KATA YA LOIBORSIRET YAPATA DIWANI
Diwani wa Kata ya
Endiamtu Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara,Lucas Zacharia akipongezwa na Mbunge
wa Jimbo la Simanjiro,Christopher Ole Sendeka baada ya kuchaguliwa kuwa Katibu
Uchumi na Fedha wa CCM Mkoa wa Manyara kwenye uchaguzi uliofanyika mjini Babati.
Diwani wa Kata ya Loiborsiret Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara,Lucas Ole Mukusi amechaguliwa tena kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa mkoa huo kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
Diwani wa Kata ya
Endiamtu Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara,Lucas Zacharia akipongezwa na
Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Manyara,Dorah Mushi baada ya kuchaguliwa kuwa Katibu
Uchumi na Fedha wa CCM Mkoa wa Manyara mjini Babati (katikati) ni Mwenyekiti wa
CCM Kata ya Endiamtu Issa Katuga.
Diwani wa Kata ya Loiborsiret Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara,Lucas Ole Mukusi amechaguliwa tena kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa mkoa huo kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
Akitangaza matokeo
ya uchaguzi huo uliofanyika juzi mjini Babati,Spika wa Baraza la Wawakilishi
Zanzibar,Pandu Amiri Kificho alisema Ole Mukusi alishinda nafasi hiyo kwa
kupata kura 629.
Kificho alisema
wagombea wengine wawili waliopitishwa kugombea nafasi hiyo walijitoa lakini
walipigiwa kura ambapo Godwin Nagol Kapurwa alipata kura 19 na Issa Omary
Katuga alipata kura 18.
Alisema Fratey
Massay alichaguliwa kuwa Katibu wa Siasa na Uenezi wa mkoa huo kwa kupata kura
41 na kuwabwaga wagombea wengine Michael Ngayda Tsaxara aliyepata kura 9 na
Ernest Fiita Sulle alipata kura 2.
Alisema nafasi ya
Katibu Uchumi na Fedha ya mkoa huo ilibidi irudiwe baada ya mshindi kutopata
nusu ya kura kwani Lucas Zacharia alipata kura 26 Gidamon Gapchojiga kura
14,Janes Darabe kura 9 na Gabriel Bukhay kura 3.
Hata hivyo,uchaguzi
huo uliporudiwa Kificho alimtangaza Diwani wa Kata ya Endiamtu,Zacharia kuwa
Katibu Uchumi na Fedha wa mkoa wa Manyara kwa kupata kura 34 dhidi ya
Gapchojiga aliyepata kura 18.
Aliwataja wajumbe wa wilaya wa Halmashauri Kuu
ya CCM wa mkoa huo wa wilaya ya Babati mjini ni Vicky Mushi (389) na Renalda
Ndekubali (383) na wilaya ya Hanang’ ni Daniel Tluway (463) na Samwel Kawanga
(268).
Wilaya ya Babati
Vijijini ni Mariam Kwimba (589) na Raphael Sumaye (273) Kiteto ni Sarah
Losuritia (546) na Ahmed Muya (306) Simanjiro ni Awadhi Omary (360) na Paulo
Sanka (301) na Mbulu ni Joseph Mandoo (353) na Aloyce Baira (169).
Akizungumza baada
ya kuchaguliwa kuwa Katibu Uchumi na Fedha wa mkoa huo Zacharia alisema atawatumikia
wanachama wa mkoa wa Manyara hata usiku wa manane kwani yeye ameomba utumishi
kwao hajaomba ubosi.
Naye,Mwenyekiti wa
CCM wa mkoa huo Ole Mukusi alisema changamoto kubwa atakayopambana nayo kwenye
uongozi wake ni kuhakikisha analirudisha jimbo la Mbulu linaloshikiliwa na
Chadema na kata zinazoshikiliwa na upinzani.


0 Comments:
إرسال تعليق
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia