ABIRIA WATESEKA USAFIRI ARUSHA

Wananchi wa mkoani Arusha leo wamepata tabu sana ya kusafiri kutokana na mabasi yaliyokuwa yanafanya safari zake za kwenda  mkoani Kilimanjaro kugoma kutokana na madai kuwa ushuru wa standi kupanda
 
Libeneke la kaskazini   lilishughudia wananchi hao ambao wengi wao walikuwa wanaelekea katika sehemu zao za kazi huko mkoani Kilimanjaro wakipata shida ya kupata mabasi huku wengine wakilazimika kulipa  nauli  kubwa ili mradi tu wafike wanapoenda.
 
Wakiongea kwa nyakati tofauti abiria hao walikuwepo standi hapo ambapo mmoja wapo alijitaja kwa jina la Msafiri jamali yeye alisema kuwa kugoma huko kwa mabasi kumewaletea matatizo makubwa kwani wengine walikuwa wanaenda mkoani Kilimanjaro katika kazi huku akisema kuwa mbali na mabasi ya fanyayosafari ya moshi kugoma (kosta) pia magari makubwa ambayo yanapita katika mji huo yamekuwa yakitaka nauli sawa na mtu ambaye anaenda dar.
 
“mbali na magari kukosekana lakini pia kuna magari yanayoenda dar yanapita apo hapo moshi lakini yanataka ukipanda basi hilo basi ulipe nauli kabisa ya dar kama ni 250000 ulipe ili wakufikishe moshi kitu ambacho wanatuumiza sana sisi wasafiri jamani”alisema Elifuraha kileo.
 
Kutokana na matatizo hayo libeneke lilibisha hodi  kwa  kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Arusha Arson Mwakyoma  azunguzie swala hilo naye alisema kuwa ni kwali swala hilo lipo ila wapo katika mazungumzo na mdua sio mrefu watatoa jibu sahihi .
 
Alisema kuwa yeye anaamini kuwa magari ya mkoani Arusha hayajagoma bali yanaogopa kwenda mkoani Kilimanjaro na abiria kwani wakienda wanaweza kufanyiwa fujo na  wenzao wa mkoani huko waliogoma .
 
Alibainisha kuwa tatizo hili lipo na linasemekana ni kutokana na halimashauri ya manispaa ya mkoa wa Kilimanjaro kupandisha  bei za kulipia ushuru wa mabasi standi pasipo ya kuwashirikiksha wamiliki wa mabasi ,pamoja na madereva na makondakta.
 
Alisema kuwa anasikitishwa sana na watu hao ambao wanawazuia wenzao na wao kama jeshi la polisi wameamua kuwachukulia hatua kali wale wote ambao watabainika wanawaletea fujo madereva ambao watakuwa wanawasafirisha abiria .
 
Kwakweli ni kitu kinachosikitisha kuona mtu ambaye analipa ushuru anagoma kubeba abiria kwakweli inasikitisha na wewe mwenyegari kumbuka unavyoweka gari yako pasipo kubeba watu basi unajikomoa mwenyewe maaana kama ni ushuru upo pale pale na utaulipa tu hivyo kama kunatatizo ni bora magari yafanye kazi huku mazungumzo yakiendelea kuliko kugoma na kuwatesa wananchi
 
“mimi naona cha muhimu ni kukaa mezani na kutafuta suluhu kuliko kufanya haya mambo ambayo wanayafanya kwakweli “alisema Mwakyoma
 
|Naye katibu mkuu wa chama cha usafirishaji (Hakiboa) Lokeni Adofu alisema kuwa kweli mgomo upo mkoani Kilimanjaro  na kwa mkoa wa Arusha walishindwa kwenda kutokana na fujo ambazo zilikuwa zinafanywa huko ila alibainisha kuwa mazungumzo yanaendelea na madereva wote wanatakiwa kuingia kazini hadi pale mazungumzo yatakamilika
 
“mimi nasema kweli mwenyekiti wetu wa  haki boa ameketi na kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro mazungumzo yanaendelea ili kupata suluhu ,lakini wakati amazungumzo  yanaendealea sisi kama haki boa tumewaamuru madereva wote mkoani Arusha waingie standi wavae sare dereva na kondakta wake wabebe abiria wawapeleke  mkoani Kilimanjaro kama kawaida na napenda kuwahakikishia usalama wao utakuwa vizuri kwani kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro ameshaweka ulinzi wa kutosha  na tutaendelea kulipa ushuru shilingi 1000 mpaka muafaka upatikane“alisema Adofu
 
Alisema kuwa lengo kuu la woa kugoma ni kutokana na kupandishiwa bei ya ushuru  kutoka shilingi 1000 hadi 2000 kw akila kituo pasipo kuuitwa na kukaa chini na kuongelea swala hilo wao kama wamiliki

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia