WANANCHI WA BABATI VIJIJINI WALALAMIKIA SEREKALI
| Mwananchi akichangia jambo |
Mwenyekiti wa kijiji cha Magugu Omary Mazinde akiwa kwenye mkutano mkuu
wa kawaida wa kijiji hicho nyuma yake mwenye gauni la zambarau ni diwani
wa kata ya Magugu Rehema Oamari wakifuatilia mkutano huo wilayani Babati vijijini
Malalamiko hayo wameyatoa wakati LIBENEKE LA KASKAZINI lilipotembelea
kijijni hapo kutaka kujua wameipokeaje Amri ya mh.Dc Khalidi Mandia aliyoitoa
ya kuendelea kuyafunga maziwa hayo wakati sheria ya uvuvi wilayani humo
inawataka kwa sasa kuendelea na uvuvi kwani maziwa hayo hufungwa kuanzi dec30
hadi july1.
Walisema kuwa huko ni kushindwa kwa idara ya uvuvi
kulishughulikia suala la uvuvi haramu kwenye kipindi cha kuachia samaki kuzaana
na kuwa wao wanaingia kwenye mtego wa panya bila sababu yeyote.
Moja wa wakazi wa kijiji hicho Matei Laizer alisema kuwa
anachojua yeye kuwa uongozi wa kijiji na halmashauri imeshindwa kuweka
ushirikiano kwa wananchi kwenye ulinzi shirikishi na kuwa wao wamekuwa mbuzi wa
kafara kwa wavuvi haramu ambao wanavua mchana kweupe bila ya uongozi wa kijiji
kuwachukulia hatua unadhani viongozi wa kijiji hawawajui wanaovua wapo na
wengine wanaishi majumbani mwao na wanawapoke bila ya kificho.
Laizer akawataka sheria ifuate mkondo wake kwa viongozi na
wananchi watakaobainika kuchukuliwa hatua kali niabu kwa serekali kutoa amri ya
kuzivunja sheria kwa kuwachia wachache kufaidi rasilimali zetu kwa manufaa ya
wachache na kumtaka Dc kutokukurupuka kutoa amri kama hizo na badala yake
kuangalia tatizo lipo wapi kuwaumiza wanaolitegemea ziwa hili kuendesha maisha
yao.
Mmoja wa wavuvi katika ziwa hilo Huseini Juma alisema kuwa kwasasa
familia yake inazidi kupata tabu kwa miezi mingine kwa uzembe wa wachache
kutotii sheria na serekali kushindwa kuwafuatilia huku ni kuumiza wengi kwa
faida ya wachache.
Sakata hilo limetokana na kauli yam h.dc aliyoitoa kwenye
kikao cha baraza la madiwani wa mji wa babati mwishoni mwa mwezi uliopita
akisema kuwa imetokana na kikao cha wakuu wa mikoa katika kikao cha ujirani
mwema kuangalia athari za mazalia ya samaki na utumiaji wa kokoro katika uvuvi
hali iliyopoelekea samaki katika maziwa hayo kupungua kwa kasi na kuhatarisha
uwepo wao.
Uvuvi haramu umekuwa ni changamoto kubwa kwa idara za uvuvi
kwenye mikoa ya Kilimanjaro,na manyara kwani idara za uvuvi zimekuwa na
changamoto mbali mbali ikiwemo vitendea kazi vya kisasa ikiwemo boti Mafuta,na
fedha za kujikimu kwani uvuvi umekuwa ukifanyika kwa kuvizia badala ya doria
endelevu na baadhi ya halmashauri kuwatupia lawama wananchi kushindwa kutoa
taarifa kwa wakati
0 Comments:
إرسال تعليق
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia