Ticker

6/recent/ticker-posts

JE WAWEZA KUJUA KIPAJI CHAKO


Leo nitazungumzia hatua na mbinu za kutambua kipaji. Kabla ya kuzama kwenye somo lenyewe, hebu turejee kwanza kwenye fasili na ufafanuzi wa neno kipaji:
Kipaji ni umahiri wa kipekee alioweka Mungu ndani ya akili ya mtu unaoongoza usadifu wa viungo na fikra zake kufanya jambo fulani kwa upekee kabisa.
Ni uwezo wa kipekee wa kuzaliwa nao uliojengeka kwa binadamu unaompa nguvu mtu kufikiri kiutofauti au kufanya jambo kwa umahiri mkubwa. Ni umaizi ndani ya michepuo ya akili ya mtu inayomuongoza kufanya kitu au kufikiri kwa tija na upekee. Ni talanta ambazo mtu anazaliwa nazo pasina kusomea. Elimu inasaidia tu kupalilia na kukuza vipaji vya mtu ili avitumie kwa mafanikio makubwa.
Vipaji vinajidhihirisha kwenye umaizi wa kiakili, kufikiri, kubuni, kuvumbua, kusanifu au vinaweza kuwa kwenye utumiaji wa viungo vya mwili kama kucheza, ufundi, usanii wa fani mbalimbali na mifumo wa kijamii na uwezo wa mwili kutenda. Kipaji ni tunu toka kwa Mungu. Haijalishi unakitumia au hukitumii kitabaki kuwa ni chako daima.
Nilisema wiki iliyopita kuwa kosa kubwa tunalofanya watu wengi ni kuishi kwa kuiga maisha ya watu wengine kana kwamba wewe ni nakala (fotokopi) ya wengine. Nilisisitiza pia kuwa watu mashuhuri na waliofanikiwa ni wale waliogundua na kutumia kikamilifu vipaji vyao.
Wasani na wanamichezo wengi ni miongoni mwa watu maarufu na matajiri duniani japokuwa wengi hawana elimu kubwa kiasi cha kushangaza, walichofanya ni kutumia vipaji na vipawa vyao kikamilifu.
Sasa basi tunajuaje kama mtu una kipaji fulani? Haya ndiyo mambo yanaweza kumsaidia binadamu kutambua kipaji alichonacho:
Moja, uwe na shauku na jitihada ya kujaribu kufanya vitu vingi pasipo kuchoka. Nilisema wiki mbili zilizopita kuwa kipaji ni kama sukari iliyowekwa kwenye chai pasipo kukorogwa. Lakini ikikorogwa ladha ya chai utaisikia.
Vivyo hivyo, tunahitaji kujaribu kufanya mambo mengi tangu tukiwa watoto hadi ukubwani bila kuchoka. Watoto wana jitihada kubwa za kujaribu mambo mengi. Hapo ndipo huanza mchakato wa kuvumbua vipaji vyao.
Mara nyingi wazazi huanza kubashiri vipaji vyao kwa kuangalia jitihada za watoto kujaribu na kufanya vitu kwa umahiri na upekee. Ukiwa na kipaji cha kuimba lakini haujawahi kujaribu kuimba huwezi kujua kama una kipaji hicho.
Ukiwa na kipaji cha kucheza mpira lakini hujawahi kucheza mpira huwezi kujua kama una kipaji hicho

Post a Comment

0 Comments