RAIS SAMIA KUFANYA ZIARA YA SIKU MBILI MKOANI ARUSHA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara ya siku mbili Mkoani Arusha kuanzia Machi Mosi, 2026, akitarajiwa kukutana na kuzungumza na Rais wa Jamhuri ya Ghana Mhe. John Dramani Mahama kwenye Ikulu ndogo Mkoani Arusha.
Kulingana na taarifa iliyotolewa leo Jumamosi Februari 28, 2026 na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla, Mhe. Mahama anakuja Mkoani Arusha kuhudhuria pia Mkutano wa Mahakama ya Afrika ya haki za binadamu utakaofanyika tarehe 2 Machi, 2026 Jijini Arusha.

0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia