BARA LA AFRIKA LATAKIWA KUJIPANANGA KUANDAA MIKAKATI YA KIUCHUMI

Bara la Afrika limetakiwa kujipanga katika kuandaa mikakati ya  kiuchumi na kuangalia mdororo wa kiuchumi unaoukumba ulimwengu kwa sasa likiwemo bara la ulaya kama changamoto ya kupambana na umaskini katika bara letu ilikufikia mafanikio waliofikia nchi kama China na Brazili.

Hayo yalisemwa na raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania dkt.Jakaya Kikwete wakati akifungua mkutano wa mwaka wa benki ya maendeleo ya Afrika(AfDB) jijini Arusha na kuwataka benki hiyo ya maendeleo kuwa mstari wa mbele kulikomboa bara hili kiuchumi.

Dkt.Kikwete alisema kumekuwa na miundombinu mibovu,kilimo kisichokidhi soko la ndani sanjari na kutotumia rasilimali zetu vizuri huku kunaliangusha bara hili kutopiga hatua za kiuchumi na kulifanya kuwa tegemezi kwa wahisani ndani ya bajeti zao.

Akawataka washiriki wanaoshiriki mkutano huo kutoa majawabu ya hali za kiuchumi yanaolikumba bara hili kwa sasa ilikufikia katika kilele cha mafanikio ya kiuchumi waliyonayo nchi zilizoendelea pia akatoa shukurani kwa wahisani wanaoendelea kuzisaidia nchi zetu.

Nae raisi wa benki ya maendeleo ya afrika Donarld Kaberuka alisema kuwa matumizi mabaya ya madaraka sambamba na vita vya wenyewe kwa wenyewe yanalifanya bara hili kuwa nyuma kimaendeleo na kuwataka kuwa na soko la pamoja la kimataifa kwa watafuta bidhaa na malighafi.

Kaberuka alisema kuwa kuwepo na mfumo wa kibiashara za kienyeji kati yetu nchi kwa nchi na baadae kuelekea katika masoko ya kimataifa kutafanya kuwa na mfumo sahihi wakuweza kujua hali la soko letu na jinsi ya kupanga bei.

“Naona fahari kusafiria bara bara kutoka Kenya hadi hapa Tanzania ambayo sisi kama benki tumeichangia uwepo wake  kwa kufanikisha barabara ya Nairobi hadi Arusha.

Mkutano huo wa siku tano unafikia kilele chake kwa uzinduzi wake ulifanywa na raisi Kikwete na mgeni wake raisi wa Aivory Coast Alasane watara na magavana kutoka mataifa wanachama wa benki hiyo na wageni mbali mbali mashuhuri kutoka mataifa mbali mbali ulimwenguni.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia