WANANCHI WA KIJIJI CHA KWAITITO WALIA UKAME MBELE YA DC WA HAI
mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga akiwa anaandika matatizo ambayo yalikuwa yanasemwa na wananchi
![]() |
| wananchi wakiwa wanamsikiliza mkuu wa wilaya kwa makini |
Wananchi wakiwa wanamsikiliza mkuu wa wilaya kwa makini
Wananchi
wa kijiji cha Kwatito wameeiomba serikali kuwapelekea chakula kutokana
na ukame unaowakabili unaotokana na kukosa kwa mvua kwa misimu mitatu
mfululizo.
Wananchi hao wametoa kilio hicho kwa mkuu wa wilaya ya Hai Mhe. Novatus Makunga katika mkutano wake wa hadhara na wananchi wa kijiji hicho hicho.
Aidha wameiomba serikali kudhibiti uingiaji wa makundi ya mifugo katika maeneo hayo kwa lengo la kutafuata mabua ya mahindi yaliyonyauka kutokana na ukosefu wa mvua.
kwa upande wake mkuu huyo wa wilaya Mhe Makunga ameeleza kuwa tayari tathimini ya mahitaji ya chakula imeshakamilika na imetumwa katika ngazi husika.
Aidha aliwataka wananchi hao kuwa tayari kubadilika na kuingia katika kilimo cha mazao yanayostahimili ukame ambapo wilaya itaingia mkakati huo katika msimu ujao wa kilimo kikiwemo kilimo cha Mtama
Wananchi hao wametoa kilio hicho kwa mkuu wa wilaya ya Hai Mhe. Novatus Makunga katika mkutano wake wa hadhara na wananchi wa kijiji hicho hicho.
Aidha wameiomba serikali kudhibiti uingiaji wa makundi ya mifugo katika maeneo hayo kwa lengo la kutafuata mabua ya mahindi yaliyonyauka kutokana na ukosefu wa mvua.
kwa upande wake mkuu huyo wa wilaya Mhe Makunga ameeleza kuwa tayari tathimini ya mahitaji ya chakula imeshakamilika na imetumwa katika ngazi husika.
Aidha aliwataka wananchi hao kuwa tayari kubadilika na kuingia katika kilimo cha mazao yanayostahimili ukame ambapo wilaya itaingia mkakati huo katika msimu ujao wa kilimo kikiwemo kilimo cha Mtama



0 Comments:
إرسال تعليق
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia