Ticker

6/recent/ticker-posts

SHILOLE APATA AHUENI BAADA YA KUKALIWA KOONI NA BASATA

 
Hatimaye mwanamuziki nchini Tanzania, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, apumua baada ya kuwa na mawazo kutokana na sakata la kusambaa kwa picha zake chafu ambazo zilipigwa alipokuwa akitumbiza nchini ubelgiji mwezi uliopita.
Akihojiwa na runinga moja nchini amesema kuwa alikuwa na hofu sana na alikuwa hapati usingizi kutokana na jambo hilo kufika hadi Bungeni, jambo ambalo Serikali iliamua BASATA kumfanyia mahojiano.
SHILOLE 2
Amesema kuwa anamshukuru Mungu leo alienda BASATA, kuitika wito aliotumiwa juzi wameongea na anashukuru wamemuelewa na kudai kuwa hakuna tena tatizo kwani wale ni kama wazazi ambao kazi yao ni kuwaonya mtoto.
Ameongeza kuwa aliwaeleza tukio zima lilivyotokea na kumuelewesha kuwa mwangalifu katika mavazi kitu ambacho amedai ni sahihi kabisa na amewashukuru kwa sababu wamemuelewa na kudai kuwa sasa ana furaha na amani tele.

Post a Comment

0 Comments