbalimbali za kisasa zinazofanya kazi katika kipindi hichi.

“unajua  wajasirimali wetu wengi wamekuwa wanatengeneza vitu  vizuri na vyenye ubora ambavyo avina tofauti na vya nchi zingine  lakini vimekuwa avithaminiwi sasa sisi kama sido tumepita katika supermarket mbalimbali tumeangalia vitu vilivyosindikwa tukaona sasa havina tofauti na vitu vyetu ambavyo tunalima tukaamua kuwapa elimu wajasirimali wetu sasa kunawengine ambao hawakupata elimu ndo tunataka tuwape katika kipindi hichi cha maonyesho haya”alisema Kiyenze

Kwa upande wa Mkurugenzi wa TAHA, Bi Jacqueline Mkindi alisema kuwa  wao kama taha wameamua kushirikiana na sido kuandaa maonyesho haya ili kuweza kuwajengea uwezo zaidi wajasirimali wadogowadogo .

Alisema kuwa mara nyingi wamekuwa wakiweka nguvu zao  nyingi kwa wazalishaji lakini kwa sasa wameamua kungia na huku ili kuweza kuwasaidia wafanyabiashara hawa wadogo wadogo kusogea mbale zaidi na kuelimika ambapo wakielimika  kutakuwepo na  ongezeko la dhamani.

Aidha wamesema kuwa kwa sasa ivi wameamaa kuwatafuta na kufanya kazi nao ili kuweza kuwasaidia kutangaza bidhaa zao ambazo zinatengenezwa hapa nyumbani.

Post a Comment

0 Comments