TAMASHA LA JAMBO FESTIVAL KUANZA KUTIMUA VUMBI OCTOBER 20 JIJINI ARUSHA

mwenyekiti wa idea afrika Augustino Namfua ambao ni waandaaji wa
tamasha kubwa la jambo festival linalotarajiwa kuanza oktoba 20-28 katika
viwanja vya kijenge jijini Arusha akizungumza na waandishi wa habari
kuhusiana na tamasha hilo kulia ni meneja wa mauzo na masoko MEGA TRADE
INVESTMENT Gudluck Kway ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo.
  meneja wa mauzo na masoko MEGA TRADE
INVESTMENT Gudluck Kway ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha hilo

Tamasha la vitu vya asili lijulikanavyo kwa jina la Jambo festival linatarajia kuanza kutimua vumbi oktoba 20-28jijini hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti wa idea afrika Augustino Namfua ambao ni waandaaji wa tamasha kubwa la jambo festival  katika viwanja vya kijenge jijini Arusha alisema kuwa maandalizi yote ya tamasha hilo yamekamilika na zaidi ya wadau 100 wamethibitisha kushiriki  .

Alisema kuwa tamasha hili ni la kwanza kufanyika  jijini hapa na linashirikisha vikundi mbalimbali  vya miziki ya asili pamoja , vyakula vya kiasili na ngoma.

Alisema kuwa   katika tamasha hilo kutakuwa na burudani mbalimbali ambapo siku ya kwanza ambayo ni October 20   mchana kutakuwa na mdahalo wa sanaa na utamaduni ambao utafanyikia via via,huku siku ya pili kukifanyika maonyesha ya sanaa za mikono, siku ya tatu kutakuwa na chakula cha usiku maalumu kwa wasanii wa sanaa za kiutamaduni ,siku ya nne kutakuwa na maonyesho ya vyakula vya kiasili ambapo alisema kuwa kutakuwa na vyakula mbalimbali vya makabila tofauti tofauti  ambapo alisema vitauzwa katika uwanja wa AICC kijenge.

Alisema kuwa lengo kuu la tamasha hili la jambo festival ni pamoja na kuibua vipaji vya sanaa kwa vijana na pamoja na kuwaeleimisha vijana jinsi ya kufanya shughuli za kijasiriamali pamoja na kujikinga na mgonjwa mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa ukimwi.
Alitaja baadhi ya wathamini wa tamasha hili kuwa ni pamoja na megatrade investment kupitia kinywaji chake cha k -vant gin,Coca Cola,Ujumbe Ink,Arusha Hotel,Viavia restaurant,Mwandago investment,sundrise radio,Arusha time,pamoja na Interlegence seccurty.
Kwa upande wa meneja meneja wa mauzo na masoko MEGA TRADE
INVESTMENT Gudluck Kwaya ambao ndio wathamini wakuu wa tamasha hili kupitia kinywaji chao cha Kvant gin alisema kuwa kampuni yao imeamua kuthamini tamasha hili kwakuwa ni tamasha linalodumisha utamaduni wetu pamoja na kuenzi vyakula vyetu asili.

Alisema kuwa hii sio mara ya o ya kwanzakuthamini matamasha bali walishathamini matamasha mbalimbali  na wao kama megatrade watandelea kuthamini pamoja na kusaidi jamii kwa ujumla kama sera yao kampuni yao inavyosema.

Aidha alihaidi kuendelea kushirikiana na jamii katika shughuli mbalimbali za maendeleo na kusema kuwa huu sio mwisho wao wa kuthamini tamasha hili watakuwa wanathamini kila mwaka huku akisisitiza wananchi wa mkoa wa Arusha kujitokeza katika tamasha hilio
Baadhi ya wasanii ambao watatumbuiza katika tamasha hili ni pamoja na kikundi cha kuinua vipaji vya vijana wanaoishi katika mazingira magumu kijulikanacho kwa jina la S.U.A.





About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia