PREMIER PALACE YAFUNGULIWA RASMI ARUSHA

MKURUGENZI WA HOTEL, ALEX MARIWA AKIONGEA WAKATI WA UZINDUZI 
 WAFANYABIASHARA jijini Arusha wametakiwa kuacha mashindano na badala yake washirikiane katika kuhakikisha wanaongeza ajira na kukuza uchumi.
 Hayo yalisemwa juzi na mkurugenzi wa hoteli ya kitalii ya Premier Palace, Alex Mariwa alipokuwa akizungumza katika hafla fupi ya uzinduzi wa hoteli hiyo iliyopo Makao Mapya kata ya levelosi.
 Alisema kuwa watajitahidi kuhakikisha kuwa mahitaji ya vitu mbalimbali vinavyohitajika kwenye hoteli hiyo vinanunuliwa Arusha na vitongoji vyake ili kuweza kuongeza kipato cha wananchi na kujenga mahusiano mema. 
 “Tupo hapa Arusha si kwa mashindano ila kufanya kazi pamoja na wenzetu wenye mahoteli na Tour Operators (mawakala wa utalii) kwa manufaa yetu wote kwa nia ya kuongeza soko la ajira na kukuza uchumi wa Taifa letu” alisema Mariwa.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia