KONGAMANO LA KWANZA UTALII NCHI ZA AFRIKA KUFANYIKA ARUSHA

naibu waziri wa utalii Lazaro Nyalandu akiwa anaongea na waandishi wa habari kuhusiana na kongamano la utalii linalianza kesho katika jumba la mikutano la AICC jijini hapa
Waandishi wa habari wa mkoa wa arusha wakiwa wanfanya kazi yao katika mkutano wao na naibu waziri

Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Mohamed Gharib Bilal anatarajiwa Kufungua Kongamano la Kwanza Afrika kuhusu usimamizi wa Utalii Endelevu katika Hifadhi za Taifa.

Akizungumza na vyombo vya habari Naibu Waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu alisema kuwa Kongamano hilo linatarajiwa kuanza rasmi October 15-18 katika ukumbi wa kimataifa wa Mikutano wa (AICC) uliopo jijini Arusha.

Bw. Nyalandu alisema kuwa kongamano hilo lina lengo la Kubadilishana uzoefu kuhusu fursa, changamoto, zilizopo katika uhifadhi katika kukuza uchumi.

Alisema kuwa Tanzania ina vivutio vingi vya utalii kama mapori ya akiba,hifadhi za taifa ngorongoro na hifadhi za asili za misitu, pia vivutio vya asili na kiutamaduni kama michoro ya mapangoni iliyopo Kondoa Irangi,eneo la kihistori la olduvai na nyayo za kale za laytoli  zilizopo ngorongoro.

Aidha alisema kuwa sekta ya utalii inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa vitanda ambapo alisema kuwa kwa ujumla swala hilo ni changamoto kubwa ambapo serikali imejipanga kukabiliana nalo ili kuhakikisha kuwa sekta ya utalii inakuwa na kuongeza pato la taifa.

“Serikali inafanya kila ambalo linawezekana ili kuweza ili tuweze kuhakikisha kuwa vitanda vinatosha pamoja na miundo mbinu kuwa bora zaidi ili viweze kutosha wageni ikiwa ni pamoja na kuwafikisha kwa urais zaidi.”alisema bw.Nyaladu

Pia alifafanua kuwa jumla ya washiriki 412 wanategemewa kushiriki kutokanchi 40 za  bara la afrika wakiwemo mawaziri kumi na tatu ambapo amesema kuwa washiriki 242 ambapo ni sawa na asilimia 59% watakuwa ni watanzania na asilimia 41%  ni wageni kutoka nchi mbalimbali za bara la afrika.

Alisema kuwa Kongamano hilo limeandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa lenye makao makuu yake nchini Hispania kwa kushirikiana na Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia