Ticker

6/recent/ticker-posts

MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BIMA LEO JIJINI ARUSHA YAZINDUA MFUMO WA KUTHIBITI UDANGANYIFU KATIKA BIMA ZA VYOMBO VYA MOTO

 Afisa wa bima kutoka  mamlaka ya usimamizi wa Bima  Arthur Mbena aakiwa anatoa maelekezo  ya mafunzo kwa afisa wa polisi kitengo cha usalama barabarani mkoa wa Arusha pamoja na wananchi waliofika eneo hilo jinsi ya kuhakiki  Bima yake ya chombo cha moto ni halali au bandia ni halali au ni bandia ,huu ukiwa ni mfumo mpya  unaotumia simu ya mkononi  au tovuti uliozinduliwa leo  ndani ya jiji la Arusha ambapo utasaidia wananchi kuepuka kuuziwa bima feki za vyombo vyao vya moto
 kamishina wa  mamlaka ya usimamizi wa bima nchini  Dkt.Baghayo Abdalah Saqware akiwa anaongea na waandishi wa habari mara baada ya kuzindua  mfumo wa kudhibiti udanganyifu katika bima za vyombo vya moto (TIRA MIS)
 meneja wa Mamlaka ya usimamizi wa Bima wa kanda ya kaskazini  Elieza Roikiza akiwa anamuelekeza mwananchi jinsi ya kuhakiki bima ambayo sio fek i 

 kamishina wa  mamlaka ya usimamizi wa bima nchini  Dkt.Baghayo Abdalah Saqware akiwa anawaelekeza baadhi ya maaskari wa  usalama barabarani jinsi ya kuhakiki bima feki na ambayo sio feki


 wamiliki wa bima wakiwa katika uzinduzi


Na Woinde Shizza,Arusha



Zaidi ya kesi  10 za kughushi nyaraka za bima zimefikishwa mahakamani  katika kipindi cha miaka mitatu na kati ya kesi hizo  watu watano wamehukumiwa  kwenda jela  na  mashauri matatu yakiwa yamekatiwa rufaa katika mahakama kuu  huku watu wawili  wakiwa wameamriwa kulipa faini.



Akiongea katika uzinduzi  wa kampeni  ya kuthibiti udanganyifu katika bima za vyombo vya  moto (TIRA MIS) kamishina wa  mamlaka ya usimamizi wa bima nchini  Dkt.Baghayo Abdalah Saqware alisema kuwa  kumekuwa na wimbi kubwa la  udanganyifu katika  soko la bima  linalohusisha utengenezaji na uuzaji wa stika na hati za bima bandia  hivyo wameamua kuanzisha kampeni hii ili kuweza kumaliza kabisa tatizo hili.



Alisema kuwa mamlaka hiyo  hadi sasa imeshawakamata wahalifu 10 na kati yahao kunawalifikishwa mahakamani na kuhukumiwa kwenda jela huku wengine wawili wakiwa wameamriwa kulipa faiini  kati ya shilingi milioni 20,000,000 hadi shilingi 40,000,000 kutokana na makosa waliyofanya .



Alisema kuwa   inakadiriwa hasara ya kiasi cha  asilimia 10% ya mapato yote  ya biashara ya bima  ya vyombo vya moto inaingia kwenye mikono haramu  ikiwa ni pamoja na wimbi la kughushi nyaraka za bima kuongezeka  ,huku uhalifu wa usafirishaji wa magari yanayopitia bandari zetu  na kupele nchi jirani (IT) pamoja na ule wa bodaboda unachangia kwa kiasi kikubwa  .



“stika hizi bandia zimekuwa zikichapishwa na watu wasio kuwa waaminifu na kusababishia hasara kubwa mawakala wa bima na makampuni ya bima kwa kuwapoteze mapato ambayo ndio hutumika kulipa hasara na majanga yanapotokea ,kutokana na haya yote  mamlaka sasa imeamua kutafuta njia mbadala kwa kutumia TEHAMA  ili kuondoa tatizo hili kwa kumuwezesha mkata bima kuhakiki taarifa za bima yake kwa kutumia teknolojia rahisi ambapo mamlaka imeanzisha mfumo  huu utakaotumika kuhifadhi na kuhakiki taarifa za bima  za vyombo vya moto “alisema Dkt.Baghayo



Kwa upande wake meja wa kanda wa  Mamlaka ya usimamizi wa bima  Elieza Roikiza  alisema kuwa utengenezwaji wa mfumo  huu umetokana na uwepo  wa bima bandia za vyombo vya moto kama magari ,pikipiki na aina zinginezo za vyombo vya moto hivyo wanaamini kabisa mfumo huu wa moto utakuwa rafiki sana kwa wanachi,na pia utamuwezesha mwananchi yeyote popote alipo Tanzania kuhakiki bima ya chombo chake kwa kutmia njia mbili za urahisi ambazo ni simu yake ya mkoni  pamoja na kufungua tofuti ya mfumo huu



Alisema kuwa mfumo huu utasiadia  kuondoa stika na hati za bima bandia,utarudisha imani  ya wananchi katika huduma za bima nchini,pia  itaongeza idadi   ya vyombo vya moto  vinavyokatiwa bima pamoja na  itaiongezea mapato  serikali yanayotokana na ushuru  pamoja na kodi inayotozwa katika bima za vyombo vya moto.

Post a Comment

0 Comments