Ticker

6/recent/ticker-posts

WAMILIKI 8000 WA MIGODI YA MADINI KUSAJILIWA KWENYE MTANDAO




Na Woinde Shizza,Arusha
Zaidi ya wamiliki 800 wa migod ya madini mbalimbali nchini na wenye leseni za uchimbaji zaidi ya 4000 wameanza kusajiliwa kwenye mtandao  na ofisi ya kanda ya kaskazini ya  madini kuweza kupata idadi yao na kuweza kuendana na teknolojia ya mawasiliano inayokuwa kwa kasi na kuweza kupata takwimu mbalimbali  kuhusu madini yao.


Hayo yameelezwa leo na Kaimu Kamishna msaidizi wa madini wa kanda ya kaskazini Bw,Alex Magayane  wakati wa mahojiano na waandishi wa habari yaliyofanyika katika ofisi za kanda hiyo zilizoko katika halmashauri ya jiji la Arusha ,mkoani Arusha .

Hata hivyo alisema kuwa lengo hasa la kusajili wachimbaji hao wa madini kuweza kuwaingiza kwenye mtandao ambapo kazi zao zitafanyika kwa urahisi kupitia technolojia hii mpya na  kuweza kurahisisha utendaji wakazi yao na wachimbaji na haswa ofisi ya madini ,na  kupata huduma kwa haraka popote pale walipo ili kuwapunguzia  usumbufu ambao awali ilikuwa inamlazimu mchimbaji pindi akihitaji huduma yoyote ya ofisi mpk aende ofisi ya kanda lakini kwa sasa itamsaidia mchimbaji huyo kupata taarifa zote kwenye mtandao kupitia huduma mbalimbali zikiwemo simu za kiganjani ,mitandao ya internet na huduma mbalimbali.

Hata hivyo alisema kuwa kupitia zoezi hilo la usajili  litawasaidia hata kuongeza ufanisi wakazi zao na kumwezesha mchimbaji huyo kuweza kupata takwimu ama taarifa zozote anazohitaji juu ya masuala ya madini na hata bei za madini na bei elekezi za siku hiyo.

Kamishna Bw,Alex  huyo mbali na jitihada mbalimbali za kuboresha huduma kwa wachimbaji hao kuwekuwepo na changamoto kubwa sana hususani upande wawachimbaji hao ambapo wengi wao wamekuwa hawajui namna  ya kutumia mitandao hali  hata kuweza kufungua email ambayo imekuwa ikikwamisha jitihada mbalimbali za kuweza kuboresha huduma hizo za kuwahudumia kwa kupitia mitandao.


Na amewataka wachimbaji hao kuweza kutoa ushirikiano wa kuweza kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuqweza kutambuliwa na ofisi yake na kuweza kuwarahisishia kupata huduma wazitakazo kwa haraka zaidi na kuweza kuongeza tija na ufanisi katika biashara zao za madini.

Hata hivyo amewataka wachimbaji hao kuweza kuhakikisha kila mmiliki wa mgodi anahakikisha anasajiliwa  kwani faida zab usajili nikubwa kulinganisha kuwa nje wa mtandaoa kwani pindi kunapohiaji kuweza kuwapa taarifa wachimbaji hao njia rahisi ya kuwapata kwa pamoja nikwenye mtandao kupitia usajili huo.

Aidha zoei hilo litadumu mpaka mwisho wa mwezi desemba mwaka huu ili kuweza kuhakikisha wachimbaji wote wenye sifa za kupata leseni wameandikishwa na kurahisisha ufanisi na utekelezaji wa kazi zao na kupunguza mlolongo wakuenda katika ofisi za kamnda hiyo ili kuweza kupata huduma.

Post a Comment

0 Comments