Ticker

6/recent/ticker-posts

SEREKALI KIPIGENI TAFU KIWANDA CHA VIKOMBE CHA KIDT KILICHOPO KILIMANJARO


 Wafanyakazi wa kiwanda cha kutengeneza vyombo vya nyumbani wakiwa kazini wilayani Same, Mkoa wa Kilimanjaro. Picha na Zacharia Osanga. 

Kutokana na juhudi za kiwanda hicho, Serikali inapaswa kukipatia ruzuku. Kiwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha vikombe kati ya 1,500 mpaka  2,000 kwa siku.
Kama unatabia ya kupenda kukagua bidhaa kwa lengo la kujua zinatengenezwa wapi, basi ni rahisi kwa kuwa vikombe vingi vinavyotumika kunywea chai, vimetengenezwa China.
Ukifika wilayani Same, Mkoa wa Kilimanjaro utakuta kiwanda cha kutengenezea bidhaa hizo zinazotumika kunywea chai pamoja na matumizi mengine.
Tununue bidhaa zetu
Kiwanda cha Kilimanjaro Industries Development Trust (KIDT) ambacho ni tawi la Kiwanda kikuu kilichopo Moshi kimekuwapo wilayani hapo kwa takribani miaka 30, kikizalisha vikombe, sahani, bakuli, birika, majagi na vifaa vya kuwekea maua.
Bidhaa hizo zinazozalishwa kutokana na malighafi zinazopatikana wilayani humo, wilaya jirani ya Mwanga na malighafi nyingine kutoka Pugu Dar es Salaam.
Msimamizi wa Kiwanda hicho, Loveness Mhina anasema vikombe hivyo vya udongo na bidhaa nyingine wanazotengeneza wanatumia mawe wanayoyatoa eneo la Kavambughu,  nje kidogo ya wilaya hiyo, udongo maalum wanaochimba eneo la Kifula wilayani Mwanga na Kaolini inayopatikana Pugu Dar es Salaam. Mhina anasema kiwanda hicho kwa siku kina uwezo wa kuzalisha vikombe kati ya 1,500 hadi 2,000 kwa siku.
Mbali na kutengeneza vyombo hivyo vya mezani pia kiwanda hicho kinatengeneza vifaa visivyopitisha umeme (insulators), vinavyotumiwa na Shirika la Umeme nchini (Tanesco) ambavyo navyo hutengenezwa kwa malighafi hizo.
Miaka 30 kiwanda kimefanya nini?
Meneja Mkuu wa KIDT, Mhandisi Frank Elisa, anasema kiwanda hicho kilipaoanzishwa mwanzoni mwa miaka ya 1980, hakikuanzishwa kwa lengo la biashara.
“Wajapan ndiyo walioanzisha viwanda hivi na lengo lao lilikuwa kuanzisha viwanda vidovidogo kwa kutumia raslimali zinazopatikana maeneo husika.Kwa mfano,  malighafi za kiwanda hiki, nyingi zinatoka Same,” anasema.
Anasema fursa za biashara zipo nyingi, lakini changamoto kubwa inayowakabili ni mtaji wa kukipanua kiwanda hicho.

Post a Comment

0 Comments