WATAALAMU WA MAWASILIANO NA UCHUKUZI WATAKIWA KUTAFUTA UMBUZI WA TATIZO LA UDUNI WA MIUNDO MBINU
WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe amewata wataalamu
wa fedha,
mawasiliano na uchukuzi kutafuta ufumbuzi wa tatizo la uduni
wa
miundombinu
unaodidimiza uchumi barani Afrika.
Aliyasema hayo
wakati akifungua mkutano wa mwaka wa Taasisi za fedha zinazofadhili maendeleo
barani Afrika
(AADFI), unaoenda sambamba na mkutano wa Magavana wa
Benki ya
Maendeleo Afrika unaofanyika Jijini Arusha , Dk Mwakyembe
alisema mipango
ya maendeleo na kukuza uchumi haiwezi kufanikiwa iwapo
miundombinu
haitaboreshwa kurahisisha usafirishaji.
Alisema hadi sasa
nchi nyingi barani Afrika zinatumia barabara kama
njia kuu ya usafirishaji badala ya reli ambayo licha ya kuwa
na
gharama nafuu lakini pia husafirisha kiwango kikubwa cha
mizigo
kulinganisha na barabara na kuwataka wataalamu hao kutafuta
njia ya
kupata fedha za ndani kugharamia ujenzi na ukarabati wa
miundombinu.
“Kukosekana na kutofanyia matengenezo ya mara kwa mara
barabara zetu
kunakwaza mawasiliano na hivyo kupunguza kasi ya kujiletea
maendeleo
kutokana na ukweli kwamba mawasiliano ndiyo nyenzo muhimu
kiuchumi,”
alisema Dk Mwakyembe
Alisema uduni wa njia za mawasiliano huchangia gharama kubwa
ya
usafirishaji ambayo humwangukia mtumiaji wa mwisho ambaye ni
mwananchi
wa kawaida anayelazimika kununua bidhaa kwa bei ya juu
kulinganisha na
wanaoishi kwenye nchi zilizoendelea kimiundombinu.
Dk Mwakyembe
alisema tatizo la miundombinu ni moja ya changamoto kwa
serikali zote za
Afrika katika juhudi za kukuza uchumi katika sekta
zote ikiwemo
kilimo ambacho ni uti wa mgongo kwa mataifa mengi,
Tanzania ikiwemo.
Alitoa mfano wa
Tanzania kwa kusema asilimia 95 ya mizigo mizito
husafirishwa kwa
njia ya barabara huku asilimia mbili pekee
ikisafirishwa kwa
reli na hivyo taifa kulazimika kutumia fedha nyingi
kujenga na
kukarabati barabara zinazoharibika mapema kutokana na
kuzidiwa na
matumizi.
Awali
akimkaribisha Dk Mwakyembe, Mwenyekiti wa AADFI, Peter Noni
alisema
changamoto kubwa inayozikabili nchi za Kiafrika ni namna na
njia bora za kumudu
kujenga miundombinu za uhakika bila kutegemea
misaada na ufadhili kutoka nchi wahisani na taasisi za fedha
za
kimataifa.
Noni ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya
Rasilimali (TIB),
allisema miongoni mwa mambo yanayotarajiwa kujalidiliwa na
kkutafutiwa
ufumbuzi na namna ya kkutumia taasisi za fedha za ndani
kugharamia
ujenzi wa miundombinu kupitia mikopo yenye masharti nafuu.
0 Comments:
إرسال تعليق
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia