SEREKALI IMETAKIWA KUTHIBITI DAWA FEKI

 
washiriki wa semina ya siku mbili ya kujadili masuala m,bali mbali ya kilimo hapa nchini wakiwemo watengenezaji,waagizaji na wasambazaji wa dawa za mimea hapa nchini wakiwa kwenye picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa semina hiyo
Serekali na wadau wa chama wa watengenezaji,waagizaji na wasambazaji wa dawa za mimea na mbegu hapa nchini(CROP LIFE TANZANIA)wameanza kupambana na uingiuzaji wa dawa feki za mazao katika kuongeza thamani ya mazao na kipato kwa mkulima hapa nchini.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa chama hicho hapa nchini Harish Dhutia wakati alipokuwa akiongea na wanahabari kwenye semina ya siku mbili kwa wadau hao pamoja na mwakilishi wa wizara ya kilimo na chakula na mkurugenzi wa TPRI.

Dhutia alisema kuwa kumekuwapo na ongezeko la madawa feki kwenye soko la bidhaa hizo hapa nchini kiasi kuwa kumekuwa kukiwanyima wakulima ongezeko la thamani ya mazao na kipato hivyo wameamua kuanzisha mapambano hayo kudhibiti uingizaji wa dawa feki.

“Unajua udhibiti wa dawa feki za kilimo unahitaji ushirikiano kati ya wadau na serekali na hasa matumizi sahihi ya dawa za kilimo katika kukuza mimea na tusiposhirikiana tutashindwa kufikia malengo ya serekali ya matokeo makubwa sasa katika sekta ya kilimo”alisema Dhutia.

Aidha mwenyekiti huyo alitanabaisha sasa kumekuwepo na matumizi ya vifungashia vya dawa na wakulima wamekuwa wakivitupa ovyo kiasi cha kuharibu mazingira na kuongeza sumu mbalimbali kwenye maeneo yao na kuwa hatari kwa afya za binadamu na mimea hvyo kampeni hii itakwenda sambamba na kutoa elimu kwa wakulima hapa nchini.

Kwa upande wake mkurugenzi wa TPRI alisema kuwa serekali na sheria za kudhibiti ongezeko la dawa feki imekuwa ni tatizo kwao kwani bajeti yao imekuwa finyu katika kudhibiti suala hilo na kuomba serekali kuongeza bajeti ili nao waweze kuingia kwa undani kwenye kudhibiti dawa feki hapa nchini.

Aktanabaisha kuwa serekali ipo makini kwenye suala hilo na kuwa mipango ya kuongeza ongezeko la chakula ipo kweny mpango wa matokeo makubwa sasa unaoendeshwa na srekali hii ni moja ya vipaumbele vya serekali.

Hapa umeona tunaanza na udhibiti wa vifungashia vya madawa hususani makopo ya dawa kwani yamekuwa yakiharibu mazingira na ni sumu kwa binadamu kama hayatawekwa katika mpangilio na kuyaharibu itakuwa tunafanya kazi bure kwenye sekta ya kilimo ambayo ni muhimili wa uchumi wa taifa hili

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia