Ticker

6/recent/ticker-posts

WAOMBA KATIBA MPYA ILI KUBADILISHA MFUMO ULIOPO

 



Na Rose Jackson ,Arusha 

Wakazi wa loliondo na ngorongoro wamesema kuwa tiba pekee ambayo itawasaidia wafugaji wa maeneo hayo ni upatikanaji  wa katiba mpya ili iweze kubadilisha mfumo uliopo.


Wameyasema hayo katika kumbukizi ya mwaka mmoja ya mateso waliyopitia wananchi wa loliondo na ngorongoro ambapo wamesema kuwa namna pekee ya kuondokana na adha wanayopitia wafugaji ni upatikanaji wa katiba mpya.

baadhi ya wananchi hao akiwemo diwani wa kata ya Nainokanoka edwadr maura na mwenyekiti  wa  viongozi wa mila  ngorongoro anaeleza kuhusiana na umuhimu wa  upatikanaji wa katiba mpya kwa wafugaji hao

"Wafugaji nchini tunapitia wakati mgumu sana haswa loliondo maa baada ya ardhi yetu kuchukulikuwa na hii hali sisi inatuathiri sana  ila kitu ambacho kitatusaidia ni katiba mpya kwani itatusaidia kuainisha ardhi yetu ambayo inatufanya tukose maeneo ya kulishia mifugo."alisema Maura

Aliongeza kuwa licha ya  serikali kuwawekea wananchi wa loliondo na ngorongoro kikwazo lakini kamwe hawataweza kuhamia Msomera mkoani Tanga.


Nae  diwani wa viti maalum tarafa ya sale kjooli kakei ameishauri serikali kuwaona wananchi wa loliondo ni wananchi na ni wahifadhi hivyo ni vema ikasitisha unyanyasaji uliopo kwani kuna huduma za afya zimesitoshwa  na hivyo kulazimika kutembea umbali mrefu.

 "Kwa sasa kuna huduma ambazo serikali imesitisha kwenye tarafa zote na hii inatupa changamoto hivyo mie naona serikali tukae kwa pamoja tuzungumze ili tupate muafaka kwani sisi hatuna mpango wa kwenda msomera "aliongeza diwani.

Wakazi hao wamesema kuwa  wanakabiliwa na changamoto lukuki mara baada ya serikali kusitisha baadhi ya huduma muhimu huku watoto wa kiume nao wakiwa wanakimbilia nchini kenya kutafuta maisha na hivyo kuiomba serikali kuangalia swala hilo kwa jicho la pili.

Post a Comment

0 Comments