HATI YA KUKAMATWA MKE WA GBAGBO YAFUNGULIWA,WANAMGAMBO WA DRC KUPATA HUKUMU SIKU TOFAUTI

Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) imeamua kuachia huru hati ya kukamatwa kwa mke wa aliyekuwa Rais wa Ivory Coast, Simone Gbagbo huku mahakama hiyo pia ikitanganza kwamba itatoa hukumu siku mbili tofauti katika kesi zinazowakabili wanamgambo wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
ICC 
Hati ya kukamatwa mke wa Gbagbo yafunguliwa: Majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) Alhamisi waliamua kuifungua hati ya kukamatwa mke wa Rais wa zamani wa Ivory Coast, Simone Gbagbo anayekabiliwa na mashitaka ya uhalifu dhidi ya binadamu. Hati hiyo ya kukamatwa kwa mwanamke huyo ambayo awali ilitolewa Februari 29, mwaka huu, inadai kuwa mwanamke huyo anahusika kwa mashitaka ya uhalifu dhidi ya binadamu ikiwa ni pamoja na mauaji, ubakaji na aina nyingine za unyanyasaji wa kijinsia ilifanywa kati ya Desemba 16, 2010 na Aprili 12, 2012. Ghasia hizo zimekuja kufuatia mume wake, Laurent Gbagbo na Rais wa sasa wa nchi hiyo Allasane Ouattara kila mmoja kujitangaza kuwa Rais baada ya uchaguzi mkuu wa nchi hiyo. Wakati Gbagbo mwenyewe hivi sasa anashikiliwa jela ICC akiwa anakabiliwa pia na mashitaka ya uhalifu dhidi ya binadamu, mkewe, Simone anashikiliwa kizuizini, Kaskazini mwa Ivory Coast na watawala wapya wa nchi hiyo.
Viongozi wa wanamgambo wa zamani DRC kuhukumiwa siku tofauti: Mahakama ya Kimataiafa ya Makosa ya Jinai (ICC) Jumatano iliamua kutoa hukumu katika kesi inayowakabili viongozi wa wanamgambo wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Mathieu Ngudjolo na Germain Katanga katika siku tafauti. Wakati hukumu ya Ngudjolo imepangwa kutolewa Desemba 18,mwaka huu, ile ya Katanga itatolewa hukumu si kabla ya mapema mwakani. Viongozi hao wawili wanakabiliwa na mashitaka ya uhalifu dhidi ya binadamu uliofanywa na wanamgambo waliokuwa chini yao  eneo la Bogoro, Ituri, Mashariki mwa DRC Februari 24, 2003.
Wanachama wa ICC wahitimisha mkutano wao:  Nchi wanachama waliotia saini kuanzishwa kwa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), wamehitimisha mkutano wao Jumatano wiki hii. Katika maazimio yaliyopitishwa na mkutano huo ni pamoja na bajeti ya Euro milioni 112 ikiwa ni chini ya kiwango kilichoombwa na mahakama hiyo ambacho ni Euro milioni 118.
Mwendesha mashitaka ICC achunguzi  waasi wa M23: Mwendesha Mashitaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), Fatou Bensouda alisema Jumatano wiki hii kwamba Mahakama yake itachunguza uhalifu unaodaiwa kufanywa na kundi la waasi la M23, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC). Alionya kwamba matukio ya hivi karibuni yanaashiria kutokea kwa ghasia zaidi katika kanda hiyo. Kundi la M23 linaoongozwa na waasi wa jeshi la DRC wakiwemo Bosco Ntaganda  na Sylvetstre Mudacumura ambao hati za kukamatwa kwao zimeshatolewa na mahakama hiyo.
RWANDA     
Kesi ya Mugesera kuanza kusikilizwa Desemba 17: Mahakama moja nchini Rwanda Jumatatu iliahirisha tena kuanza kusikilizwa kwa kesi ya mauaji ya kimbari dhidi ya mwanasiasa mkongwe nchini humo, Leon Mugesera, aliyerejeshwa kutoka Canada karibu mwaka mmoja uliopita.Majaji wamepanga tarehe mpya ya Desemba 17, mwaka huu kuanza kusikiliza kesi hiyo.Kesi hiyo imeahirishwa kutoa muda zaidi kwa wakili wa mshitakiwa huyo kutoka Kenya iweze kuajiandaa.
WIKI IJAYO
Kesi ya Bemba kuendelea kuunguruma wiki ijayo: Kesi ya utetezi inayomkabili kiongozi wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), Jean Pierre Bemba anayeshitakiwa kwa uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita itaendelea kusikilizwa Jumatatu ijayo, Novemba 26. Uhalifu huo unadaiwa kufanywa kati ya mwaka 2002 na 2003 katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia