WANNE WAUWAWA SOMALIA KWENYE OPERETION


Wakaazi wa mji mmoja wa kusini mwa Somalia wanasema raia wanane waliuwawa katika jaribio lilofanywa na makamando wa Ufaransa kumkomboa mwananchi mwenzao aliyezuwiliwa na wapiganaji.
Ramani ya mji wa Bulo Marer
Walioshuhudia tukio hilo wanasema watu wane walikufa wakati makamando wa Ufaransa walipotua nje ya mji wa Bulo Marer.
Wengine walikufa katika mapambano ya risasi.
Mwanajeshi mmoja wa Ufaransa alikufa Jumamosi kwenye operesheni hiyo na mwengine ametoweka.
Wapiganaji wa Kiislamu wa Al Shabaab ambao walikuwa wanamzuwia askari wa ujasusi wa Ufaransa walisema afisa huyo yuhai, lakini Ufaransa inasema pengine aliuwawa.
CHANZO BBC SWAHILI

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia