WANAFUNZI 160 AMAN KARUME WILAYANI KONDOA WAANDAMANA HADI KWA MKUU WA WILAYA

Na Woinde Shizza, Kondoa
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Amani Abeid Karume ilyopo kata ya Pahi wilayani Kondoa wameandamana hadi ofisini kwa mkuu wa wilaya hiyo Sezaria Makota wakidai kupewa Adhabu za kuchimba visiki, na vibarua vya kushusha mizigo ya ujenzi wa shule jambo ambalo linawakatisha masomo yao.
Hayo yamebainika wakati mkuu huyo wa wilaya akiongea na wanafunzi hao kwenye ukumbi wa Kondoa Irangi na kutoa Agizo la wanafunzi hao kurejea shuleni wakati malalamiko yao yakiendelea kutatuliwa na mwisho wake ni jumamosi ya wiki hii yote yatakuwa yameshughulikiwa.
Amesema kuwa malalamiko waliowasilisha ofisini kwake na viongozi wa wanafunzi hao ni pamoja na kukosa huduma sahihi za afya ikiwemo kutokuwepo kwa dawa kwenye kituo cha Afya Pahi na kadi za CHF za wanafunzi wengine kutofanya kazi,pia kupewa Adhabu ya kuchimba visiki wakati wa masomo.
Mkuu huyo wa wilaya Amebainisha kuwa uonevu kwa wanafunzi hao ni marufuku ambapo akawataka Afisa elimu kuhakikisha kunakuwepo na Box la maoni shuleni hapo sanjari na kuchukuwa hatua za kinidhamu kwa wale wote watakaokaidi Agizo hilo.
“Nawataka watoto wangu kubwa ni nidhamu ila mwende shule wakose sababu na mbadilike kwani watawatafutia sababu ila malalamiko yenu mpaka jumamosi mabadiliko mtayaona na tunaendelea kuyafuatilia kwa ukaribu nami ntafika shuleni hapo wakati wowote wiki hii” alisema dc
Miongoni mwa malalamiko ya wanafunzi hao ni matibabu hafifi,kadi za CHF hazifanyikazi,kupewa adhabu za kuchimba visiki wakati wa masomo, kulipia Nembo ya shule hadi sasa hawajapewa, makamu wa mkuu wa shule kumpiga mwanafunzi teke na michango iliyopitiliza ikiwemo kutakiwa kulipia rimu 8 kwa ajili ya majaribio na mitihani.
Amesma kuwawaraka wao ameoupokea na atahakikisha anaufanyiakazi haraka iwezekanavyo na kumuagiza mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kondoa Vijijini kuhakikisha wanafunzi wote waliofika ofisini kwake na wale 7 walioshindwa kufika ofisini kwake wanafika salama shuleni na wasibugudhiwe na waendelee na masomo yao.
DC Makota amewataka waalimu wote ambao hawaingii Darasani kuingia mara moja kufundisha,huku akisema kuwa wanafunzi hao ni marufuku kufanya vibarua vya kubeba mizigo ya ujenzi wa majengo na kumtaka pia mkurugenzi kuhakikisha wanafunzi saba waliobakia njia kama wapo salama

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia