Ticker

6/recent/ticker-posts

WAHANGA WA MAFURIKO KATIKA KIJIIJI CHA THEMI YA SIMBA WAPATIWA MSAADA WA CHAKULA


mzee wa kanisa la Waadventista wasabato  mtaa wa kijenge   Agrey Tumaini akiwa anagawa maindi kwa wananchi wa  kitongoji cha nyamagana 

Zaidi ya wananchi  50  wa kitongoji  cha Nyamagana  kilichopo katika kijiji cha Themi ya simba wilayani Arumeru MKoani Arusha ambao waliathiriwa na mafuriko yaliotokea mwisho mwa mwezi wa nne mwaka huu wamepatiwa msaada wa chakula na nguo kijijini hapa.
 Akikabidhi chakula hicho mzee wa kanisa la Waadventista wasabato  mtaa wa kijenge   Agrey Tumaini alisema kuwa wameamua kuwasaidia wananchi hawa kutokana na janga ambalo liliwakuta la kuingiliwa na mafuriko ya maji  ambapo yaliwasababishia nyumba pamoja na mazao yao kuezuliwa na maji hayo

Alisema kuwa wao kama kikundi cha WAMO  kutoka katika kanisa hilo waliguswa sana na tatizo hili ambalo liliwatokea hivyo wakaamua kujichanga na kununua vyakula ivyo na nguo kwa ajili ya wahanga hao wa mafuriko.

Alisema kuwa wameweza kutoa gunia kumi za mahindi ,maharage kunia tatu,unga wa ugali pamoja na nguo kwa ajili ya watoto  wa wananchi ambao walikubwa na janga hilila mafuriko.

“sisi tumeguswa sana na tukio hili wenzetu kukubwa na  mafuriko kwa kweli wameadhirika vikubwa kwani wengine awana sehemu zakukaa wengine walikuwa wamelima mazao yao kama mahindi yaliezuliwa na mafuriko hayo yaani kiukweli hadi sasa kuna watu awajui wataishije kwa mwaka huu lakini tumeona sio vibaya iwapo tukiwasaidia ichi kidogo  tulichonacho maana ata neno la mungu linasema  katika mathayo uwa mlikuja na njaa nikawapa chakula,mlikuja uchi nikawavisha sasa na sisi tumeamua kuwapa ichi kidogona tunawaomba watu wengine waendelee kujitokeza kwa wingi kuwasaidia wananchi hawa kwani wapo katika mazingira magumu sana”alisema Tumaini.

Akipokwa msaada huo mmoja wa wananchi hao alietambulika kwa jina la  Gidion Maganga alisema kuwa anashukuru sana kanisa hili la wa sabato kwa kuja kuwasaidia kwani kuna baadhi yao walikuwa hawajui hatima ya maisha yao kwani ata chakula kwao kupata ni tabu ..
Alisema kuwa pamoja kuwa kuna baadhi yaviongozi na taasisi ambazo zimewapelekea chakula kama maindi ,magodoro  pamoja na nguo lakini bado wanaitaji maada kwani mvua zile ziliwachukulia vitu vyao vingi ikiwemo mazao maindi waliokuwa wameyaifadhi ndani vyombo ,magodoro na sio ivyo tu lakini pia zileweza kumuua mwananchi mmoja.

Akizungumzia tukio hilo mwananchi mungine ambaye aliyejitaja kwa jina la Zainabu Minja alisema kuwa siku hiyo ya tukio lilitokea majira ya saa saba usiku wakati wamelala  huku mvua ikinyesha ndipo gafla waliona maji mengi yamekuja na kujaa ndani  ya nyumba  kitu ambacho kiliwaogopesha zaidi ni pa le maji yale yalivyoanza kusomba vitu.

“yaani ndugu muandishi usione apa yaani maji yalikuja na kasi unaona hii chuma ina uzitowa kilomia ndio niliichukuwa nikaishika na uyu ni mama yangu na unamuona alivyo mzee nilimwambia ashikilie iyo chuma akashika mwishowe mikono ikafa ganzi ndipo nikachukua kanga na kumfunga kiunoni nikaunganisha na chuma ili asipelekwe na maji ila nashukuru mungu alituona pamoja vitu vilizolewa lakini sisi ni wazima kwakweli”alisema bi Zainabu

Alitoa wito kwa wananchi serekali pamoja na taasisi mbalimbali kujitokeza kwa wingi kuwasiaidia kwani wapo katika halingumu sana  katika kipindi hichi.

Post a Comment

0 Comments