KIDUMU BAND KUPAMBA MISS VYUO VIKUU MKOA WA ARUSHA

Kidum akiwa   


 Msechu


Msanii kutoka nchini Burundi ,Jean Pierre(Kidum) kwakushirikiana na msanii wa nyimbo za kizazi kipya Peter Msechu wanatarajia kuburudisha wananchi wa mkoa wa arusha na vitongoji vyake katika shindano la kumsaka mrembo wa vyuo vikuu vya mkoani hapa shindano linatarajiwa kufanyika June mbili

Akiongea na waandishi wahabari muandaaji wa shindano hilo ambaye ni mkurunzi Fame city decor  Gaudencia Magessa alisema kuwa wasanii hao wanatarajiwa kutumbuiza katika usiku huo wa kumsaka mrembo wa vyuo vikuu wa mkoa wa Arusha shindano ambalo alisema kuwa litafanyika katika ukumbi wa naur ajijijini hapa.

Alibainisha kuwa jumla ya warembo 14 kutoka katika vyuo mbalimbali vilivyopo jijini hapa wanatarajiwa kupanda ukumbini ambapo alisema kuwa warembo hao wametoka katika vyuo mbalimbali ikiwemo chuo cha uhasibu arusha, chuo  kikuu cha makumira,pamoja na vyuo vingine vya jijini hapa.

Aidha alitaja zawadi ambazo zitatolewa kwa washindi kuwa ni mshindi wa kwanza atajinyakulia kitita cha shilingi laki 500000 ,wapili akiondoka na kitita cha shilingi laki 300000 huku mshindi wa tatu akiondoka na kitita cha shilingi 2000000.

Alitaja lengo haswa la mashindano haya ni kumpata mrembo wa mkoa wa arusha ambaye ataenda kuwakilisha vyuo vikuu vya mkoani hapa ambapo alisema kuwa pia wameamua kuandaa mashindano haya wakiwa na nia ya kuweza kusaidia jamii mbalimbali za mkuyani hapa ikiwa ni pamoja na kugawa misaada mbalimbali katika vituo vya kulelea watoto yatima pamoja na wale wanaoishi katika mazingira hatarishi.

"pia sisi tunasaidia watoto yatima wale wasiojiweza na mbali na hapo tunasaidia kulipa ataq kwa watoto ambao wanaitaji kusoma lakini hawana uwezo na huu  ni mwanzo tutaendelea kufanya hivi kila mara"alisema Gaudencia

alitoa wito kwa wananchi wa mkoa wa arusha kujitokeza kwa wingi katika shindano hili kwani shindano hili ni la kwanza na limeboreshwa sana huku akibaiinisha kuwa wameaandaa burudani za aina mbalimbali

Alitaja baadhi ya wathamini waliothamini shindano hilikuwa ni TBL kupitia kinywaji chao cha Reds,Real metal graft,Modern supermarket,Perfect supermarket ,Sg resort,mwandago investment,clouds fm,Trile a fm,Libeneke la kaskazini blog,mount meru pure drinking water pamoja na kasse store

wakati huo huo kituo cha kulelea watoto yatima cha Hope Ophans kimetoa shukurani kwa waandaaji wa shindano hili kwa kuwapelekea msaada wa vyakula

akizungumza wakati akipokea msaada huu lusi juma alisema kuwa wanashukuru kwa kupokea msaada huo kutoka kwa warembo wao kwani unaweza kuwasidia katika kipindi hichi huku akitoa wito kwa wananchi kuendelea kusaidia vituo hivi ambavyo vinalelea watoto yatima pamoja na wale wanaoishi katika mazingira magumu ili watoto hawa nao waweze kujisikia kama watoto wengine kwani watoto wote ni sawa

Akikabidhi msaada huo muaandaaji wa shindano hili gaudencia magessa alisema kuwa wameamua kuwasiadia watoto hawa  ili nao wajisikie kaa watoto wengine

"hii ni njia moja wapo ya kazi zetu katika kipindi cha kufanya onyesho hili na litakuwa endelevu alitaishia hapa kwani sisi tumejipanga  kusaida jamii kwa ujumla"alisema gaudencea

Alitaja baadhi ya misaada walioyopeleka kuwa ni pamoja na mchele,sabuni ,unga wa ugali,mafuta ya kupikia pamoja na maji ya kunywa.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia