TATIZO LA MAJI LIPO KILA SEHEMU NCHI HII
Mikokoteni ikiwa inapakiwa maji kwenye mji wa Magugu Wilayani Babati
vijijini Tatizo la maji kwenye mji huu ni kubwa hali inayofanya ndoo
moja kuuzwa kwa shilingi 300 (MAWASA)MPO .
Usafiri wa shida jamani eeh
Wanyama kazi wakiwa wanavuta mkokoteni kwenye kijiji cha minjingu
wilayani Babati Vijijini kama walivyokutwa na kamera yetu hapa wakiwa
wamefikisha maji ambayo ni adimu kijijini hapa.
Ubomoji wa nyumba za kituo cha mikutano cha kimataifa(AICC)Kupisha ujenzi wa kituo cha kibiashara ukiwa umekamilika hapa baadhi ya wabomoaji wakiwa na wananchi wakiokota masalia ya nongo na matofali kwenda kujipatia chochote kama walivyokutwa na kamera yetu maeneo ya Soweto jijini Arusha
Jiji la Arusha katika muonekano wa kisasa na kuwa jiji la mfano hapa nchini kama linavyoonekana hii ni kituo cha kibiashara cha NSSF kwenye Round About ya Florida kikiwa katika hatua za mwisho za ujenzi kama kamera yetu ilivyokuta mafundi wakiweka vioo.
0 Comments:
إرسال تعليق
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia