NJOO MTO WA MBU! JESSY RAHA SPORTS BAR &LOUNGE INAKULETEA BURUDANI YA KIPEKEE!”
Mto wa Mbu, Arusha
Wapenzi wa burudani, chakula safi na vinywaji vya aina zote sasa wana nafasi ya kufurahia huduma bora karibu na nyumbani.
Jessy Raha sports bar &Lounge, kiota kipya kilichomilikiwa na Jesca Richard, kimefunguliwa rasmi Mto wa Mbu na kinatoa burudani ya kiwango cha juu kila wiki.
Jesca Richard alisema uwekezaji huu ni sehemu ya kuunga mkono maono ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuvutia utalii wa vyakula.
Wageni kutoka ndani na nje ya nchi wanaweza kuonja chakula safi cha Kiafrika, nyama choma, juisi, shisha na vinywaji mbalimbali huku wakifurahia mazingira mazuri ya Mto wa Mbu.
“Jessy Raha sports bar &Lounge sio tu burudani, bali ni nafasi ya kukutana na marafiki, familia au kufanya mikutano ya kikazi huku ukifurahia chakula bora na mazingira tulivu,” alisema Jesca.
Jesca amewaalika wapenzi wa burudani wote
“Karibuni Jessy Raha sports bar &Lounge Mto wa Mbu, pata burudani ya kila aina na ufurahie kila kipengele tulichokikusanyia!”
Meneja wa kiota hicho, Denis, alisema mbali na burudani na vyakula, wateja wanapata huduma ya super market na barbershop ya kisasa. Kiota hicho pia kimekuwa chanzo cha ajira kwa vijana wa eneo hilo na Jesca anatarajia kutoa nafasi zaidi.



.png)
0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia