Na Woinde Shizza , Arusha
NAIBU Waziri Mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania na Waziri wa nishati,Dkt Dotto Biteko ameielekeza Wizara ya Maliasili.na utalii kutumia fursa za ukuaji wa sekta ya TEHAMA katika utangazaji utalii na upatikanaji wa masoko ya utalii kwa ushirikiana na mamlaka mbalimbali za Serikali katika kuboresha mazingira ya biashara za utalii nchini ili kuchochea na kuvutia uwekezaji zaidi.
Ameyasema hayo jijini Arusha wakati akifungua onesho la utalii la kimataifa la Karibu -Kilifair 2025 linalofanyika kuanzia juni 6 hadi 8 katika viwanja vya magereza vilivyopo jijini Arusha .
Dkt.Biteko ambaye aliwamwakilisha Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ,Dkt .Samia Suluhu Hassan amewataka pia
Kuendelea kubuni njia mbalimbali za uendelezaji wa mazao ya utalii nchini kwa kuzingatia mgawanyiko wa aina ya mazao na mtawanyiko wa kijiografia wa nchi yetu.
Aidha ametoa rai pia kwa Sekta Binafsi kuendelea kuwekeza katika sekta ya utalii, hususan katika eneo la huduma za malazi, ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya soko hasa tukizingatia uwepo wa matukio mbalimbali ya kimataifa yatakayofanyika nchini kadhalika na mwitikio chanya wa watalii kutoka katika masoko yetu ya kimkakati na yale yanayokua kwa kasi Duniani.
“Napenda Niwahakikishie kwamba,Serikali itaendelea kushirikiana nanyi wadau katika nyanja mbalimbali kuhakikisha ustawi wa biashara za utalii nchini na maendeleo ya sekta kwa ujumla wake.”amesema Dkt.Biteko.
Ameongeza kuwa,Kauli Mbiu ya Onesho la KARIBU-KILIFAIR kwa mwaka 2025 ni “Utalii Endelevu, Kujenga Ustahimilivu na Ubunifu” hususan katika kipindi hiki ambacho sekta ya utalii imerejea katika hali yake ya ustawi baada ya kutokea kwa changamoto ya UVIKO-19, kauli mbiu hii imeakisi malengo yetu ya kisera katika kukuza utalii endelevu yaani Sustainable tourism, kama ambavyo imekuwa ikitiliwa mkazo na Shirika la Utalii Duniani (UN-Tourism).
Amesema kuwa, kauli.mbiu hiyo inaenda sambamba na azma yetu ya kukuza na kuendeleza sekta ya utalii nchini kwa kuimarisha ubunifu katika kutangaza vivutio na kutanua wigo wa mazao ya utalii, kusimamia matumizi endelevu ya rasimilmali za utalii, na kujenga uchumi jumuishi kwa jamii zetu na Taifa.
Amefafanua kuwa, onesho la KARIBU-KILIFAIR linaendelea kukua Kimataifa na kuvutia idadi kubwa ya washiriki, ambapo huwakutanisha wadau wa utalii kwa ajili ya kuwaunganisha kibiashara, kubadilishana uzoefu katika biashara za utalii na masoko ikiwemo pia, kuhamasisha uwekezaji kwenye sekta hii muhimu ya kiuchumi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa masoko na biashara kutoka kampuni ya RSA Harveer Bhamra ,akizungumza mbele ya Dkt Biteko alipotembelea banda lao amesema kuwa, wana kiwanda kipo Moshi walikuwa na mashine lakini sasa hivi wameagiza mashine nyingine kwa ajili ya kufanyia kazi zao kwani wamechukua tender katika nchi ya Uganda,Kenya ,Malawi ,Angola na Congo .
Amesema kuwa,wanatengeneza magari Afrika nzima sio lazima Tanzania yenyewe na wanapeleka katika nchi mbalimbali ikiwemo ,Malawi , Congo na Dubai kwani wana mkataba nao katika kufanya kazi .
“Nakushuru sana Mhe kwa kutembelea banda letu na kuweza kujionea shughuli mbalimbali tunazozifanya kwani tumekuwa tukifanya kazi nzuri sana na tuna masoko ndani na nje ya nchi kwani wateja wetu wanatuamini kutokana na huduma nzuri tunazotoa “amesema Bhamra.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia