Rais  Donald Kaberuka
BAJETI nyingi za Nchi za Afrika zimekuwa tegemezi kwa kutegemea  wahisani na Nchi kutozikidhi bajeti hizo jambo ambalo linapelekea kutumia rasilimali za Nchi  vibaya kwa maslahi ya wahisani

Pia SERIKALI imetakiwa kutumia Utawala bora wa fedha kwa wananchi wake na matumizi sahihi ya mali Asili kwa manufaa ya vizazi vijavyo na kuitumia demokrasia katika kukuza pato la wananchi wake hapa Nchini

Hayo yamesemwa na Waziri wa Elimu mafunzo ya Amali kutoka (SMZ)Ally Juma Shamuhuna wakati akizungumza na vyombo vya habari jana jijini Arusha kwenye mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika(AfDB)

Alisema kuwa wamekuja kujifunza na leo wamejifunza juu ya suala zima la Demokrasia inavyoweza kukuza uchumi wa Nchi yeyote Sanjari na  utawala bora wa matumizi ya fedha za serikali na kuwa wanaelekea kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2012-13 ambapo watakuwa wamepata uzoefu

Waziri huyo alisema kuwa serikali yeyote itakayo fuata mambo matatu na kuyajali kwa maslahi ya wananchi wake huku akitaja kuwa Utawala bora wa fedha,Matumizi sahihi ya Demokrasia sanjari na Matumizi ya Mali Asili zitaifanya serikali hizo kutokuwa tegemezi kwa wahisani

“Mashirika haya ya fedha ulimwenguni hayatoi fedha bure lazima watangulize maslahi yao hali inayopelekea Nchi zilizofadhiliwa kubaka demokrasia na wananchi wake kuendelea kuwa maskini”alisema Bw.Shamuhuna


About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia