SERIKALI YAPIGA MARUFUKU MAKAMPUNI YANAYOTUMIA KIGEZO CHA FURSA KUWAKANDAMIZA VIJANA

 


Wilaya ya Arumeru imepiga marufuku makampuni na watu binafsi wanaotumia kigezo cha fursa kuwatapeli na kuwakandamiza vijana kuacha mara moja


Akizungumza wakati wa maadhimisho  ya kilele cha siku ya Vijana duniani yaliyofanyika katika  Halmashauri ya Wilaya ya Meru, mwakilishi wa Mkuu wa ya Arumeru Mwl.Marcus Nazi ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Elimu ya Awali na Msingi wa halmashauri hiyo ametoa wito kwa vijana kuitumia vema fursa  mbalimbali kujikwamua kiuchumi ikiwemo fursa ya mikopo  isiyo na riba inayotolewa na halmashauri .


Mwl.Nazi alisema serikali  imeweka mikakati kupitia sera mbalimbali za kuwaletea vijana maendeleo kwa kuzingatia kundi la vijana ni kundi kubwa kwani  tafiti zinaonyesha kuwa asilimia 65% ya waishio bara  ni vijana ambapo ametoa wito kwa wadau kuungana na serikali  kuwasaidia vijana na si kuwakwamisha kwani Serikali wilayani humo haitosita kuwachukulia hatua makampuni au watu binafsi wanaowakandamiza vijana kwa kigezo cha fursa .


Elisante Nnko ambaye ni miongoni mwa vijana walioshiriki maadhimisho hayo ametoa wito kwa vijana kufuata  imani waliojengewa kwenye jamii na serikali kwa kuchapa kazi kwa weledi na bidii.


Maadhimisho hayo ya siku ya vijana yaliyofanyika katika viwanja vya MS TCDC yamewezeshwa na Halmashauri ya Wilaya ya Meru kwa kushirikiana na wadau wa Mashirika ya   SOS  CHILIDREN'S VILLAGES, VOICE OF YOUTH  TANZANIA, DUSAFO, SAVE AFRICA TANZANIA ,TAMIHA,KAMBELE


Ikumbukwe kila  mwezi Agosti  Dunia huadhimisha siku ya Vijana,ikiwa lengo ni kukumbuka mchango wa vijana katika kukuza maendeleo  huku  kaulimbiu ya mwaka ikisema  "Kuelekea 2030: Tanzania ya viwanda,boresha elimu  Kwa vijana,kwa maendeleo ya Taifa".

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia