Ticker

6/recent/ticker-posts

JIJI LA ARUSHA LAKABILIWA NA CHANGAMOTO YA UGONJWA WA U.T.I

 

 Na Woinde Shizza wa Libeneke la kaskazini blog
Jiji la Arusha bado linakabiliwa na changamoto ua ugonjwa ambao unaambukizwa kwa njia ya mkojo(U.T.I) ambao unakuwa siku hadi siku ambapo takwimu za mwaka 2014 zinaonyesha kuwa takribani wagonjwa 32085 walikutwa na ugonjwa huo hali ambayo inakwamisha jitihada za kujiletea maendeleo kutokana na ugonjwa huo.

Ambapo alisema kuwa hadi hivi sasa hawajagundua tatizo na chnanzo halisi cha ugonjwa huo ambao unakuwa kwa kasi sana katika jiji hili la arusha hali mabayo inakwamisha jitihada za kupambana na adui maradhi kwa wananchi wake.

Hayo yameelezwa jana  na kaimu mganga mkuu wa jiji la Arusha Sr,Jane Balalukululiza wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake na kuweza kuelezea ugonjwa huo amabo umekuwa ni tatizo lajiji  kwa wananchi wake,mahojiano hayo yaklifanyika ofisini kwake katika jiji hili mkoa wa Arusha.

Hata hivyo alisema kuwa rika linaloongoza kwa ugonjwa huo nikuanzia miaka mitano kuendelea hadi watu wazima ambapo hadi sasa hawajagundua chanzo hasa cha ongezeko hilo la ugonjwa wa u.t.i .

Aliongeza kuwa ingawa kuna viashiria vya sababu vya ugonjwa huo kuwa ni kutoweka mazingira safi ya vyoo ,mazingira opia ya kujiassaidiua haja ndogo mahali amabpo si salama kwa afya ya mtumiaji eneo hilo hali ambayo inapelekea kupata kwa ugonjwa huo.

 Sr,Jane aliongeza kuwa bado pia kuna changamotio ya kujitokeza kwa wananchi kupima afya zao ili kuweza kujua kama afya ninzuri ama imepeta maambukizi yoyote ya magonjwa mbalimbali ili kuweza kucukua tahadhari na kuweza kupata matibabu ya ugonjwa husika.

Mbali na jitihada za jiji hilo kuweza kupambana na adui maradhi wameunda mkakati wa kutumia kikosi kazi cha kuweza kukagua mazingira ya wananchi wake kuangalia namna ya kuweka mazingira safi ili kuweza kuepuka kupata maradhi na kuweka sheria ndogondogo endapo mtu atakiuka basi apelekwe kwenye vyombo vya sheria ili kuweza kudhibiti wananchi wakaidi wa taratibu za kuishi na nchi.

Ameitaka jamii kwa ujumla kuweza kuwa na taratibu ya kupima afya zao kwani hivi sasa ugonjwa huo umekuwa ni kikwazo cha utekelezaji wa majukumu yao.

Kwa upande wake mwakilishi wa wananchi Bi,Emiliani Msuya aliiomba Serikali kuweza kutenga fungu la kuweza kuwapa elimu wananchi wake ili kuweza kuwafundisha namana ya urtunzaji mazingira ili kuweza kuepuka kupata ugonjwa wa maambukizi ya njia ya mkojo ili kuweza kunausuru kurudisha nyuma jitihada za kujiletea maendeleo kupitia famili na wananchi wake.

Aliongeza kuwa  wananchi wanatakiwa kuiunda vikundi vidogovidogo ili kuweza kusimsmiana katika kutunza mazingira na si kusubiri pindi Serikal;i mpaka ianze kampeni ya upimaji na kuweza kuhamasisha wananchi kupima afya zao.

Post a Comment

0 Comments